Wanaomaliza vyuo vikuu kipindi hiki cha awamu ya tano mpaka nawaonea huruma. Ajira zote zimezimwa kana kwamba nchi imesimama

Ifike mahali sasa watu wajiulize wanaenda vyuoni kusoma ilia kupata kazi au kuongeza maarifa tu.
 
Jiongeze bana....
unalia lia kuajiriwa....!!??
na ajira hakuna....
 
Kwa muhitimu wa chuo kikuu kukosa kuajiriwa au kujiajiri ni aibu kwa mfumo wetu wa elimu.Itakuwaje kwa wahitimu wa vyuo vidogo ,shule za sekondari na shule za msingi?
 
Mimi nimegraduate tangu 2016 nikiwa na miaka 26 mpaka leo nimefikisha miaka 31 bila bila.

Shetani [emoji216] kakanyaga waya.
Nimegraduate na wewe at the same time and age. Ila fikra yangu ya kuajiriwa ilitoka toka nipo mwaka wa kwanza chuo. Hasa baada ya kusoma vitabu vya rich dad poor dad. Sasa hivi maisha yangu namshukuru Mungu nina familia tyar na sifikirii kuajiriwa. Na sijutii maamuzi yangu.
 
Ni maamuzi sahihi. Ila kwasasa ni kipindi kigumu sana hata kwa waliojiari.

Siwezi kusema huwezi kufanya progress yoyote, ila kama ulipaswa kupiga hatua 10, ukikaza sana utapiga hatua 2 tu.

Hata mimi siyo kwamba nimekaa tu home namsubiria roho wa Mungu amshukie Magufulu, hapana.

Kuna shughuli nafanya, nalipa kodi ya Serikali, ya nyumba, home mama nampa chochote na ndoto zangu bado ziko hai kabisa.

But, kwa sisi ambao ndio freshers na tegemeo kubwa kwenye familia zetu, ajira ingekuwa booster kubwa mnoo.
 
[emoji23][emoji23]dah kwa kweli acha tu nicheke.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…