Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 301,577
- 754,412
Hili sijui ni la Waziri wa Afya ama mazingira ama wote wawili?
Kuna uchafuzi mkubwa sana kwenye barabara za Dar es Salaam pamoja na mifereji na mitaro yake unaofanywa na makampuni yaliyopewa kandarasi za kusafisha barabara za jiji mitaro na mifereji yake na wahusika wala hawagutuki ama kuchukua hatua.
Je hii inatokana na kupeana kandarasi kwa kujuana ama kwa rushwa? Wafanyakazi wa makampuni husika wanapofagia michanga barabarani hukuisanya na kuihamishia kwenye hifadhi na kingo za barabara ambazo nyingine zina bustani nzuri za maua.
Wafanyakazi wa makampuni husika wanaposafisha mitaro na mifereji pembezoni mwa barabara lile tope hurundikwa pembezoni, kingoni na kwenye hifadhi za barabara mifereji na mitaro
Matokeo yake ni nini?
Ni kuharibu mandhari nzuri za hifadhi za barabara zenye bustani nzuri kuchafua na kuharibu kingo za barabara
Kuchafua na kuharibu mitaro na mifereji iliyojengwa kwa gharama kubwa. Kutengeneza vilima vya uchafu kwenye hifadhi za barabara, mifereji na mitaro.
Soma Pia: Kariakoo kuna chemba zinatema maji machafu na kuhatarisha afya za Watu, Viongozi wapo kimya
Kusababisha baadhi ya mitaro na mifereji kufurika ama kuziba wakati wa mvuta kutokana na uchafu mwingi uliowekwa pembezoni kurudi kwenye mtaro ama mfereji, Kusababisha magonjwa ya milipuko hasa nyakati za mvua.
Wakandarasi wanaopewa hizi tenda wanalipwa pesa za, Kufagia, Kusafisha, Kukusanya na kwenda kutupa taka ama uchafu kwenye maeneo rasmi yaliyotengwa kwa shughuli hizo. Kinachoshangaza ni kwamba huo mtiririko wa hizo Kazi haifanyiki kwa usahihi na kwa ukamilifu pengine kutokana na uzembe, uvivu, kutojali, kutofuatiliwa
Ukosefu/uhaba/uhafifu/uchache wa vitendea Kazi na wafanyakazi mahiri wenye ujuzi
Mamlaka husika zipo zinaona, wahusika wapo, wakaguzi wapo lakini hakuna uwajibikaji hata kidogo na kila mwisho wa tenda mtu hupewa hati safi, kulipwa na kupewa tena tenda nyingine mpya! Hii kero iwafikie washika dau Wote. Wizara ya afya, Wizara ya mazingira (kama ipo), Mamlaka ya jiji, Serikali za mitaa Wakandarasi wa usafi, Wananchi katika ujumla wao!
Nawakilisha!
Kuna uchafuzi mkubwa sana kwenye barabara za Dar es Salaam pamoja na mifereji na mitaro yake unaofanywa na makampuni yaliyopewa kandarasi za kusafisha barabara za jiji mitaro na mifereji yake na wahusika wala hawagutuki ama kuchukua hatua.
Je hii inatokana na kupeana kandarasi kwa kujuana ama kwa rushwa? Wafanyakazi wa makampuni husika wanapofagia michanga barabarani hukuisanya na kuihamishia kwenye hifadhi na kingo za barabara ambazo nyingine zina bustani nzuri za maua.
Wafanyakazi wa makampuni husika wanaposafisha mitaro na mifereji pembezoni mwa barabara lile tope hurundikwa pembezoni, kingoni na kwenye hifadhi za barabara mifereji na mitaro
Matokeo yake ni nini?
Ni kuharibu mandhari nzuri za hifadhi za barabara zenye bustani nzuri kuchafua na kuharibu kingo za barabara
Kuchafua na kuharibu mitaro na mifereji iliyojengwa kwa gharama kubwa. Kutengeneza vilima vya uchafu kwenye hifadhi za barabara, mifereji na mitaro.
Soma Pia: Kariakoo kuna chemba zinatema maji machafu na kuhatarisha afya za Watu, Viongozi wapo kimya
Kusababisha baadhi ya mitaro na mifereji kufurika ama kuziba wakati wa mvuta kutokana na uchafu mwingi uliowekwa pembezoni kurudi kwenye mtaro ama mfereji, Kusababisha magonjwa ya milipuko hasa nyakati za mvua.
Wakandarasi wanaopewa hizi tenda wanalipwa pesa za, Kufagia, Kusafisha, Kukusanya na kwenda kutupa taka ama uchafu kwenye maeneo rasmi yaliyotengwa kwa shughuli hizo. Kinachoshangaza ni kwamba huo mtiririko wa hizo Kazi haifanyiki kwa usahihi na kwa ukamilifu pengine kutokana na uzembe, uvivu, kutojali, kutofuatiliwa
Ukosefu/uhaba/uhafifu/uchache wa vitendea Kazi na wafanyakazi mahiri wenye ujuzi
Mamlaka husika zipo zinaona, wahusika wapo, wakaguzi wapo lakini hakuna uwajibikaji hata kidogo na kila mwisho wa tenda mtu hupewa hati safi, kulipwa na kupewa tena tenda nyingine mpya! Hii kero iwafikie washika dau Wote. Wizara ya afya, Wizara ya mazingira (kama ipo), Mamlaka ya jiji, Serikali za mitaa Wakandarasi wa usafi, Wananchi katika ujumla wao!
Nawakilisha!