Wanaopinga kuungama dhambi kwa Padri, ndio wapinga Kristo wanaohubiriwa na wasabato na ndio wale wanaosoma maandiko kwa kurukaruka.

Wanaopinga kuungama dhambi kwa Padri, ndio wapinga Kristo wanaohubiriwa na wasabato na ndio wale wanaosoma maandiko kwa kurukaruka.

Kuna wapuuzi mpk leo wanatetea ujinga huu? Kweli shetani bado hajafa loh! Padre yeye ni “mtu” kama Yesu? Kuomba msamaha kwa uliyemkosea (mtu mwenzako) ni sahihi. Tatizo nnaloliona ambalo walokole tungependa kujua ni maombi ya ‘via’ kw Padre ndipo akupelekee kwa Mungu.

Ikiwa binadam baada ya dhambi amepungukiwa, padre ni nani mpk asiwe ‘binadamu?’

Yohana mbatizaji alipokuwa anawaondolea watu dhambi alikuwa Mungu? Hebu soma Matayo 3:1-6:


“1Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema,2 Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. 3 Kwa sababu huyo ndiye aliyenenwa na nabii Isaya, akisema, Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.4 Naye Yohana mwenyewe alikuwa na vazi lake la singa za ngamia, na mshipi wa ngozi kiunoni mwake; na chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu. 5 Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani; 6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi”.
 
Siyo Bwana aliyewapa huo uwezo sema kanisa katoliki ndiyo limewapa Mungu hawezi kumpa mwanadamu uwezo wa kumsamehe mwanadamu mwenzie dhambi kanisa katoliki mnafanya makufuru maana hiyo kazi ni ya Mungu pekee

Tatizo ni kwamba hamkusoma vizuri Lugha mashuleni kwenu na hivi msomapo lolote mnaambulia patupu. Ukisoma nukuu hii hapa chini utagundua kuwa kuna watu wa aina ya uelewa wako waliokuwa wanaelewa kwamba mwanadamu hana uwezo wa kuondoa dhambi isipokuwa Mungu.Ni katika mktadha kama huo Yesu anasema wanadamu wanao huo uwezo na mamlaka.Mkazo nimuokoleza katika aya ya 10:

5Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza,“Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.” 6 Baadhi ya waalimu wa sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao, 7 “Anathubutuje kusema hivyo? Anamkufuru Mungu! Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake.” 8 Yesu alitambua mara mawazo yao, akawaambia, “Mbona mnawaza hivyo mioyoni mwenu? 9 Ni lipi lililo rahisi zaidi: Kumwambia mtu huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kumwambia, ‘Inuka! Chukua mkeka wako utembee?’ 10 Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anayo mamlaka ya kuwasamehe watu dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, 11 “Nakuambia simama; chukua mkeka wako uende nyumbani!”
 
Hahahaha mtoa mada nikajuaga dini yako imekamilika kumbe ni majanga tu hadi imekupasa kujipinda itetea. Hayo ndo maswala ya dini(imani) yalivyo, kwani hakuna dini(dhehebu) lililokamilika kwa ambae si muumini wake.
Jinsi unavyouponda uislam kwenye jukwaa lile sikutegemea nawe kwako kuna mapungufu.

Yapi mapungufu? Kutoelewa kwa watu mambo ndio upungufu?
 
RC ilikua serikali yakwanza duniani kwaio kuungama kwa padri ilikua ndo style yao ya inteligensia ....kujua watu wao wanafanya nn na wapi...mm ni RC...dini zote ni akili za binadamu so kama yesu alivo sema Amri kuu ni upendo.na ukifwata hutokua na shida yakwenda kuungama.

Kama wewe ni Mkatoliki na huu ndio uelewa wako karudie mafundisho ya Ubatizo au Komunio ya Kwanza.
 
Padre ni kwa kiswahili...kwa kingereza ni Priest...

Haya nipe andiko
Padre > Father
Kuhani > Priest
Kwenye biblia hakuna neno Padre, na maana ya padre ni Father, kwenye biblia linamaana tofauti kabisa mfano sala ya wakatoliki ya Our Father,Who is in heaven..huwezi sema Padre wetu uliyembinguni....
 
Pointless

Imekupasua mfumo wa fahamu,nini? Kama ulikuwa hujui huo ndiyo "usangoma" alioufanya William Miller na wenzie(akiwemo Ellen White).Walianzisha dhehebu la kupiga ramli ya lini Yesu atarudi mara ya pili. Yesu alikwisha kusema kuwa kwa ubinadamu wake haijui tarehe lakini William na kundi lake kwa nia ya kutaka kupiga pesa za watu, wakajigeuza waganga wa kiimani kutabiri tarehe ya kurudi kwa Yesu Kristu! Upo hapo?
 
Padre > Father
Kuhani > Priest
Kwenye biblia hakuna neno Padre, na maana ya padre ni Father, kwenye biblia linamaana tofauti kabisa mfano sala ya wakatoliki ya Our Father,Who is in heaven..huwezi sema Padre wetu uliyembinguni....

Wapi kwenye Biblia kuna neno "Mwinjilisti" au "Mchungaji" katika muktadha ambao ninyi wasabato mnatumia?
 
Ninakiri kwamba nimekutana na uzi wa mwana-JF, “King Mufasa” leo ukihoji uaminifu walio nao mapadri wa Kanisa Katoliki,mintarafu utunzaji wa siri za mambo yanayojiri wakati sakramenti ya Upatanisho.

Kimsingi ukisoma katikati ya mistari ya mtoa uzi, utagundua kwamba mtoa mada ni Mkatoliki bandia, ndio kusema ni mprotestanti lakini kwa kuwa bila kujua yeye ameamua kutoa nafasi ya wakatoliki kuonyesha kwamba huwa hawafanyi mambo kwa kurupuka,nimeamua kujibu hoja yake “kwa nini maungamo yanafanyika kwa Padri” kwa uzi kamili.

Awali ya yote naomba kutoa tafsiri ya maneno makuu ambayo nimeyatumia katika Kichwa cha mada hii: Mosi,Mpinga Kristo ni mtu mmoja mmoja au kikundi cha watu ambao wanapingana na sehemu au mafundisho yote ya Yesu Kristu na ya Mitume ambao ndio Yesu aliwakabudhi mamlaka ya kuliendesha Kanisa.Pili, Na Mtu anayesoma mambo kwa kuruka ruka ni yule ambaye anavamia machapisho na kuanza kuyasoma bila kufuata misingi na kanuni za usomaji na uchakataji maudhui husika.

Ni hivi, suala la kuungama watu dhambi kwa Padri lina teolojia yake kutoka katika kisa cha kutano la Zakayo na Yesu kule Yeriko.Katika kutano hilo,kuna mambo mengi sana ambayo Kanisa Katoliki tunachota na mojawapo ni hilo la kuungama dhambi kwa Mungu, tena kwa sauti, kupitia mwakilishi wa Yesu,ambaye ni Padri.Tunasoma hivi:
Jesuit wamefanikiwa sana kwenye taratibu zao walizo weka kwamba dhambi zinasamehewa ikiwa utazitaja na kuziungama kwao hii ni aina ya upelelezi .
 
Wapi kwenye Biblia kuna neno "Mwinjilisti" au "Mchungaji" katika muktadha ambao ninyi wasabato mnatumia?
Umenipotezea mda kusoma post yako kumbe hata biblia huijui..unatetea udini badala ya Kuikubali kweli ili uwe huru..haya nambie maneno haya yanamaana gani na yanapatikanikana kitabu gani:
"Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;... "
 
Nitaipinga hoja yako mkuu kupitia kipengele chako cha mada chenye maneno "Historia ya maungamo ya dhambi katika agano la kale"

Nianze kwa kukupa history kidogo. Mara baada ya anguko la Adamu na Hawa pale Eden Mungu alikuwa ameshaanda mpango wa wokovu wa Mwanadamu ndiyo maana utaona kuna mnyama alichinjwa pale ili wapate nguo za kuficha uchi wao lkn halikuwa lengo hasa Ila alichinjwa ili awe mbadala wao kwa dhambi walizotenda ndiyo maana hawakufa kama sheria isemavyo ya mshahara wa dhambi ni mauti.

Kutokea hapo utaona ibada za kafara kupitia wanyama zikianza kwa kila aliyekuwa akitenda dhambi na hata habari ya ukuhani pia baadaye hema ya kukutania ilipoanzishwa katika kitabu cha kutoka 25 agizo la ujenzi wa hema hiyo lilipotolewa.

Katika ujenzi ule Mungu anamwambia musa kuwa hema ile itakuwa mfano wa ile ya mbinguni kwa hiyo note hata mbinguni kuna huduma ya upatanisho kupitia kuhani

Turudi kwa mada hema ya kukutania Ilikuwa na sehemu kuu tatu uwa wa nje, patakatifu na patakatifu pa patakatifu ambapo ktk uwa wa nje ndiyo sadaka za kuteketezwa zilipotolewa ambapo mdhambi alitwaa kondoo kama mbadala wake na kwenda naye kwa kuhani ambaye aliact kama mpatanishi baina ya mwanadamu mdhambi na Mungu ambapo aliungama dhambi zake kwa kuweka mikono yake juu ya kichwa cha kondoo kama namna ya kuhamisha dhambi kutoka kwake kwenda kwa kondoo kisha alimchinja na kuhani kukinga damu na kuingia nayo kwenye chumba cha pili cha patakatifu kwa ajili ya kufanya upatanisho wakati kondoo akiteketezwa katika ua wa nje huu ndiyo ulikuwa utaratibu wa wokovu ulioandaliwa na Mungu kabla ya Kristo kuja duniani

Baada ya Kristo na kufa kama mwanakondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu yohana 1:29 na kufa pale msalabani habari za kwenda kuungama kwa kuhani zilikoma au huduma za kikuhani na utoaji kafara ulikwisha maana huduma ile ilikuwa kivuli kumuwakilisha Kristo na sasa Kristo ameshakuja hakuna haja tena kwenda kwa mwanadamu kuungama wakati Kristo yupo

Kwa hiyo hoja yako ya kuungama kwa padri ni kutaka kuturudisha kwa huduma ya kikuhani ya mwanadamu ambayo ni hatari sana maana unapinga kwamba Kristo bado hajafa kwa ajili ya dhambi na wewe unageuka kuwa mpinga Kristo

Leo hatuna haja ya kuungama kwa mwanadamu tena maana tunaye Kristo mwombezi wetu kuhani asiyepatikana na mauti anayehudumu ktk hekalu lisilofanywa kwa mikono ya mwanadamu huyo pekee astahili kutuombea msamaha kwa Mungu Baba na si mwingine yoyote
Kwanza naanza kwa kupinga hoja yako kuwa "hakuna mnyama aliyechinjwa ili Adam na Hawa wapate vazi"
Hakuna mahali Biblia inasema hivyo
Usipende kuleka "assumption" kwenye maandiko.
Mungu ni muweza wa yote ili kupata ngozi sio lazima achinje mnyama

Tatu,unaposema hoja ya kuungama kwa padre ilikomeshwa na Yesu alipokufa msalabani.
Je,kama ilikomeshwa mbona aliwaagiza "MKIWASAMEHE WAMESAMEHEWA,MSIPOWASAMEHE HAWAJASAMEHEWA"

hilo agizo tuta li apply wapi kama tusipoungama kwa makuhani(mapadre)?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu umewahi kusoma kisa cha watu wawili walioenda hekaluni,mmoja aliungama dhambi zake kwa kunyenyekea mbele ya Mungu na mwingine alijivuna kwa wema wake,na Yesu akasema yule aliyenyenyekea alipata msamaha wa dhambi zake.Mbona alisamehewa bila kwenda kwa padri?
Wakati mwingine biblia inanipa changamoto!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza naanza kwa kupinga hoja yako kuwa "hakuna mnyama aliyechinjwa ili Adam na Hawa wapate vazi"
Hakuna mahali Biblia inasema hivyo
Usipende kuleka "assumption" kwenye maandiko.
Mungu ni muweza wa yote ili kupata ngozi sio lazima achinje mnyama

Tatu,unaposema hoja ya kuungama kwa padre ilikomeshwa na Yesu alipokufa msalabani.
Je,kama ilikomeshwa mbona aliwaagiza "MKIWASAMEHE WAMESAMEHEWA,MSIPOWASAMEHE HAWAJASAMEHEWA"

hilo agizo tuta li apply wapi kama tusipoungama kwa makuhani(mapadre)?

Sent using Jamii Forums mobile app

1. Mkuu uelewa huo wa wasabato kwamba Yesu hakuagiza watu kwenda kuungama dhambi ni matokeo ya kusoma mambo kwa kurukaruka.

2.Kingine wasichokijua ni kwamba wanafikiria mapadri wao hawaungami dhambi zao wanazosema mapadri wanazo kama za kulawiti, uzinzi na wizi.Dhambi hizo mapadri sio wa kwanza kuzitenda na wala hizo dhambi sio kwamba ndio dhambi kubwa kuliko zote.Hata mitume nao walikuwa wanatenda dhambi na bado dhambi hizo hazikubatilisha utume wao.
 
Jesuit wamefanikiwa sana kwenye taratibu zao walizo weka kwamba dhambi zinasamehewa ikiwa utazitaja na kuziungama kwao hii ni aina ya upelelezi .

1. Kipi kigumu zaidi, mtu kuja na kueleza dhambi zake kwa Padri kama Yesu alivyoagiza na kisha Padri mhusika kumwambia Mungu amemsamehe dhambi zake au Ellen White kujigeuza na kuwa Mungu wa kufahamu dhambi za watu na kutaka kuzitaja?

2. Yasome maandiko matakatifu sanjari na Historia.Shirika la Jesuits lilianzishwa kati ya mwaka 1545 na 1563 wakati suala la Kitubio linaonekana katika Kanisa la mwanzo kabisa kabla hata haijajulikana ni lini hao Jesuits walingalianzisha hilo shirika lao.(Rejea Society of Jesus - Wikipedia)
 
Umenipotezea mda kusoma post yako kumbe hata biblia huijui..unatetea udini badala ya Kuikubali kweli ili uwe huru..haya nambie maneno haya yanamaana gani na yanapatikanikana kitabu gani:
"Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;... "

Ndio maana nimesema ninyi mnasoma kwa kurukaruka. Nimetumia Istilahi "Mktadha" umeelewa nilikutega nini?
 
Imekupasua mfumo wa fahamu,nini? Kama ulikuwa hujui huo ndiyo "usangoma" alioufanya William Miller na wenzie(akiwemo Ellen White).Walianzisha dhehebu la kupiga ramli ya lini Yesu atarudi mara ya pili. Yesu alikwisha kusema kuwa kwa ubinadamu wake haijui tarehe lakini William na kundi lake kwa nia ya kutaka kupiga pesa za watu, wakajigeuza waganga wa kiimani kutabiri tarehe ya kurudi kwa Yesu Kristu! Upo hapo?
Sasa mbona unawasambulia wasabato tu? Kwani hamna walutheran, walokole, waanglicana, wamoravian, nakadhalika? Cha muhimu muombe Roho Mtakatifu akupe mwongozo wa kusoma biblia vizuri na akupe ufahamu wa kuelewa. Mungu akubariki sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Kipi kigumu zaidi, mtu kuja na kueleza dhambi zake kwa Padri kama Yesu alivyoagiza na kisha Padri mhusika kumwambia Mungu amemsamehe dhambi zake au Ellen White kujigeuza na kuwa Mungu wa kufahamu dhambi za watu na kutaka kuzitaja?

2. Yasome maandiko matakatifu sanjari na Historia.Shirika la Jesuits lilianzishwa kati ya mwaka 1545 na 1563 wakati suala la Kitubio linaonekana katika Kanisa la mwanzo kabisa kabla hata haijajulikana ni lini hao Jesuits walingalianzisha hilo shirika lao.(Rejea Society of Jesus - Wikipedia)
Padre siyo yesu, Na padre hana mamlaka ya kumsamehe mtu dhambi. Kanisa limetekwa.
 
1. Kipi kigumu zaidi, mtu kuja na kueleza dhambi zake kwa Padri kama Yesu alivyoagiza na kisha Padri mhusika kumwambia Mungu amemsamehe dhambi zake au Ellen White kujigeuza na kuwa Mungu wa kufahamu dhambi za watu na kutaka kuzitaja?

2. Yasome maandiko matakatifu sanjari na Historia.Shirika la Jesuits lilianzishwa kati ya mwaka 1545 na 1563 wakati suala la Kitubio linaonekana katika Kanisa la mwanzo kabisa kabla hata haijajulikana ni lini hao Jesuits walingalianzisha hilo shirika lao.(Rejea Society of Jesus - Wikipedia)
Kanisa la roma halijawahi kuwa la kweli hata siku moja, lenyewe ndilo lililo waua wakina petro.
 
Back
Top Bottom