Wanaobeba vifurushi mgongoni huku wakiomba barabarani huwa wanabeba nini?

Wanaobeba vifurushi mgongoni huku wakiomba barabarani huwa wanabeba nini?

Katikati mwa miji nakutana na wabibi wengine wanakuwa ombaomba wamefunga mizigo mgongoni ni kama vipande vya nguo kwenye kanga unakuta anatembea nao huo mzigo mchana kutwa, ile inakuwa ni kitu gani? Mbona kama ni mambo ya kishirikina wanakuwa nayo?

Mimi naogopa sana kumsaidia bibi wa namna hiyo na kuna wale wengine watoto wenye ulemavu wa akili unawakuta stand au sokoni wanaomba mpaka unajiuliza huyu anatumiaje hela, ananunua kitu gani?

Maana kwa hali aliyonayo hata msaada wa chakula atapewa bure na mama ntilie wale itakuwa wanatumwa na watu wakubwa, wamegeuzwa kama misukule.
Wanabeba ID zao
 
Kuna mbibi alivaa ushungi wiki jana aliniomba maji niliyokuwa nakunywa kwenye chupa nikashangaa ila ikabidi nimpe, akauliza ninywe kidogo au nichukue yote nikasema chukua.
Nikasogea mbele nikashtuka, logic ya mtu kuniomba maji niliyokuwa nakunywa. Na mauzo siku mbili zilizofuata yalikuwa mabaya sana nikaona coincidence tu.

Ningefikiria vizuri ningempa hela akanunue mwenyewe
Nimecheka kweli kweli. Nadhani hakuna haja ya kuogopa kwa sababu hawezi kukufanya chochote. Japokuwa inawezekana kabisa alikuwa na nia ovu au alitumwa na mganga kufanya hivyo, lakini kwangu mimi huwa naona watu wa aina hiyo wanapoteza muda tu. Mbaya ni ikiwa utalishwa kitu kwani inaweza kuwa sumu au uchafu mbaya sana. Babu yangu ambaye ni marehemu sasa, kijijini huko, kuna siku alikuwa anatembea njiani, wakati nikiwa mdogo kama miaka 17 hivi, nikaona jirani yetu, mwanamke akamlia timing, na kwenda kuzoa mchanga wa sehemu aliyokanyaga, yaani unyayo ulipokanyaga. Nikaja kumwambia, akacheka kweli kweli na kusema achana naye huyo, mwache azoe mpaka ajaze lori.
 
Kuna Mchaga alienda dodoma akawakusanya wenye ukoma akawaketa dar akawachukulia nyumba mzima kule kiwalani.Basi aliwanunulia wheelchair kila mmoja halafu kila mtu kamuwekea muhasibu Kwa maana yule anayemsukuma,Kila jioni wanaleta hesabu ukizingua unapakizwa ndani ya gari unarudishwa Dom.Mchaga yule anatengeza pesa hatari.
 
Kuna mbibi alivaa ushungi wiki jana aliniomba maji niliyokuwa nakunywa kwenye chupa nikashangaa ila ikabidi nimpe, akauliza ninywe kidogo au nichukue yote nikasema chukua.
Nikasogea mbele nikashtuka, logic ya mtu kuniomba maji niliyokuwa nakunywa. Na mauzo siku mbili zilizofuata yalikuwa mabaya sana nikaona coincidence tu.

Ningefikiria vizuri ningempa hela akanunue mwenyewe
Duh!...maji na pesa ni coincidence tu......

ungempa pesa na mauzo yakawa mabaya ungesema pia ni chuma ulete.
 
Wanabebeaga ballistic missile zakutungulia wanyima omba omba
 
Back
Top Bottom