Wanaopinga kuungama dhambi kwa Padri, ndio wapinga Kristo wanaohubiriwa na wasabato na ndio wale wanaosoma maandiko kwa kurukaruka.

Mkuu umewahi kusoma kisa cha watu wawili walioenda hekaluni,mmoja aliungama dhambi zake kwa kunyenyekea mbele ya Mungu na mwingine alijivuna kwa wema wake,na Yesu akasema yule aliyenyenyekea alipata msamaha wa dhambi zake.Mbona alisamehewa bila kwenda kwa padri?
 

Kwa hiyo, tueleze Yesu alipotoa agizo la kuwaondolea watu dhambi alimaanisha nini?
 
Hivi wazazi wa wale watoto kule Ireland nao wanaenda kuungama kwa mapadre? Kama wanafanya hivyo imani yao ni kubwa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mtu akinambia wenye biblia mi binafsi sijaona neno padre, kupitia hapo tu padre simtambui. Au padre ndo mchungaji??

Nikakosa jibu.


OK Nije kwenye mada ya kuungama kwa padre,swali langu ni hili, nikiungama kwa padre Mwenye dhambi nasamehewa??

PILI, Niliwahi kuungama kwa padre,huku padre akiwa anasinzia,,niligundua baada ya kumaliza ye akiwa kasinzia badae akashtuka akanipa sala za kusali,,je pale nilisamehewa?? Mana msameheji alilala

TATU, padre akiwa kanitongoza naweza kwenda kuungama kwake??
 
Akikujibu unitag au tukio la mwiz Mwizi Msalabani alikuwepo Padre nan?
Mbona mnaacha mafundisho ya Mungu ili mtimize matakwa yenu?.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kukosa kwa Petro hakukuwahi kumuondolea mamlaka na madaraka(ukulu) ambao alishapewa naYesu.Kwa hiyo,Padri kushindwa kuzingatia siri za maungamo hakumuondolei mamlaka hayo ya kukuondolea dhambi.
 
😀😀 umenichekeshaa sana point yako ya pili. ulimsubiri mda gani mpaka alipomka.
 
Kukosa kwa Petro hakukuwahi kumuondolea mamlaka na madaraka(ukulu) ambao alishapewa naYesu.Kwa hiyo,Padri kushindwa kuzingatia siri za maungamo hakumuondolei mamlaka hayo ya kukuondolea dhambi.
Basi kwa padri kama huyo utaendelea vipi kwenda kwake!? Wengine naweza kufikiria ila siwezi rudia kosa.
 

Nadhani ndio nasema watu tuna matatizo ya kuchakata maudhui. Yesu kwa mfano huo alitaka kufundisha jinsi ya watu tunavyoweza kujiona wakamilifu na wengine wanaotambua kwamba ni wakosefu na hivi wanastahili msamaha.Ingalikuwa ni hivyo kwamba hakuna haja ya kuungama dhambi basi Yesu asingaliweza kuacha huo muundombinu wa kuwaondolea watu dhambi. Mungu hawezi kujipinga hata kidogo.
 
tangia zamani nilikuwa nawahoji wazaz wangu ambao ni wakatoliki ujasiri huo unatoka wapi kuungama kwa padre?jibu ni kwamba haifai hata kidogo kwako mwenyewe usalama wako ni mdogo napia hata kwa mungu pia utakuwa umenyanganya mamlaka ya yesu
 
Umeandika meeeengi hoja no padri no binadamu,naye ana mapungufu ,vipi uunhame kwake usiungame Kwa mungu?

Sent using Jamii Forums mobile app

1. Kwa hiyo umeambiwa Binadamu hawezi kuondoa dhambi? Kajisomee
Zaidi ya Yote, Marko 2:5-10. Baadhi ya watu walipotilia shaka suala la Yesu katika ubinadamu kuwaondolea watu wengine dhambi, Yesu aliwathibitishia kuwa mwana wa mtu anao uwezo huo wa kuondoa dhambi za walimwengu:

“5Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza,“Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.” 6 Baadhi ya waalimu wa sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao, 7 “Anathubutuje kusema hivyo? Anamkufuru Mungu! Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake.” 8 Yesu alitambua mara mawazo yao, akawaambia, “Mbona mnawaza hivyo mioyoni mwenu? 9 Ni lipi lililo rahisi zaidi: Kumwambia mtu huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kumwambia, ‘Inuka! Chukua mkeka wako utembee?’ 10 Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anayo mamlaka ya kuwasamehe watu dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, 11 “Nakuambia simama; chukua mkeka wako uende nyumbani!”

2. Vile vile, kupitia Luka 5:24, tunaelezwa pia kwamba katika suala la uwezo wa Yesu kuwaondolea watu dhambi alifanya hivyo katika ubinadamu wake na sio kwa ule Umungu wake.

3. Mwinjili Matayo tena katika sura ile ya 18:15-20, anatudokeza jinsi Yesu kabla ya kuwapatia Mitume rasmi uwezo wa kuondolea watu dhambi, alipata kuwadokeza jambo hilo.Uwezo wa kufunga na kufungua ndio kule kuwaondolea watu adhabu za muda mfupi, zitokanazo na dhambi:

“15 Na ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo.16 La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike.17 Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.18 Amin, nawaambieni, yoyote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.19 Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. 20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”
 
tangia zamani nilikuwa nawahoji wazaz wangu ambao ni wakatoliki ujasiri huo unatoka wapi kuungama kwa padre?jibu ni kwamba haifai hata kidogo kwako mwenyewe usalama wako ni mdogo napia hata kwa mungu pia utakuwa umenyanganya mamlaka ya yesu

Ubatizo huondoa dhambi na maungamo huondoa dhambi.Kwani hujawahi kujibatiza mwenyewe kwa maana si unajua maji ndiyo yanaondoa dhambi na unafahamu fika yanapatika kwenye mito na maziwa au baharini?
 
Basi kwa padri kama huyo utaendelea vipi kwenda kwake!? Wengine naweza kufikiria ila siwezi rudia kosa.

1.Kwani umeambiwa lazima uende kwa padri yule yule tu? Ndivyo kanisa Katoliki linavyofundisha?

2. Kwa nini unauona tu upungufu wa Mapadri katika kuungama dhambi ila kukubatiza bado unaendelea kwenda kwao na bado hata watoto wako bado unampelekea padri yule yule?

3. Mtu yeyote "anayemtunishia" Padri kuungama dhambi hana tofauti na Adamu na Eva kutokuwa tayari kukiri makosa yao na badala yake waliishia kutafuta visingizio.Ni dalili ya kukosa unyenyekevu.Ni dalili ya kujiona sisi tunafahamu zaidi kuliko wengine au kwamba sisin tuna hadhi sana kuliko wengine.
 
Catholism is ant Christ by nature

Ndivyo "roho wa unabii" wa William Miller na Ellen (aliyewafanya wahangaike na tarehe ya kurudi Yesu badala ya kuwahimiza watu namna ya kumsubiria Yesu) alivyokujalia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…