Wanao sumbuliwa na tatizo la umeme mdogo solution hii hapa!

Transistor

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2013
Posts
1,061
Reaction score
1,637
Umeme mdogo umekuwa kero kwa watu wanao tumia vifaa vikubwa kama vile motor;mafriji n.k

Hata Stabilizer zimekuwa zikishindwa kukabiliana na tatizo hilo

Inafikia hatua vifaa hivyo havifanyi kazi kabisa na hali hiyo ya umeme mdogo imepelekea mara nyingi vifaa hivyo kuungua au kuharibika.

Hiki ni kifaa ambacho kimewasaidia wengi ambao wanaishi maeneo yenye low voltage
kifaa hiki ni Automatic low voltage boostrer





kinaondoa tatizo la umeme mdogo kwa asilimia 99%

Kifaa hiki kinatengenezwa kwa order tu kutokana na vipimo vitakavyo fanyika katika nyumba yako
 
Hiki kimashine kimetusaidia sana nyumbani kwenye mashine ya kupandisha maji
 
Hongera sana, kazi nzuri, sehemu nyingi Tanzania kuna shida ya Low Voltage. data gani unahitaji ili kutengeneza kwa watu walio mbali na Dar? wateja wanaweza kupima na kukutumia oda pamoja na hizo specs.
 
Du kuna jirani yangu alinunua kifaa hiki tena kwa laki tatu, mwaka jana alikuta kinashika moto yaani ni Mungu tu ilikuwa weekend alikuwa nyumbani la sivo tungempa hifadhi Mabwepande
 
Du kuna jirani yangu alinunua kifaa hiki tena kwa laki tatu, mwaka jana alikuta kinashika moto yaani ni Mungu tu ilikuwa weekend alikuwa nyumbani la sivo tungempa hifadhi Mabwepande

Japo sisi hatujawahi kupata tatizo kama hilo ndio maana Kifaa hiki zaidi ya kuwa na overload protection kina temperature protection hiyo yote ni kulinda mambo kama hayo.

Unajua mara nyingi vifaa vya umeme vinaungua kutokana na kukiuka maelekezo ya utumiaji;si hivi tu hata stabilizer nyingi zinaungua moto sababu unakuta kitu cha Watt 1000 mtu anafunga mzigo wa watt 2000,ingekuwa kwa kila mtu kinaungua ingekuwa tatizo la production.

Hata hivyo sisi tulilitambua hilo ndio maana kifaa hicho unacho kiona hapo juu kimewekewa protection za kulinda matumizi yasio takiwa kama ikitokea mteja akazidisha mzigo basi booster itajizima.

Na kitu kingene watu wamekuwa wakinunua stabilizer na kuzitumia kama booster kwenye visima vya maji ,hivyo husababisha zikaungua kwani stabilizer hazijatengenezwa kwa kazi kama hiyo!

Vifaa hivi ni salama,kuna watu kama 37 wamefungiwa na wanaendelea vizuri na wengine guarantee zao zimeisha siku zote hakikisha unafata maelekezo ya matumizi!

Na kuna watu wengine wanazitengeneza hizi bila kuweka security system wanatumia step-up transformer basi hii pia ni sababu ya kiufundi inayoweza kusababisha kifaa kama hiki kuungua!

Kuna mwingine alinunua dukani stabiliza ya watt 5000 ikaja ikaungua sababu tu aliitumia kama booster wakati ile ni stabilizer. Kiutaalamu stabilizer haitakiwi kutumika eneo ambalo lina umeme chini ya volt 110.
 
Hongera sana, kazi nzuri, sehemu nyingi Tanzania kuna shida ya Low Voltage. data gani unahitaji ili kutengeneza kwa watu walio mbali na Dar? wateja wanaweza kupima na kukutumia oda pamoja na hizo specs.

Tunahitaji kujua
1.Voltage Range
2.Flactuation Frequency
3.Appliance Watts
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…