Wanaodhaniwa kuwa wachawi wanasa Njombe

Wanaodhaniwa kuwa wachawi wanasa Njombe

Jamal Akbar

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2014
Posts
413
Reaction score
471
Wanawake wawili, wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Wamachinga wakazi wa Wilaya ya Makete, mkoani Njombe wanaofanya shughuli zao ujasiriamali mjini Makambako wamezua taharuki mjini Njombe baada ya kuganda ghafla barabarani wakishindwa kusema chochote na kutembea kwa zaidi ya saa moja huku sababu ikitajwa kuwa imetokana na imani za kishirikina.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Njombe, Hamis Issa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo katika eneo la mtaa wa posta Jengo la TRA zamani ambapo amebainisha kuwa akina mama hao ni wakazi wa kijiji cha Lupila wilaya ya Makete lakini wanafanya kazi mjini Makambako.

Kamanda Issa amebainisha kuwa mara baada ya kupata taarifa waliweza kufika na kuwachukua ili kuwafikisha kituo cha polisi lakini mmoja kati yao alitamka neno moja tu YESU na kurudi katika hali ile ile ambapo iliwalazimu kuwapeleka hospitali ambapo madaktari walibainisha kuwa watu hao hawana tatizo lolote la kiafya.

Baadhi ya Mashuhuda wa mkasa huo wamesema waliona wanawake hao wakipita na viatu lakini baada umbali mfupi wakasimama ghafla huku wakishindwa kuongea wala kusogea na pale ambapo watu walijaribu kuwatikisa walikuwa wakilia huku wakitamka maneno Moto Moto!

WhatsApp Image 2023-02-22 at 15.26.01.jpeg
 
Kamanda issa amebainisha kuwa mara baada ya kupata taarifa waliweza kufika na kuwachukua ili kuwafikisha kituo cha polisi lakini mmoja kati yao alitamka neno moja tu YESU na kurudi katika hali ile ile ambapo iliwalazimu kuwapeleka hospitali ambapo madaktari walibainisha kuwa watu hao hawana tatizo lolote la kiafya.
Kama wenyeji waliwagusa wakashindwana nao basi kuna wengi nyuma yao
 
Tukio la kutengenezwa hilo na mganga mpigaji ama mchungaji mpigaji
 
Wanawake wawili, wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Wamachinga wakazi wa Wilaya ya Makete, mkoani Njombe wanaofanya shughuli zao ujasiriamali mjini Makambako wamezua taharuki mjini Njombe baada ya kuganda ghafla barabarani wakishindwa kusema chochote na kutembea kwa zaidi ya saa moja huku sababu ikitajwa kuwa imetokana na imani za kishirikina.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo katika eneo la mtaa wa posta Jengo la TRA zamani ambapo amebainisha kuwa akina mama hao ni wakazi wa kijiji cha Lupila wilaya ya Makete lakini wanafanya kazi mjini Makambako.

Kamanda issa amebainisha kuwa mara baada ya kupata taarifa waliweza kufika na kuwachukua ili kuwafikisha kituo cha polisi lakini mmoja kati yao alitamka neno moja tu YESU na kurudi katika hali ile ile ambapo iliwalazimu kuwapeleka hospitali ambapo madaktari walibainisha kuwa watu hao hawana tatizo lolote la kiafya.

Baadhi ya Mashuhuda wa mkasa huo wamesema waliona wanawake hao wakipita na viatu lakini baada umbali mfupi wakasimama ghafla huku wakishindwa kuongea wala kusogea na pale ambapo watu walijaribu kuwatikisa walikuwa wakilia huku wakitamka maneno Moto Moto!

View attachment 2526308
Wameshindwa kuzungumza ila wakasema yesu na mnajua walipotoka


USSR
 
Una uzoefu sio?

Ndio hayo matukio yanajulikana

Kuna mtu mlandizi aliganda na kiroba hakishuki mgongoni kiuchawi. Polisi wakambananisha wakagundua ni mganga alimpanga

Njombe pia kuna bibi alikutwa juu ya bati na kaniki kuzuga ni uchawi. Walivyombananisha wakagundua alipangwa na nabii mpigaji.

Matukio hayo yapo kibao na post zake zimo humu jamiiforums
 
Hello!

Sisemi neno ila Moja,tudumishe na kukuza sayansi zetu za asili..

 
Back
Top Bottom