Wanaoamini Yanga haitafuzu, waacheni waamini watakavyo

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
Wanaosema timu yetu haiwezi kufuzu, tukifuzu watakuwa upande wetu na wataelezea kitaalam kwa nini tumefuzu.
.
Kwa hiyo tunaheshimu mawazo yao na tunaomba waendelee kuizungumza timu yetu ili tupate mahali pa kuboresha kutoka kwenye maoni wanayotoa.
.
Hatupo hapa kumzuia mwandishi/mchambuzi yeyote kuizungumzia Yanga.
.
Tupo hapa kushirikiana na vyombo vya habari na wachambuzi kuhakikisha Yanga inakuwa brand kubwa Afrika.... Ali Kamwe.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Hao ni wale mashabiki wachache ambao Ismail Aden Rage wakati fulani, aliwaita mbumbumbu. Mashabiki wa Yanga tunaamini katika falsafa ya mpira ni dakika 90!

Tuna wachezaji wenye uzoefu na haya mashindano! Hivyo lolote linaweza kutokea. Tumeshathibitisha ubora wa kikosi chetu kwenye Ligi ya ndani! Hivyo hata Kimataifa bado tuna nafasi ya kufanya vizuri.

Wanaonuna na wanune. Ila huu ndiyo ukweli wenyewe.
 
Hivi ile ada yenu ya kupokea wageni airport mlikuwa mkiwaza nin ninyi utopolo????
 
Akuna mwenye akili timamu anahangaika na pimbi wa umbumbuni waache wajipe furaha ya muda mfupi
 
Nyinyi ni km mwenge mmeenda kimakosa tu huko...Nyie ni wa hapa hapa tu huko kwingine waachieni SIMBA ....SIMBA .....keshokutwa sio mbali tuombe uhai tu watu tucheke kichapo cha mtani
 
Hivi ile ada yenu ya kupokea wageni airport mlikuwa mkiwaza nin ninyi utopolo????
Hivi natakiwa kujibu maswali ya aina hii kweli mimi ambaye hiyo airport yenyewe tu naiona kwenye tv!!

Mimi nakushauri uwaulize hao wenzako mnaokutana huko airport kuwapokea hao wageni wenu.
 
Mmetoka mkuu haya maneno ya kwenye Kanga hayawasaidii.. mnaenda kule Kwa wadogo Caf..
 
Siyo suala la kutoaamini bali hiyo ni fact kuwa Utopolo wanaenda kupigwa kama dufu kule Sudan
 
Nyinyi ni km mwenge mmeenda kimakosa tu huko...Nyie ni wa hapa hapa tu huko kwingine waachieni SIMBA ....SIMBA .....keshokutwa sio mbali tuombe uhai tu watu tucheke kichapo cha mtani
Tunaendaje kimakosa, na wakati msimu uliopita tulikuwa ni mabingwa wa makombe yote? Uko serious kweli mkurugenzi?

Nadhani nyinyi wenyewe ndiyo mnatakiwa kujitathmini. Maana mlipata hiyo nafasi baada ya kushika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.
 
Hivi natakiwa kujibu maswali ya aina hii kweli mimi ambaye hiyo airport yenyewe tu naiona kwenye tv!!

Mimi nakushauri uwaulize hao wenzako mnaokutana huko airport kuwapokea hao wageni wenu.
Usijitoe ufahamu ni kawaida yenu watopolo kwenda kuwapokea washindani wa Simba.
 
Hahahaha sasa hivi mnaongea kwa busara sana
 
Tunaendaje kimakosa, na wakati msimu uliopita tulikuwa ni mabingwa wa makombe yote? Uko serious kweli mkurugenzi?

Nadhani nyinyi wenyewe ndiyo mnatakiwa kujitathmini. Maana mlipata hiyo nafasi baada ya kushika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.
Watani mm nawaambia huko sudan mmeenda kwa bahati tu na kosa kubwa mmepanda boti ya vibwengo yaaan kichapo mtakacho kipata huko ni aibu yenu wala si ya taifa ..maana SIMBA ndo inawakilisha taifa.
 
Najitahidi kuwa na kichwa kama cha mwendawazimu ili niweze kuamini kuwa yanga atafuzu makundi caf lakini hata kichwa cha mwendawazimu kinagoma!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…