Mkumbwa Jr
JF-Expert Member
- Mar 23, 2016
- 2,668
- 3,751
Miaka ya hivi karibuni viongozi wa umma wameingiwa na tabia ya kusifu na kushangilia hovyo.
Kupitia mitandao ya kijamii tunashuhudia wakurugenzi na wakuu wa wilaya wakijisifia ujenzi wa madarasa kana kwamba nikitu ambacho hakikua kinawezekana.
Hao hao viongozi wameandamwa na msiba wa shule za umma kufelisha ikilinganishwa na zile za binafsi.
Kupitia mitandao ya kijamii sijaona hata mkurugenzi mmoja au mkuu wa wilaya aliyegusia huu msiba mzito wa watoto kupata zero.
Viongozi badilikeni acheni tabia ya kusifiasifia mambo ya kawaida hata pale ambapo mtu anatimiza wajibu wake. Ujenzi wa madarasa nijukumu la serikali. Kwanini mnasifu kupita kiasi kana kwamba mmeoewa msaada kutoka jamii nyingine?
Nimeshangaa sana kuona eti mkurugenzi anaingia darasani na kuanza kusema mama Samia Suluhu hoyeeeee wanafunzi wanaitikia......hii ilikua mkoani kagera nadhani. Hili limekaa kisiasa zaidi kuliko kitaaluma.
Watanzania tubadilike. Tuache ushabiki wenye lengo la kuneemesha na kupalilia zaidi teuzi hata pale pasipo stahili.
Viongozi sasa baada ya kujenga madarasa mjipange watoto wapate elimu bora na zero zipungue kwa kiasi kikubwa kama sio kuisha.
Hebu jutieni hizo sifuri ambazo hata nyie mnao mchango hata kwa asilimia ndogo
Msijitoe ufahamu kufanya sherehe ya madarasa wakati manao msiba wa kufelisha. Badilikeni
Kupitia mitandao ya kijamii tunashuhudia wakurugenzi na wakuu wa wilaya wakijisifia ujenzi wa madarasa kana kwamba nikitu ambacho hakikua kinawezekana.
Hao hao viongozi wameandamwa na msiba wa shule za umma kufelisha ikilinganishwa na zile za binafsi.
Kupitia mitandao ya kijamii sijaona hata mkurugenzi mmoja au mkuu wa wilaya aliyegusia huu msiba mzito wa watoto kupata zero.
Viongozi badilikeni acheni tabia ya kusifiasifia mambo ya kawaida hata pale ambapo mtu anatimiza wajibu wake. Ujenzi wa madarasa nijukumu la serikali. Kwanini mnasifu kupita kiasi kana kwamba mmeoewa msaada kutoka jamii nyingine?
Nimeshangaa sana kuona eti mkurugenzi anaingia darasani na kuanza kusema mama Samia Suluhu hoyeeeee wanafunzi wanaitikia......hii ilikua mkoani kagera nadhani. Hili limekaa kisiasa zaidi kuliko kitaaluma.
Watanzania tubadilike. Tuache ushabiki wenye lengo la kuneemesha na kupalilia zaidi teuzi hata pale pasipo stahili.
Viongozi sasa baada ya kujenga madarasa mjipange watoto wapate elimu bora na zero zipungue kwa kiasi kikubwa kama sio kuisha.
Hebu jutieni hizo sifuri ambazo hata nyie mnao mchango hata kwa asilimia ndogo
Msijitoe ufahamu kufanya sherehe ya madarasa wakati manao msiba wa kufelisha. Badilikeni