Wanaofanyakazi ya kupamba kumbi za starehe, kusherehesha (Ma-MC), wapishi wa sherehe na wapiga picha, watatakiwa kulipa ada na ushuru

Wanaofanyakazi ya kupamba kumbi za starehe, kusherehesha (Ma-MC), wapishi wa sherehe na wapiga picha, watatakiwa kulipa ada na ushuru

Waelekeze nguvu misibani..maana misiba ni mingi siku hizi kuliko sherehe...maana misiban nako kuna sound,cameras,magari ya kukodi ya misiba,ukumbi/uwanja. Hii itapunguza watu kufia gest
 
, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]kweliiii
Waongeze na tozo ya parking 100,000/= kwa kila tukio.

Tozo ya mazingira (uchafu/pollution) 100,000/=

Tozo ya kuacha kufanya kazi na kwenda kwenye sherehe 200,000/= kwa kila tukio.

Nasema uongo ndugu zangu?
 
Waelekeze nguvu misibani..maana misiba ni mingi siku hizi kuliko sherehe...maana misiban nako kuna sound,cameras,magari ya kukodi ya misiba,ukumbi/uwanja. Hii itapunguza watu kufia gest
kwan bang imeruhusiwa 😂😂😂😂
 
Tuangalie tusifishe moyo wa KUJIAJIRI. Wanaopanga kodi wafikirie madhara yatakayoweza kujitokeza. Kwa vingine shughuli za kiuchumi zitapungua, na madhara yake ni makubwa mno.
 
Itakuwaje huduma hizo zikitolewa msibani?
Au na kuwaita msibani lazima kupata kibali cha Halmashauri.
Tuelimishane tusije kufanya nakosa bila kufahamu.
 
Aiseeee tumefikia kubaya, hata kama ni kukusanya kodi imekuwa too much.
 
Gharama hizo zote zitarudi kwa kwa mwenye shughuli, kamati, hivyo wachangiaji ambao ni wananchi
 
Sasa ivi kila Wizara imekuwa TRA inakusanya mapato......
Hazitoi tena huduma zinakusanya Pesa........


MitanoTena
 
WATU wanaofanyakazi ya kupamba kumbi za starehe, kusherehesha (Ma-MC), wapishi wa sherehe na wapiga picha, watatakiwa kulipa ada na ushuru.

Ni baada ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema jijini Mwanza, kupitisha sheria ndogo za ada na ushuri ambazo tayari zimepata baraka za Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).

Barua iliyosainiwa na Emmanuel Kaponoke, Afisa Utamaduni wa halmashauri hiyo ya tarehe 15 Januari 2021 kwenda kwa walengwa, inabainisha ada hizo.

Washereheshaji (MC) watapaswa kulipa Sh.50,000 kwa sherehe moja huku wapambaji kumbi za burudani/sherehe watalipa Sh.30,000.

Wamiliki wa kumbi, unaochukua watu kati ya 100-200 ni Sh.50,000 kwa siku, ukumbi unaochukua watu kati ya 201-500 atalipa Sh.100,000.

Wapishi wa vyakula kwa siku moja ya tukio atapaswa kulipa Sh.30,000 na wapiga picha za video na mnato watapaswa kulipa Sh.30,000 huku muziki ikiwa ni Sh.30,000

“Kamwe, mmiliki wa ukumbi asiruhusu sherehe kufanyika ndani ya ukumbi wake bila kibali cha halmashauri,” inaeleza sehemu ya barua hiyo

“Ikumbukwe, ada hii ni kwa ajili ya kubali cha halmashauri tu na si gharama ya kukodi ukumbi.”

Wilaya ya sengerema haipo jiji la mwanza
 
Waongezee na hii....

-kila chombo Cha usafiri kitakayoshiriki Kwenye msafara wa maharusi
- gari = 50,000
-bajaji= 30,000
-pikipiki= 20,000
-baskeli= 10,000
Viatu vilivyo kwenye miguu viwe 5000
 
Waongeze na tozo ya parking 100,000/= kwa kila tukio.

Tozo ya mazingira (uchafu/pollution) 100,000/=

Tozo ya kuacha kufanya kazi na kwenda kwenye sherehe 200,000/= kwa kila tukio.

Nasema uongo ndugu zangu?
Aaawapi, husemi uongo mkuu.
Mitano tena au uongo jamani?
 
Hao madiwani wa uko Sengerema watakuwa hawajielewi kabisa,Watakuwa wameiga katiba ya madiwani wa Jiji na manispaa zilizopo dar,uku dar wakisema wapambaji,na ma-mc na wenye kumbi ni sawa,Sasa uko Sengerema kuna nini cha ajabu
 
Tatizo watanzania tulizoea kuishi kiujanja ujanja Ndio maana tunaumia
Tii sheria bila shuruti
Lipa kodi
Utafaidi matunda ya awamu hii ya Rais mwema mwenye Moyo wa huruma na upendo kwa RAIA wake
Vinginevyo utaumia sana maana mianya ya wapiga dili imeziba kabisa
Kuna wendawazimu hudhani kuwa kumtoza mwananchi kodi ni kumnyima haki yake. Wasomi wetu wengi middle class wanajaa mitandaoni hapa kutuaminisha kuwa waandaaji sherehe na ma-mc ni masikini sana hawapaswi kulipa kodi.

Maisha ya wasomi wengi yamefungwa kwenye kijiboksi kinaitwa mshahara. Anadhani kila asiye na mshahara hana kipato kisichostahili kulipa kodi. Hii ndiyo sababu serikali duniani kote huwatumia kama chanzo cha uhakika cha mapato. Unampa kazi kisha unaanza kuchukua kodi rahisi kuliko zote.

Mimi kwenye shughuli yangu ya ufugaji, hudili na hawa watu wa sherehe au shughuli! Mnyonge anayedhani hawa watu ni wanyonge kama yeye ajilaumu yeye na ujinga wake.

Kila Mtanzania anapaswa kulipa kodi,ili mradi tu iwe "good tax".
 
Naona wamewasahau wale wanaokidishwa kuja kusherehesha na kutingisha makalio kwenye sherehe za watu...

Walipe kodi kwa matendo yao...




Cc: mahondaw
 
Wamebakiza kutoza kodi Mbingu pale Mvua zinaponyesha
 
Back
Top Bottom