SANCTUS ANACLETUS
JF-Expert Member
- Mar 5, 2016
- 3,338
- 4,676
- Thread starter
-
- #201
Kuna wapuuzi mpk leo wanatetea ujinga huu? Kweli shetani bado hajafa loh! Padre yeye ni “mtu” kama Yesu? Kuomba msamaha kwa uliyemkosea (mtu mwenzako) ni sahihi. Tatizo nnaloliona ambalo walokole tungependa kujua ni maombi ya ‘via’ kw Padre ndipo akupelekee kwa Mungu.
Ikiwa binadam baada ya dhambi amepungukiwa, padre ni nani mpk asiwe ‘binadamu?’
Yohana mbatizaji alipokuwa anawaondolea watu dhambi alikuwa Mungu? Hebu soma Matayo 3:1-6:
“1Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema,2 Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. 3 Kwa sababu huyo ndiye aliyenenwa na nabii Isaya, akisema, Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.4 Naye Yohana mwenyewe alikuwa na vazi lake la singa za ngamia, na mshipi wa ngozi kiunoni mwake; na chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu. 5 Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani; 6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi”.