Wananchi Wanadai Serikali ya Mtaa inahujumu ulipaji wa Fidia kupisha Bandari Kavu, Tunduma Mkoani Songwe

Wananchi Wanadai Serikali ya Mtaa inahujumu ulipaji wa Fidia kupisha Bandari Kavu, Tunduma Mkoani Songwe

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Baadhi ya wananchi Wanaotakiwa kupisha Ujenzi wa Bandarikavu katika eneo la Nandanga, Kata ya Mpemba, Halmashauri ya Mji wa Tunduma, Mkoani Songwe wameilalamikia Ofisi ya Serikali ya Mtaa kushindwa kuwashirikisha katika hatua za Mchakato wa kulipa fidia na kuandikisha watu wasiohusika kwa lengo la kuwalipa fidia.

Wananchi hawa Wanadai Serikali ya Mtaa inahujumu Mchakato wa ulipaji wa Fidia katika eneo hilo kwa kuweka watu wasiohusika, huku wakienda mbali zaidi kuiomba Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kuingilia kati kwa kuitisha mikutano ya hadhara ya kusikiliza kero zao.

TIPSONI NZUNDA Mkazi wa Nandanga. AIZACK MWAMPASHI Mkazi wa Nandanga, HAMIS MSUKWA mkazi wa Nandanga LANGBOSS SICHONE Mkazi wa nandanga wanaelezea

Upande wake Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa, ELISHA MSOMBAanakiri kukosekana kwa nyaraka za umiliki wa maeneo haya wakati wa uhakiki huku anaeleza utaratibu uliotumika.

Licha ya kuishukuru serikali kwa kutoa zaidi ya Bilioni 7 kwaajili ya kulipa fidia kwa wananchi zaidi ya 300 katika mitaa ya Msinde na Nandanga, Diwani wa kata hii, JIMMY MTAWA anasema hajapokea Malalamiko ya Wananchi.

Chanzo: EATV
 
Sisi wakazi wa Hapa Nandanga Hii ni kero kubwa.
Tunachokijua Serikali ilishamaliza kulipa fidia wanufaika wa mradi wa Bandarikavu katika eneo la Katenjele lakini kinachoendelea Huku Nandanga ni eneo ambalo liko
Pembezoni mwa Bandari kavu ambapo kuna Mwekezaji anataka kuchukua Maeneo yetu kwaajili ya Viwanda.
Amewanunua viongozi wa Serikali ili watukandamize Wananchi.

Serikali ilikuwa inanunua maeneo kwa Squaremeter kule katenjele iweje Serikali hiyohiyo inunue Nandanga Bila kufuata Squaremeter et Heka moja Mil 3.

Kibaya zaidi serikali iwaonyeshe watu Maeneo?

Tunaomba vyombo vya Uchunguzi muangalie Swala hili wananchi tunaumia
 
Back
Top Bottom