Wanaokuja kuishi Dar wapewe semina elekezi

Wanaokuja kuishi Dar wapewe semina elekezi

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Katika utafiti mdogo niliofanya hapa Dar es Salaam nimegundua kuwa changamoto za mji huu haziishi na kwa kiasi kikubwa ni zile zile miaka yote kwa kuwa wakaazi wa mjii huu, hasa wale wageni hawataki kubadilika.

Leo nimepita barabara ya Bagamoyo maeneo ya Mbezi, nikaona mdada mmoja anamwaga mihogo mchana kweupe katika njia ya watembea kwa miguu kiasi cha kufunga eneo zima kitendo kitakachowalazimu watembea kwa miguu kuingia barabarani ili kupita eneo lile maana njia ameifunga.

Nikajiuliza, si ni juzi tu kulikuwa na zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara wa aina hii? Kuna vituo vya daladala sasa hivi vimegeuzwa ni sehemu za biashara, si machungwa, karanga, matikiti hadi mahindi yanachomwa. Unaweza kuona hali na mbaya kuliko hata kabla zoezi hili lilipofanyika.

Kuna hii dhana ya kuwa tusizibiane riziki. Najua kuna watu watakuja katika uzi huu na mtazamo huo. Lakini kwa mfano nilioutoa wa huyo muuza mihogo, angeweza kabisa kuweka biashara yake upande wa pili bila kubughudhi taratibu na usalama wa wengine, hili ndiyo lilinitatiza. Hawa watu hawaoni tofauti ya shambani na mijini.

Mji huu wa Dar baada ya miaka hii yote, kuna watu wengi sana wamestaarabika na wangependa kuishi katika mazingira ya kistaarabu na yote haya yanawezekana bila kuzuia mtu yoyote kutoka sehemu yoyote kuishi na kufanya biashara zake kwa kufuata taratibu.

Tatizo kubwa ninaloliona ni kuwa wengi wa watu wanaotoka vijijini wanakuja mijini na mitazamo ile ile ya huko walikotoka na wanalazimisha wengine wasalimu amri kwao. Na watu hawa hata wakae Dar miaka 20 hawezi kubadilika maana wakuja wapya wanaendeleza hizi taratibu na hivyo kushinikiza muendelezo wa fikra mbaya.

Nimeleta mada hii huku nikiheshimu harakati za kila mtu za kujitafutia riziki na pia napenda sana mchanganyiko wa mji wa Dar es Salaam ambapo hatuulizani makabila wala tulipotoka ila inahitaji nguvu ya ziada kuleta ustaarabu mjini hapa.

Hawa watu inabidi wakifika Chalinze, washushwe, wakalishwe kama wiki hivi pale wafundishwe taratibu za kuishi mijini zilivyo. Bila kufanya hivyo, huu mji hautabadilika kamwe nawaambia.
 
😅😂 unaita wenzako wageni kwasabab wewe umezaliwa Dar, umesomeshwa na wazaz wako shule za kata ukabahatika kufikw chuo umemaliza sasa hivi upo kwenu unakula bure unalala bure choo bure,

kwahio huwez kuona hao wageni wanajishughurisha ili wapate pesa za kumudu familia zao, baada ya miezi miaka kupita hao unaowaita wageni wanao fanya biashara ndogo ndogo wanatajirika wanawaacha nyie wenyeji mnalamba lips mnatoboa masikio mnakunywa alkasusu na kuomba bia ktk ma bar... Vijana wa Dar mna akili finyu sana...

Unadhan serikal yako ingeandaa mazingira mazur kwa wafanya biashara wadogo unadhan ungewaona wametapakaa barabarani...?

Halafu tatzo lako huna exposure tu, nenda hata London, New York, Paris etc utawakuta wafanyabiashara wadogo wameweka vitu vyao barabarani pamoja kwamba hairuhusiwi but sometimes maisha yanalazimisha kukubaliana na hali...

Think positive kijana
 
Sahihi kabisa ndugu. Tena wapewe semina Kali na ikishindikana arudishwe mkoani/kijijini kwao. Wachina wao kwao uwezi ingia mijimikubwa kufanya maisha kama huko kwenu ulipo Toka kama haujafika viwango flani vya (kazi ustarabu. na Heshima)
 
Katika utafiti mdogo niliofanya hapa Dar es Salaam nimegundua kuwa changamoto za mji huu haziishi na kwa kiasi kikubwa ni zile zile miaka yote kwa kuwa wakaazi wa mjii huu, hasa wale wageni hawataki kubadilika...
Dah!Hata Paris ukienda haupewi semina elekezi ya kuishi aisee!DSM watu wengi wamevurugwa na hali ngumu ya maisha.

Muwe mnajipa hata likizo ya lazima mje huku vijijini kwetu mpumzike miezi miwili.Zawadi mtakazotuletea ni mikate tu.

Mnapoondoka tutawafungashia unga,mchele,maharage na hata kuku wazimawazima.Maana mmezoea utapeli na unyang'anyi.😂😂😂😂
 
Dah!Hata Paris ukienda haupewi semina elekezi ya kuishi aisee!DSM watu wengi wamevurugwa na hali ngumu ya maisha.Muwe mnajipa hata likizo ya lazima mje huku vijijini kwetu mpumzike miezi miwili.Zawadi mtakazotuletea ni mikate tu.Mnapoondoka tutawafungashia unga,mchele,maharage na hata kuku wazimawazima.Maana mmezoea utapeli na unyang'anyi.😂😂😂😂
Usisahau na misasati na mikusu🤣
 
God did
Dsm Ni jiji la kawaida Sana
I'm feel sorry and fa*ck for those who writes shites
 
😅😂 unaita wenzako wageni kwasabab wewe umezaliwa Dar, umesomeshwa na wazaz wako shule za kata ukabahatika kufikw chuo umemaliza...
Hao wanaofanya hivyo huko New York na Paris ni hawa hawa waliweza kupenya wakafika huko wanaendeleza tabia za kuishi bila kufuata taratibu zilizowekwa.
 
Mchg. Mgogo alishauri ifungwe machine pale terminal kwajili ya kuscan vichwa vya wageni na akili zao watu wakamwona mzushi
Haya mambo tunayasema tunaonekana tunatania au hatujali harakati za maisha za wengine wakati wahusika wao hawajali wengine. Yaani yule dada anamwaga mihogo kama vile yuko sebuleni kwake!
 
Fedha za tozo zitagharamia.
Asa izo fedha za tozo ndo zitumike kwenye ushubwadu kama huu usiokua na kichwa wala miguu? Si bora zigharamie madawa uko hospitalini watu wanakufa kwa kukosa dawa.

Halafu unajuaje labda huo unaouona sio ustaarabu kwetu ndo ustaarabu wenyewe huo. Ustaarabu fundisheni watoto zenu uko watakua nao mjini kla mtu yupo na mishe zake za kusaka tonge
 
Asa izo fedha za tozo ndo zitumike kwenye ushubwadu kama huu usiokua na kichwa wala miguu? Si bora zigharamie madawa uko hospitalini watu wanakufa kwa kukosa dawa. Alaf unajuaje labda huo unaouona sio ustaarabu kwetu ndo ustaarabu wenyewe huo. Ustaarabu fundisheni watoto zenu uko watakua nao mjini kla mtu yupo na mishe zake za kusaka tonge
Mimi sijaunga mkono semina elekezi ya namna ya kuishi "Ndalisalama" isipokuwa nimeshauri tozo zigharamie.Nia yangu watu wote wahamie Daslam kupata hiyo tuisheni.
 
Back
Top Bottom