Wanaolalamikia Uteuzi wa Wakuu wa Wilaya tuongee hapa kidogo

Wanaolalamikia Uteuzi wa Wakuu wa Wilaya tuongee hapa kidogo

Tee Bag

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2013
Posts
7,220
Reaction score
5,622
Kuna watu wanalalamika kuhusu Uteuzi wa Ma DC. Hebu tuongea Kidogo hapa.....

Na Thadei Ole Mushi

1. Kuwa Mwigizaji au Msanii Hakukunyimi kuwa na sifa za kuwa Kiongozi. Tena Mwigizaji anaweza kuwa Kiongozi mzuri. Kinachoangalia ni uwezo wake katika kufanya vitu. Nilisema wiki Chache hapa zilizopita ni vigumu Sana kufanya vetting kwa vijana wanaosifia tu kuanzia January hadi December. Watu wanahoji why Nick wa Pili lakini niwaambie Nick ni msomi mzuri Sana na ameshaonyesha kuwa ana kitu Cha Ziada. Niliwahi kuandika kuhusu Chine's Mediocrity kuwa ili uwe Kiongozi angalau lazima uwe una kitu ulishakifanya Nick na Mchopanga kawapita wengi katika Hili tuwaacha tuwapime katika Majukumu.

2. Issue ya Uteuzi wa Rais ni kwamba Rais huangalia yupo comfortable kufanya Kazi na nani. Kumbukeni hawa ni wawakilishi wake..... Ukiachana na masuala ya Vetting Rais hupenda kufanya Kazi na watu anaoona kuwa hawa wanamfaa katika mazingira anayoyataka yeye. Hapa Kuna Utashi binafsi wa Rais.

3. Kuhusu Vijana wa Upinzani kuteuliwa ni jambo Zuri. Ni Kweli kwamba kwa siku za karibuni nimekuwa nikisema kuwa hawa vijana wanaotokea upande wa Pili wanapimika na Mara nyingi wapo Smart sana kuliko huku kwenye Jembe na Nyundo. Kitalu Chao kipo vizuri Sana na hapa ndipo HUWA nasema screening ya Vijana wa CCM Izingatie weledi sio Uchawa. Niliwahi kushauri kuwa CCM ianze kuchukua vijana walio machachari Kutoka vyuoni kama wanavyofanya Chadema badala ya kuwachukia na kuwaacha wakaangukia kwenye mikono ya Upinzani.

4. Kwa wale ambao BADO Wana matumaini ya kuwinda U DED na U DAS waanze kufikiria Kazi nyingine za kufanya. Ipo hivi Para A1 (21) ya Standing Orders ya 2009 kama kanuni za kudumu za Utumishi wa Umma........inasema "District Administrative Secretary" means a public servant in-charge of administration in a district; Ikimaanisha kuwa ni mtumishi wa umma atakayewajibika na shughuli za kiutawala ofisi ya Mkuu wa Wilaya.....Kwa kifupi kabisa huyu ni mtumishi wa umma ambaye upatikanaji wa upo wazi kabisa. Mama SAMIA anaonekana kuwa mfuasi mzuri wa kanuni na Sheria za nchi. Hivyo kama haupo kwenye Utumishi wa Umma hadi sasa maana yake U-DAS na U- DED ushakupita. Anza kutafuta Kazi nyingine ya kufanya kama Polepole anavyosema kwenye video hii [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

6. Angalau sasa Mwenyekiti na Katibu wa UVCCM wamegraduate toka ngazi Moja kwenda nyingine. Nimekuwa nikisema Sana kuhusu hii kumuiya kutoivisha viongozi watakaograduate kutoka level Moja kwenda nyingine nikifanya Comparison na Chama kikuu Cha Upinzani. Kwa Miaka kadhaa hawa vijana walikuwa baada ya Utumishi wao kwenye kumuiya ya Vijana walikuwa wakipoteza kabisa kwenye Ramani tunao kina Sadifa, Beno Malisa na wengineo hawajulikani wapo wapi huku kina Katambi, Henge na wengineo wakigraduate. Haya ni mafanikio ya UVCCM inaanza angalau kuivisha viongozi wa Kutumika maeneo mengine.

6. Naongea Sana kuhusu Self Actualization kwa vijana. Taifa letu limekumbwa na pepo la kila Mtu kutaka kuitwa Mheshimiwa. Kwa mataifa mengine hasa yaliyoendelea vijana hawana thinking hiyo. Wengi Wana matamanio ya kutimiza Ndoto zao kwenye biashara, Kwenye fani walizosomea nk. Kama vijana wakilielewa Hili wanaweza kulisaidia Taifa vizuri zaidi kuliko kuwaza kuteuliwa. Na hapa ndipo ninapotaka wengi wadondoshe dhana ya UCHAWA wavae uhalisia wao na waonyeshe Wana vitu Gani vya Ziada.

7. Ni makosa makubwa kudhani kigezo Cha kuteuliwa ni Kumtukana Mbowe na Chadema au ni kuimba nyimbo za kampeni Sana, au ni kusifia Tu. Kuna mambo mengine ya msingi ambayo huangaliwa. Ndio maana unaona sura Mpya ambazo hazijawahi kusema hata CCM hoyee mahali.

8. Soon tutaanza kuona Sura halisi za watu, Expectations sasa zimeisha kabisa. Akili zitarudi kwenye fuvu la kichwa. Lilikuwa ni Suala la Muda tu.

Tufundishane Adabu

Ole Mushi
0712702602.
 
Ishu ni kupata kujihakikishia kipato na ndomaana wateuliwa huwa hawalalamiki kwanini wameteuliwa ila tu wale walokosa..tuongeze network za kujuana IPO siku tutaonwa na wakaribu wakiwa in charge
 
Badala kuteua teua sehemu kubwa ya uongozi ipatikane kwa uchaguzi huru
 
Mimi binafsi sitaki na sijawahi kuwaza kuteuliwa wazazi wangu kuwa serikalini miaka mingi imetosha kuona maisha yao na kunipa msukumo nijiajiri mwenyewe.

Maisha ya kutumwa na kuelekezwa kila muda ndio kitu sipendi nataka kutumia brain yangu kufanya maamuzi na kazi bila kushurutishwa na mtu yeyote.

Uhuru wangu na kufanya kazi kwa ubunifu ni kitu bora sana kuliko cheo cha miaka 5 hii inanifanya nisibweteke na kufanya kazi kwa kuzingatia professional yangu na ya wenzangu ninao Fanya nao kazi.

Kuheshimu makampuni mengine ninayoshirikiana nayo na watu wake kuwa mtu wa kujifunza kuwa mahali popote muda wowote Je ukinipeleka kalambo kuwa mkuu wa wilaya nitajifunza sangapi? Zaidi ya kupotezeana muda miaka 5

Cheo pekee ninachoweza kukubali kukitumikia ni kuwa Rais, Makamo Wa rais au waziri mkuu ili kuleta changes za kweli katika nchi otherwise siwezi kutamani cheo chochote cha kuteuliwa.
 
Kwa cheo cha Mkuu wa Wilaya hata Stive Nyerere sawa tu. Taabu kwa DED hapo ndo nasubiri kuona uhalisia na mwelekeo wa serikali. Humo nikiwakuta kina JB nitajua tumepigwa.
 
Good points, but no. 2 sikubaliani nayo, rais achague watu wenye tija katika kujenga nchi, hata kama hayupo comfortable nao, otherwise ndio kujaza watu wa ndio mama.
 
Back
Top Bottom