Wanaopinga mahakama Kadhi "Intellectual Arguments" only

Wanaopinga mahakama Kadhi "Intellectual Arguments" only

Status
Not open for further replies.
Hapo ndio kwenye ujinga wako. Hivi pale kwenye mahakama ya kadhi ni sawa na hospitali na shule ambayo kila mtu hutibiwa na kusoma bila kuangalia dini wala kabila lake?

Tumia akilli kufikiri. Kinachowasumbua ni yale mazoea mliorithi kwa waarabu ya kutokupenda kuwajibika. Hospitali ni kwa ajili ya jamii nzima tofauti na hiyo mahakama ya ndoa za kiislamu. Hivi ni kweli huoni tofauti au ndio akili zile zile za kwenye mihadhara?
una uhakika hakuna ubaguzi ?
 
Ndugu, nimesoma hoja zenu zote wengi wenu mnajenga hoja kwenye issues zifuatazo

1. Swala la Gharama linajirudia sana: Tumetoa maelezo mengi sana hapa tumesema kwamba serikali kuhudumia wananchi wengi si kosa ikiwa huduma hiyo inasaidia jamii hiyo kuwa na amani na kufanya ibada zake vema. Tunawapa mifano ya miradi ya kanisa inavyofadhiliwa na kanisa (kama mfano tu). pili hukumu nyingi zinazotolewa na mahakama ya kawaida inakuwa mara nyingi inaingilia imani zetu mfano kugawanya mali sawa kwa sawa kati ya wana ndoa, kitu ambacho kwa uislamu ni makosa kwani kuna watu wengi wanatakiwa kupata sehemu ya mirathi ya mali ya mtu wakiwemo wazazi..kwakuwa hakimu wa sasa anakosea kuwepo kwa kadhi atasaidia kutoa hukumu sahihi ambayo waislamu watafurahia na kuwa na amani kuliko sasa..lazima serikali i-finance hukumu sahihi..kwa wananchi wake kwa mujibu wa imani zao..kuhukumu vinginevyo wakati ndoa inatambulika ndiyo kuingilia imani zetu..tunataka tukifunga ndoa kiislamu zihukumiwe kiislam pia??

2. Wengine wanaongelea hukumu kuwa kandamizi..hao nafikiri hawaamini hukumu za Allah (Muumba wa Mbingu na Ardhi), hukumu za Allah ni just wala si kandimizi. kwa mfano katika sharia mwanamke anapata nusu ya mwanaume lakini yeye mwanamke anatakiwa kutunzwa na baba yake, au kaka yake au mume wake hakuna wakati mwanamke anatakiwa kukaa peke yake bila kutunzwa na mwanamume japo bado anapata nusu ya mali..above all kama wewe unaona ni kandamizi wanawake wengi wa kiislam wako radhi na hukumu hizo kwa hiyo hiyo hoja ni dhaifu..na zingine zote zinazosema ni kandimizi tunaweza kusema ni dhaifu..sana na kwamba haiwahusu tuachie tuliomuamini Allah.

3. Wengine wanajenga hoja kwanini tusiombe fully sharia??..ndugu ikiwa tunaomba mahakama kwa ajili ya mirathi inakuwa mbinde hivi itakuwaje fully sharia?. pili waislam wanaamini katika mwendo wa hatua kwa hatua. ikiwa waislamu wataona kuna faida na heri kubwa imepatikana baada ya kupata mahakama ya kadhi (mirathi na ndoa) wanaweza baada kukubali kuhukumiwa hata katika biashara, makosa ya jinai n.k. kwangu mimi hii itakuwa ni wakati wa kadhi kujijengea uwezo (capacity) huwezi kuanza kwa ujumla wakati capacity ni ndogo na waislamu wengi hawako tayari au mazingira hayaruhusu kufanya hivyo. hoja hii jibu lake ni kwamba kila kitu huanza na hatua moja na ikiwa waislamu wataona ni muhimu wanaweza kuendelea kutumia MyK kwa ajili ya hukumu zingine siku zijazo. Na pia uislamu una amini katika DHARURA hali na mazingira tuliyopo ni ya dhararu kwahiyo ikiwa itapatikana ya mirathi Alhamudulalihi.

3. Wengine wana hoji kwanini tupate authority ya kikatiba? tena katiba ya kikafiri/makafiri?: tumeeleza mara nyingi jambo hili kinachotakiwa hapa si lingine ila mamlaka ya kutoa hukumu. ukilifanya jambo hili nje ya katiba itakuwa sawa na hukumu iliyotolewa na NGO na maana nzima ya ibada itakuwa haipo. Kwakuwa authority inatokana na katiba hivyo swala la kadhi linatakiwa liwe kwenye katiba na hukumu zake zitambulike na katiba. Maana yake ni kwamba ikiwa waislamu wame opt kutumia mahakama hii lazima hatimaye waridhike na wafuate hukumu na si vinginevyo. wakitaka wasifunge kabisa ndoa kiislamu au wakane uislamu ili wahukumiwe kwa sheria za nchi..(choice ni yao)

4. Wengine wameenda kwenye extreme case eti tuondoke nchini kamwe hakutakuwepo MyK: hao nawaambia hivi ikiwa waislamu wachache wa kenya wameweza kuwa na Mahakama ya kadhi itakuwa sisi waislamu wa Tanzania tulio wengi? hili swala kusema ukweli iko siku tutapata mahakama ya kadhi. ama kuhusu kuhama hatutakimbia nchi kwasababu ya wakristo wenye chuki nasi ila tutabanana hapa hapa..kwakuwa hoja hii ni dhaifu wala haijengi utaifa wetu..

Nasisitiza kama hoja zenu ni hizo ukweli ni kwamba hakuna sababu ya kuzuiliwa mahakama ya kadhi zaidi ya "wananchi wa Tanzania wakristo kuwa na roho ya uchoyo na chuki kwa waislam wenzio wa Tanzania"

Nasikitika sana kwamba ikifikia waislamu wakanuna na kuacha kusikilizana na wakristo wa Tanzania kama sasa, sasa hivi tunashare information kuhusu mahakama ya kadhi, tunafuata kanuni zote tupo wazi kwa wakristo walioko serikalini tukitegemea nao wako wazi na wako na GOODWILL lakini kadiri siku zinavyopita naona ufa wa goodwill una pungua.. ili kuilinda umoja wa kitaifa kati ya waislamu na wakristo wa Tanzania. wakristo waache kushindana na kuonyesha wana nguvu ya kukataa maombi ya waislamu kwa serikali yao. Mambo haya yakiendelea na umoja wa kitaifa utakuwa kwenye matatizo na taifa linaweza kuingia kwenye mgogoro mkubwa sana ambao watu wenye busara wanashindwa ku-solve very simple problem kwa arguments ambazo haizna mshiko. ni afadhali watu wakaacha ushabiki na kuongea kisomi kuliko chuki na upofu wa hoja nilizoweka hapo juu..maana

Swali la msingi?? lina baki "Hivi nyie wakristo mnakosa nini kwa waislamu kuwa na mahakama ya kadhi kama sio mashindano na kiburi???
 
Nasikitika sana kwamba ikifikia waislamu wakanuna na kuacha kusikilizana na wakristo wa Tanzania kama sasa, sasa hivi tunashare information kuhusu mahakama ya kadhi, tunafuata kanuni zote tupo wazi kwa wakristo walioko serikalini tukitegemea nao wako wazi na wako na GOODWILL lakini kadiri siku zinavyopita naona ufa wa goodwill una pungua.. ili kuilinda umoja wa kitaifa kati ya waislamu na wakristo wa Tanzania. wakristo waache kushindana na kuonyesha wana nguvu ya kukataa maombi ya waislamu kwa serikali yao. Mambo haya yakiendelea na umoja wa kitaifa utakuwa kwenye matatizo na taifa linaweza kuingia kwenye mgogoro mkubwa sana ambao watu wenye busara wanashindwa ku-solve very simple problem kwa arguments ambazo haizna mshiko. ni afadhali watu wakaacha ushabiki na kuongea kisomi kuliko chuki na upofu wa hoja nilizoweka hapo juu..maana

Swali la msingi?? lina baki "Hivi nyie wakristo mnakosa nini kwa waislamu kuwa na mahakama ya kadhi kama sio mashindano na kiburi???

Topical.. unachokosea ni kuwa unataka kujenga hoja ya mahakama ya kadhi na kutaka watu wakubali tu bila kuuliza, kuhoji au hata kukataa. Kwamba, kwa vile Waislamu wanasema hivyo basi watu wengine wote wakae kimya. Bahati mbaya hakuna namna ambayo mahakama ya kadhi inaweza kuanzishwa Tanzania bila kuwahusisha Wakristu. Hakuna namna au jinsi ya kufanya hivyo. Ili iweze kuanzishwa ni lazima Watanzania wahusishwe (wakristu na waislamu na hata wapagani). Namna pekee ya kutowahusisha Wakristu ni kwa Waislamu peke yao kuanzisha mahakama yao na wao wakakubaliana jinsi ya kuiendesha na kuisimamia.

Mnapotaka Serikali ya Watanzania wote kuhusishwa mnawalazimisha Wakristu na wasio Wakristu kutolea maoni - hawawezi kukaa kimya. HOja ya umoja wa kitaifa na migongano ni hoja yenye nguvu na bahati nzuri au mbaya haiwezi kutumiwa kama tishio kwa Wakristu kwamba wasipokubali basi kutakuwa na vurugu nchini. Ni hoja isiyo na msingi na inatolewa ikifikiria kwamba basi watu watishike na kukubali tu. Unafikiria vurugu za watu wenye msimamo mkali huko Pakistani zinawadhuru wale maadui zao? Unafikiri wale wenye msimamo mkali Afghanistani ambao wanawachukia wengine wakifanya vurugu wao wenyewe wananusurika?

Ukitoa mgongano Tanzania hakuna Mkristu au MUislamu ambaye atasema anaishi kwa amani. Matokeo yake itakuwa ni kama Nigeria ambapo Wakristu waliamua kufuatia vurugu kuanza kuondoka maeneo yenye Waislamu wengi kule Kaskazini na kuja maeneo ya Kusini na Waislamu nao kuanza kuondoka maeneo yenye Wakristu wengine na kurudi Kaskazini. Lakini katika yote hawajapata amani. Ni kwa sababu upande mmoja unataka usikilizwe kwa gharama yoyote ile.

Wanaotaka mahakama ya kadhi wana haki kabisa ya kujenga hoja hiyo na kwa kweli kwa sisi wengine tunaunga mkono kabisa. Tatizo ni kuwa Topical inaonekana unachosema ni kuwa "hatujali Watanzania wengine wanasema nini" na hivyo ni 'our way or the highway". Well, it ain't gonna happen vinginevyo ingekuwa imeshatokea. Jifunze kusikiliza hoja tunazotoa, acknowledge nguvu zake, na jaribu kuwa upande wetu kama sisi wengine tunavyojaribu kuwa upande huo. Wakristu wa TAnzania wangekuwa hawataki mahakama za kadhi wasingesema WAislamu waanzishe wenyewe! Hawaogopi mahakama za kadhi kwani Waislamu ni ndugu zetu na jamaa zetu na ukiangalia utakuta kuwa ni sisi wenyewe! Sijui kama kuna familia hata moja ya Kitanzania ambayo haina pande zote mbili za Wakristu na Waislamu. Kama zipo ni chache sana. Sisi hatuko kama Nigeria au nchi nyingine ambazo mstari wa udini umepitishwa kwa ukali zaidi.
 
Topical.. unachokosea ni kuwa unataka kujenga hoja ya mahakama ya kadhi na kutaka watu wakubali tu bila kuuliza, kuhoji au hata kukataa. Kwamba, kwa vile Waislamu wanasema hivyo basi watu wengine wote wakae kimya. Bahati mbaya hakuna namna ambayo mahakama ya kadhi inaweza kuanzishwa Tanzania bila kuwahusisha Wakristu. Hakuna namna au jinsi ya kufanya hivyo. Ili iweze kuanzishwa ni lazima Watanzania wahusishwe (wakristu na waislamu na hata wapagani). Namna pekee ya kutowahusisha Wakristu ni kwa Waislamu peke yao kuanzisha mahakama yao na wao wakakubaliana jinsi ya kuiendesha na kuisimamia.

Mnapotaka Serikali ya Watanzania wote kuhusishwa mnawalazimisha Wakristu na wasio Wakristu kutolea maoni - hawawezi kukaa kimya. HOja ya umoja wa kitaifa na migongano ni hoja yenye nguvu na bahati nzuri au mbaya haiwezi kutumiwa kama tishio kwa Wakristu kwamba wasipokubali basi kutakuwa na vurugu nchini. Ni hoja isiyo na msingi na inatolewa ikifikiria kwamba basi watu watishike na kukubali tu. Unafikiria vurugu za watu wenye msimamo mkali huko Pakistani zinawadhuru wale maadui zao? Unafikiri wale wenye msimamo mkali Afghanistani ambao wanawachukia wengine wakifanya vurugu wao wenyewe wananusurika?

Ukitoa mgongano Tanzania hakuna Mkristu au MUislamu ambaye atasema anaishi kwa amani. Matokeo yake itakuwa ni kama Nigeria ambapo Wakristu waliamua kufuatia vurugu kuanza kuondoka maeneo yenye Waislamu wengi kule Kaskazini na kuja maeneo ya Kusini na Waislamu nao kuanza kuondoka maeneo yenye Wakristu wengine na kurudi Kaskazini. Lakini katika yote hawajapata amani. Ni kwa sababu upande mmoja unataka usikilizwe kwa gharama yoyote ile.

Wanaotaka mahakama ya kadhi wana haki kabisa ya kujenga hoja hiyo na kwa kweli kwa sisi wengine tunaunga mkono kabisa. Tatizo ni kuwa Topical inaonekana unachosema ni kuwa "hatujali Watanzania wengine wanasema nini" na hivyo ni 'our way or the highway". Well, it ain't gonna happen vinginevyo ingekuwa imeshatokea. Jifunze kusikiliza hoja tunazotoa, acknowledge nguvu zake, na jaribu kuwa upande wetu kama sisi wengine tunavyojaribu kuwa upande huo. Wakristu wa TAnzania wangekuwa hawataki mahakama za kadhi wasingesema WAislamu waanzishe wenyewe! Hawaogopi mahakama za kadhi kwani Waislamu ni ndugu zetu na jamaa zetu na ukiangalia utakuta kuwa ni sisi wenyewe! Sijui kama kuna familia hata moja ya Kitanzania ambayo haina pande zote mbili za Wakristu na Waislamu. Kama zipo ni chache sana. Sisi hatuko kama Nigeria au nchi nyingine ambazo mstari wa udini umepitishwa kwa ukali zaidi.

Nafikiri wakristo wa Tanzania ndicho wanachotegemea waislamu wafanye vurugu ili waseme kuwa waislamu wameleta fujo nchini kumbe wameomba miaka nenda rudi lakini wananchi wenzao wakristo wenye madaraka wamekataa kwasababu ambazo hazina mshiko bali kuinyesha kiburi na mashindano...unafikiri wanigieria walipenda, unafikiri mataifa mengine walipenda na Tanzania ni tofauti sana??? BIG time NO ufa unaojengwa kwa mashindano ambayo yapo kwenye hoja ya gharama ni dhaifu sana...

Nimekuuliza wewe kama mkristo unakosa nini waislamu kuwa na mahakama ya kadhi???Tanzania
 
Nafikiri wakristo wa Tanzania ndicho wanachotegemea waislamu wafanye vurugu ili waseme kuwa waislamu wameleta fujo nchini kumbe wameomba miaka nenda rudi lakini wananchi wenzao wakristo wenye madaraka wamekataa kwasababu ambazo hazina mshiko bali kuinyesha kiburi na mashindano...unafikiri wanigieria walipenda, unafikiri mataifa mengine walipenda na Tanzania ni tofauti sana??? BIG time NO ufa unaojengwa kwa mashindano ambayo yapo kwenye hoja ya gharama ni dhaifu sana...

Nimekuuliza wewe kama mkristo unakosa nini waislamu kuwa na mahakama ya kadhi???Tanzania

Inaonekana hujasoma majibu yangu ambayo nimeanza kuyaandika miaka minne iliyopita - hakuna kitu ambacho Mkristu anahofia kuhusu mahakama ya kadhi kuwepo. Ndio maana sisi wengine tunawapigia debe muianzishe na utaona hakuna Wakristu wanaokataa uwepo wa mahakama ya kadhi.

Ila pia inaonekana hujafikiria vya kutosha jinsi gani mahakama ya kadhi inawahusu Wakristu vile vile. Mahakama ya kadhi haitaathiri Waislamu peke yao.

a. Kama wanataka serikali ilipie gharama za kuendesha mahakama ya kadhi kwa kodi za wananchi basi walipa kodi (wakristu wakiwemo) wanayo haki ya kutoa kauli yao. Kama vile tunavyosikiliza hoja za Waislamu wanaopinga serikali kutoa ruzuku kwenye hospitali za rufaa zinazoendeshwa na makanisa. Waislamu hao wanayo haki kabisa ya kuhoji matumizi ya fedha hizo na kama wanaona kanisa linapendelewa wanayo haki kabisa ya kupinga fedha hizo kwenda kwenye mahospitali hayo na kutaka makanisa yaendeshe mahospitali yake kwa gharama zake. Sasa kama WAislamu wanaweza kujenga hoja hiyo kuhusu gharama kwenda kwa makanisa (japo utaona mahospitali yanahudumia na kuajiri watu wa dini zote). Lakini hoja ya Wakristu inaweza kuwa na nguvu zaidi kwa sababu mahakama ya kadhi si kwa ajili ya wananchi wote na wale haiwezi kuwa na kadhi Mkristu au Mhindu (hata kama atakuwa amesomea sharia!). Kwa hiyo wanayo haki ya kuzungumzia jinsi fedha zao zinataka kutumiwa.

b. Mahakama za kadhi zitagusa familia za Wakristu vile vile. Fikiria mahali ambapo mwanamme ni Muislamu na Mke ni Mkristu. Je, Mkristu akitaka kutafuta haki kwa njia ya mahakama za kawaida na Muislamu (mume) anataka kwenda mahakam za kadhi ni nani anakuwa muamuzi? Je, mirathi ambapo baba na mama walikuwa Waislamu lakini mtoto wao mmoja ni Mkristu na hatambui nguvu ya mahakama za kadhi ataomba haki yake wapi? Kwa hiyo kwamba Mahakama ya kadhi inawahusu Waislamu peke yake utaona haina mshiko vile vile kwa sababu kwa jinsi jamii yetu ilivyo Wakristu watajikuta wanaingizwa humo isipokuwa kama kuna kipengele ambapo mtu hata kama Muislamu ataamua yeye mwenyewe kesi yake iende wapi (state court system au islamic courts). Je, mahali ambapo Waislamu wawili wanaamua kwenda katika mahakama ya nchi (kama ilivyo sasa) itakuwaje?

c. Bahati mbaya Waislamu wanataka serikali iwasikilize na hata kupitisha sheria ya kutambua uwepo wa mahakama ya kadhi. Bahati mbaya zaidi hatuna bunge la Waislamu peke yao. Sheria yoyote ambayo itataka kujadiliwa na kupitishwa ni LAZIMA wabunge Wakristu wahusishwe. Vinginevyo, itabidi mtake Wabunge Wakristu wasishiriki mjadala na wala wasipinge wakae kimya na kuwaacha wabunge Waislamu wajadiliane wao wenyewe na kupitisha sheria hiyo. Hakuna NAMNA YOYOTE ambapo mahakama ya kadhi inaweza kuanzishwa Tanzania pasipo kuwashirikisha Wakristu kama serikali inatakiwa ihusike. Njia PEKEE ya mahakama ya kadhi kuanzishwa bila kushirikishwa Wakristu ni kwa Waislamu kuianzisha yenyewe. Kama tatizo ni uwezo wa fedha nina uhakika wapo watu wengi tu wanaweza kusaidia kuanzisha mahakama hiyo - Wakristu na Waislamu.
 
Assume wewe ni muislam na una wake watatu na watoto 5:4:3 yaani 12 jumla kwa wake watatu..umefariki

Kwa sheria za ndoa ya 1971; ugawaji wa urithi huo hauwezekani japo muislam huyu aliruhusiwa kuoa kiislam

Kwanini mali yake isigawanywe kiislam?? tunataka kadhi wawasaidie hao wanawake, watoto kuhusu mgawanyiko wa mali ya muumini huyu.. siyo voluntarily iwe sheria kabisa na hukumu itolewe na mahakama..ok

Ndio maana tunataka mahakama ya Kadhi..

NB: Naomba wale wenye hasira na uislam na waislamu watuache kwanza tuseme kwanini tunataka mahakama ya kadhi ili mtuelewe

Nimefuatilia kwa makini Hoja kwa ujumla, Mtoa hoja na wachangiaji.. Sijaona point zaidi ya Ubabe . By the way Hiki ndicho Shekhat ya kiislam inachokipinga kwa Nguvu Zote. Kwanini Baadhi ya Vijibaba vijifanye vyenyewe ndio vidume vya mbegu kwa kurundika Lundo la wanawake Ndani ya Ndoa kwa kisingizio cha Dini?... Ni kunyanyapaa wanawake, Hebu Tupashane au tuelezane ukweli jamvini bila chenga, Mwanaumme huchukua 2-15 minutes kwenye tendo la ndoa kabla ya kujiradhi ila mwanamke huchukua zaidi ya nusu saa, na kwa wapendanao inamgharimu mwanaume aende mbele zaidi ili amrdhia mkewe kwenye tendo la ndoa.. na Hii inamgharimu mwanaume kausumbufu flani, Nguvu pamoja na concentration. Sasa unapokuwa na mke zaidi ya mmoja utawezaje kuwafikisha wote radhia, kwa mateso gani.. kama sio kuwachafuachafua na kuwatosa. Ni nani mwenye mke zaidi ya mmoja na ukawasikia wanawake hao wakiwa happy radhiani.
Kwani shahidia inasemaje, mwanamke wa kiislam anayo haki ya kumtaka mumewa mahaba muda wowote, sasa kama unao wawili au balaa zaidi watatu na wote wanataka mahaba kwa wakati mmoja Utawawezaje?.. kwanini kuendekeza mawazo mgando kwamba wanawake wa kiislam ni vyombo vya starehe kwa wanaume na zana za kufyatulia watoto??.
Tuseme Ukweli Kuoa mke zaidi ya Mmoja ni Tamaa tu za wababa ambao wanasingizia kwamba ni Amri ya mtume. Mtume alikuwa na wake kadhaa, yes that is true, but yeye aliwaoa kwa misingi ya safari alivyosafiri kwenye kwa kuipigania dini kwa hivyo asingebeba familia zake zote, that is why akiwa mji mwingine alioa huko then alipokwenda another mji akaoa tena, sasa wewe mbaba wapi umekwenda kupigana vita gani mpaka urundike kinamama ndani.. Tamaa tu, Muone.. aiibu hata Ukimwi huogopi?
Shekhat ya Kiislam inachojua kuna agenda za siri zinazopelekea uundwaji wa mahakama za kadhi, sasa kwanini nyie wababa msizisemeeee mpaka mtumie mlango wa kudhalilisha wanawake this way?.. eti mtu anajitapa kabisa eti ana wake 3, hata aibu huoni.
unaposema kwa ajili ya mirathi, hiki ndicho shekhat ya kiislam haitaki kabisaaa kusikia, Kwenye mirathi mwanamke wa kiislam hana sauti kabisa, Hata kama Sheria za nchi zikaruhusu mahakama ya kadhi, humo ndani viwembe vitatembea kwa sana, mtueleze mnaiunda kwa mujibu wa sharia ipi, za sunni au shia, na kama ni suni, mnasemaje kuhusu mwanamke kuwa eda huku mali walizochuma na mumewe zikigawanywa??.. m kama ni shia mnasemaje kuhusu talaka komoa 2, na mume akafa, mke atakuwaje?!! Tunaiita talaka komoa kwa sababu ni ubabe tu wa mwanaume kumtaliki mkewe talaka mbili ati iko siku atamuoa tena kisha yeye huku anaendeleza libeneke na wanawake wengine anaowaoa. Mbona huu ni ujinga KAMILI?. Dini haisemi hivyo ni Ubabe tu wa vibaba vya kileo. Mmetengeneza Baaza la Maulamaa kimywakimya hata mwanamke hajuikani ndani ya uislam. Tulisemanini kuhusu Bakwata. Mbona watu mnatumia Kigezo Cha Dini mliyochakachua sheria zake kukandamiza wanawake???
Mwisho wa hoja umesema Tuache waislam tuelezee kwanini tunataka mahakama ya kadhi, kumradhi turnabal, badilisha semi yako mara moja, useme kundi Fulani la wababa wa kiislam wasiodhibiti hisia za tamaa zao zilizopindukia na kuoa rundo la wanawake kwa starehe ambao hufa mapema kwa tamaa hizo ndio wanataka waeleze kwanini wanahitaji mahakama ya kadhi, hapo ungeeleweka. Ashkhum
 
Nimefuatilia kwa makini Hoja kwa ujumla, Mtoa hoja na wachangiaji.. Sijaona point zaidi ya Ubabe . By the way Hiki ndicho Shekhat ya kiislam inachokipinga kwa Nguvu Zote. Kwanini Baadhi ya Vijibaba vijifanye vyenyewe ndio vidume vya mbegu kwa kurundika Lundo la wanawake Ndani ya Ndoa kwa kisingizio cha Dini?... Ni kunyanyapaa wanawake, Hebu Tupashane au tuelezane ukweli jamvini bila chenga, Mwanaumme huchukua 2-15 minutes kwenye tendo la ndoa kabla ya kujiradhi ila mwanamke huchukua zaidi ya nusu saa, na kwa wapendanao inamgharimu mwanaume aende mbele zaidi ili amrdhia mkewe kwenye tendo la ndoa.. na Hii inamgharimu mwanaume kausumbufu flani, Nguvu pamoja na concentration. Sasa unapokuwa namke zaidi ya mmoja utawezaje kuwafikisha wote radhia, kwa mateso gani.. kama sio kuwachafuachafua na kuwatosa. Ni nani mwenye mke zaidi ya mmoja na ukawasikia wanawake hao wakiwa happy radhiani.
Kwani shahidia inasemaje, mwanamke wa kiislam anayo haki ya kumtaka mumewa mahaba muda wowote, sasa kama unao wawili au balaa zaidi watatu na wote wanataka mahaba kwa wakati mmoja Utawawezaje?.. kwanini kuendekeza mawazo mgando kwamba wanawake wa kiislam ni vyombo vya starehe kwa wanaume na zana za kufyatulia watoto??.
Tuseme Ukweli Kuoa mke zaidi ya Mmoja ni Tamaa tu za wababa ambao wanasingizia kwamba niAmri ya mtume. Mtume alikuwa na wake kadhaa, yes that is true, but yeye aliwaoa kwa misingi yasafari alivyosafiri kwenye kwa kuipigania dini kwa hivyo asingebeba familia zake zote, that is why akiwa mji mwingine alioa huko then alipokwenda another mji akaoa tena, sasa wewe mbaba wapi umekwenda kupigana vita gani mpaka urundike kinamama ndani.. Tamaa tu, Muone.. aiibu hata Ukimwi huogopi?
Shekhat ya Kiislam inachojua kuna agenda za siri zinazopelekea uundwaji wa mahakama za kadhi, sasa kwanini nyie wababa msizisemeeee mpaka mtumie mlango wa kudhalilisha wanawake this way?.. eti mtu anajitapa kabisa eti ana wake 3, hata aibu huoni.
unaposema kwa ajili ya mirathi, hiki ndicho shekhat ya kiislam haitaki kabisaaa kusikia, Kwenye mirathi mwanamke wa kiislam hana sauti kabisa, Hata kama Sheria za nchi zikaruhusu mahakama ya kadhi, humo ndani viwembe vitatembea kwa sana, mtueleze mnaiunda kwa mujibu wa sharia ipi, za sunni au shia, na kama ni suni, mnasemaje kuhusu mwanamke kuwa eda huku mali walizochuma na mumewe zikigawanywa??.. m kama ni shia mnasemaje kuhusu talaka komoa 2, na mume akafa, mke atakuwaje?!! Tunaiita talaka komoa kwa sababu ni ubabe tu wa mwanaume kumtaliki mkewe talaka mbili ati iko siku atamuoa tena kisha yeye huku anaendeleza libeneke na wanawake wengine anaowaoa. Mbona huu ni ujinga KAMILI?. Dini haisemi hivyo ni Ubabe tu wa vibaba vya kileo. Mmetengeneza Baaza la Maulamaa kimywakimya hata mwanamke hajuikani ndani ya uislam. Tulisemanini kuhusu Bakwata. Mbona watu mnatumia Kigezo Cha Dini mliyochakachua sheria zake kukandamiza wanawake???
Mwisho wa hoja umesema Tuache waislam tuelezee kwanini tunataka mahakama ya kadhi, kumradhi turnabal, badilisha semi yako mara moja, useme kundi Fulani la wababa wa kiislam wasiodhibiti hisia za tamaa zao zilizopindukia na kuoa rundo la wanawake kwa starehe ambao hufa mapema kwa tamaa hizo ndio wanataka waeleze kwanini wanahitaji mahakama ya kadhi, hapo ungeeleweka. Ashkhum
Hii kali , ngoja niende kanisani nitaudi baadaye
 
Unapoleta hoja hapa jitahidi uwe na uelewa japo kidogo juu ya mada yako topical, otherwiz uliza ueleweshwe.
 
Kama wanataka serikali ilipie gharama za kuendesha mahakama ya kadhi kwa kodi za wananchi basi walipa kodi (wakristu wakiwemo) wanayo haki ya kutoa kauli yao. Kama vile tunavyosikiliza hoja za Waislamu wanaopinga serikali kutoa ruzuku kwenye hospitali za rufaa zinazoendeshwa na makanisa. Waislamu hao wanayo haki kabisa ya kuhoji matumizi ya fedha hizo na kama wanaona kanisa linapendelewa wanayo haki kabisa ya kupinga fedha hizo kwenda kwenye mahospitali hayo na kutaka makanisa yaendeshe mahospitali yake kwa gharama zake. Sasa kama WAislamu wanaweza kujenga hoja hiyo kuhusu gharama kwenda kwa makanisa (japo utaona mahospitali yanahudumia na kuajiri watu wa dini zote). Lakini hoja ya Wakristu inaweza kuwa na nguvu zaidi kwa sababu mahakama ya kadhi si kwa ajili ya wananchi wote na wale haiwezi kuwa na kadhi Mkristu au Mhindu (hata kama atakuwa amesomea sharia!). Kwa hiyo wanayo haki ya kuzungumzia jinsi fedha zao zinataka kutumiwa.
Nimeandika katika thread hii nikimueleza Topical kuwa ni waislam wanaotaka wawe na vyombo huru vya mambo yao. Kuingiza senti ya serikali ni kukaribisha tatizo kama lile la BAKWATA. Na kama basi suala ni kupata ruzuku kwanini waislam wasikubaliane ipitishwe BAKWATA ambako wanadai kuwa serikali ina ufadhili? Angalia contradiction!

Pili, Topica, unapodai haki kwanza unatakiwa ujue unadai nini na kwa nini. Usipojua kimoja kati hivyo unaweza kushindwa kesi hata kabla hakimu hajakaa kwenye kiti.
Unasema waislam wamedai mahakama ya kadhi kwa muda mrefu na itafika mahali wataleta vurugu.

Kabla sijakuuliza swali lenyewe, hebu nipe ufafanuzi kidogo. Je waislam wameanza kudai mahakama ya kadhi kuanzia lini.
 
Nimefuatilia kwa makini Hoja kwa ujumla, Mtoa hoja na wachangiaji.. Sijaona point zaidi ya Ubabe . By the way Hiki ndicho Shekhat ya kiislam inachokipinga kwa Nguvu Zote. Kwanini Baadhi ya Vijibaba vijifanye vyenyewe ndio vidume vya mbegu kwa kurundika Lundo la wanawake Ndani ya Ndoa kwa kisingizio cha Dini?... Ni kunyanyapaa wanawake, Hebu Tupashane au tuelezane ukweli jamvini bila chenga, Mwanaumme huchukua 2-15 minutes kwenye tendo la ndoa kabla ya kujiradhi ila mwanamke huchukua zaidi ya nusu saa, na kwa wapendanao inamgharimu mwanaume aende mbele zaidi ili amrdhia mkewe kwenye tendo la ndoa.. na Hii inamgharimu mwanaume kausumbufu flani, Nguvu pamoja na concentration. Sasa unapokuwa namke zaidi ya mmoja utawezaje kuwafikisha wote radhia, kwa mateso gani.. kama sio kuwachafuachafua na kuwatosa. Ni nani mwenye mke zaidi ya mmoja na ukawasikia wanawake hao wakiwa happy radhiani.
Kwani shahidia inasemaje, mwanamke wa kiislam anayo haki ya kumtaka mumewa mahaba muda wowote, sasa kama unao wawili au balaa zaidi watatu na wote wanataka mahaba kwa wakati mmoja Utawawezaje?.. kwanini kuendekeza mawazo mgando kwamba wanawake wa kiislam ni vyombo vya starehe kwa wanaume na zana za kufyatulia watoto??.
Tuseme Ukweli Kuoa mke zaidi ya Mmoja ni Tamaa tu za wababa ambao wanasingizia kwamba niAmri ya mtume. Mtume alikuwa na wake kadhaa, yes that is true, but yeye aliwaoa kwa misingi yasafari alivyosafiri kwenye kwa kuipigania dini kwa hivyo asingebeba familia zake zote, that is why akiwa mji mwingine alioa huko then alipokwenda another mji akaoa tena, sasa wewe mbaba wapi umekwenda kupigana vita gani mpaka urundike kinamama ndani.. Tamaa tu, Muone.. aiibu hata Ukimwi huogopi?
Shekhat ya Kiislam inachojua kuna agenda za siri zinazopelekea uundwaji wa mahakama za kadhi, sasa kwanini nyie wababa msizisemeeee mpaka mtumie mlango wa kudhalilisha wanawake this way?.. eti mtu anajitapa kabisa eti ana wake 3, hata aibu huoni.
unaposema kwa ajili ya mirathi, hiki ndicho shekhat ya kiislam haitaki kabisaaa kusikia, Kwenye mirathi mwanamke wa kiislam hana sauti kabisa, Hata kama Sheria za nchi zikaruhusu mahakama ya kadhi, humo ndani viwembe vitatembea kwa sana, mtueleze mnaiunda kwa mujibu wa sharia ipi, za sunni au shia, na kama ni suni, mnasemaje kuhusu mwanamke kuwa eda huku mali walizochuma na mumewe zikigawanywa??.. m kama ni shia mnasemaje kuhusu talaka komoa 2, na mume akafa, mke atakuwaje?!! Tunaiita talaka komoa kwa sababu ni ubabe tu wa mwanaume kumtaliki mkewe talaka mbili ati iko siku atamuoa tena kisha yeye huku anaendeleza libeneke na wanawake wengine anaowaoa. Mbona huu ni ujinga KAMILI?. Dini haisemi hivyo ni Ubabe tu wa vibaba vya kileo. Mmetengeneza Baaza la Maulamaa kimywakimya hata mwanamke hajuikani ndani ya uislam. Tulisemanini kuhusu Bakwata. Mbona watu mnatumia Kigezo Cha Dini mliyochakachua sheria zake kukandamiza wanawake???
Mwisho wa hoja umesema Tuache waislam tuelezee kwanini tunataka mahakama ya kadhi, kumradhi turnabal, badilisha semi yako mara moja, useme kundi Fulani la wababa wa kiislam wasiodhibiti hisia za tamaa zao zilizopindukia na kuoa rundo la wanawake kwa starehe ambao hufa mapema kwa tamaa hizo ndio wanataka waeleze kwanini wanahitaji mahakama ya kadhi, hapo ungeeleweka. Ashkhum

Bi Salma,
MASHALLAH umejaaliwa shoga.Umewapa vidonge vyao nadhani wanaungulia ndani kwa ndani.
Humo kwenye bold kwahusika vilivyo.Muda umefika wanawake wa kiislam wanyanyuke wapaaze sauti zao vilivyo.
Wanaume wataendelea hadi lini kutukalia hadi midomoni? Au kwa vile siye twavaa hijab na kufunika nyuso zetu basi ndo hata sauti tufinike?
Tena wewe Topic na huyo sijui Ally.. mnaojifaya maintelechuo uchwara, tutawapasha na mpeleke ujumbe kwa wenzenu.
1. Hamna nia njema kulazimisha mahakama za Kadhi.Kiketwe alishawagundueni mapemaaa. Akawakata ngebe! Mnachotaka ni kuficha maovu yenu na kuyatafutia baraka ndani ya sheria.Mnajua ndani ya mahakama ya Kadhi, hakuna atakayehoji kitu kwa vile mtajitetea ni agizo la Kuraani tukufu! Mmesahau nchi za Afrika Magharibi - Gambia, Senegal na Naijeria wanawake wamekuwa wakinyanyaswa miaka nenda rudi kwa kisingizio cha dini kumbe uongo mtupu! Hata ukeketaji ulihusishwa na agizo la Mtume ( pbuh)! Hamna hata haya kumsingizia Mtume! Puuh!
2. Hizo tamaa zenu za kuoaoa kila mkitamani sketi ndio zinawaponzeni.Kwanza Tanzania nchi maskini mnaoshindia mlo mmoja kwa siku mna ubavu gani kuoa mke zaidi ya mmoja? Mtawalisha nini? Kama ni tamaa za zinaa si muoe zile ndoa za muda mfupi mkishatenda tendo mtoe talaka kama wafanyavyo wenzenu Arabuni? Hamshangai kwanini nchi kama Indonesia nchi yenye zaidi ya 90% Waislam, ni kinyume cha sheria kuoa zaidi ya mke mmoja! Hii inaondoa upuuzi wenu wa kutesa wanawake.

Salma kaulza hapo juu, wake zenu wakiwataka kimahaba mnaweza? Kwanza siku hizi hata mke mmoja anawatoa nishai ndio itakuwa 2, 3 hadi 4? Kariakoo unakuta mijibaba imepanga foleni ati inanunua " viagra ya kienyeji". Nguvu hamna mnalazimisha kulundika wanawake.Kama siyo kuwataka wake zenu wazini ni nini?

Naishia hapa kwa sasa.Nitarudi.
 

Bi Salma,
MASHALLAH umejaaliwa shoga.Umewapa vidonge vyao nadhani wanaungulia ndani kwa ndani.
Humo kwenye bold kwahusika vilivyo.Muda umefika wanawake wa kiislam wanyanyuke wapaaze sauti zao vilivyo.
Wanaume wataendelea hadi lini kutukalia hadi midomoni? Au kwa vile siye twavaa hijab na kufunika nyuso zetu basi ndo hata sauti tufinike?
Tena wewe Topic na huyo sijui Ally.. mnaojifaya maintelechuo uchwara, tutawapasha na mpeleke ujumbe kwa wenzenu.
1. Hamna nia njema kulazimisha mahakama za Kadhi.Kiketwe alishawagundueni mapemaaa. Akawakata ngebe! Mnachotaka ni kuficha maovu yenu na kuyatafutia baraka ndani ya sheria.Mnajua ndani ya mahakama ya Kadhi, hakuna atakayehoji kitu kwa vile mtajitetea ni agizo la Kuraani tukufu! Mmesahau nchi za Afrika Magharibi - Gambia, Senegal na Naijeria wanawake wamekuwa wakinyanyaswa miaka nenda rudi kwa kisingizio cha dini kumbe uongo mtupu! Hata ukeketaji ulihusishwa na agizo la Mtume ( pbuh)! Hamna hata haya kumsingizia Mtume! Puuh!
2. Hizo tamaa zenu za kuoaoa kila mkitamani sketi ndio zinawaponzeni.Kwanza Tanzania nchi maskini mnaoshindia mlo mmoja kwa siku mna ubavu gani kuoa mke zaidi ya mmoja? Mtawalisha nini? Kama ni tamaa za zinaa si muoe zile ndoa za muda mfupi mkishatenda tendo mtoe talaka kama wafanyavyo wenzenu Arabuni? Hamshangai kwanini nchi kama Indonesia nchi yenye zaidi ya 90% Waislam, ni kinyume cha sheria kuoa zaidi ya mke mmoja! Hii inaondoa upuuzi wenu wa kutesa wanawake.

Salma kaulza hapo juu, wake zenu wakiwataka kimahaba mnaweza? Kwanza siku hizi hata mke mmoja anawatoa nishai ndio itakuwa 2, 3 hadi 4? Kariakoo unakuta mijibaba imepanga foleni ati inanunua " viagra ya kienyeji". Nguvu hamna mnalazimisha kulundika wanawake.Kama siyo kuwataka wake zenu wazini ni nini?

Naishia hapa kwa sasa.Nitarudi.
Kumbe hii mahakama ni ukandamizaji wa wanawake?dah!hawa wababa kweli Mungu atawahukumu.
 
una uhakika hakuna ubaguzi ?

Kama upo huo ndio wa kuuzungumzia. Leta ushahidi kuwa nilienda sehemu fulani kupata huduma ya afya, nikafanyiwa ABC kwa kuwa mimi si mkristo. Au nilienda sehemu fulani kupata huduma lkn nikakuta mazingira yananibana kama muislamu, tuliambiwa tusali kikristo ndio tupate matibabu and some things like that. Lkn kwa huu mtaji wa kukurupuka na mambo yasiyo na msingi kwa kuwa tu Shehe Basaleh kasema, huo ni upotofu usio na mfano. Hospitali, Shule na huduma zingine za jamii zinatolewa kwa wote na mimi sijawahi sikia au kuona haya unayotaka kuyazusha hapa. Tafadhali leta hoja za kweli na sio mambo ya kufikirika na uchochezi.
 
Nauliza hivi: Kwani tatizo liko wapi hadi saasa la kuundwa kwa Mahkama ya Kadhi, kule Znz wenzetu wanayo na mambo yao yanakwenda vyema kwa utatuzi wa masuala ya ndoa/talaka pamoja na mirathi kwa watu wao. Suala kwa mara nyengine huku DSM na Tanganyika tunashinwa ama tunakwama wapi?
 
Nauliza hivi: Kwani tatizo liko wapi hadi saasa la kuundwa kwa Mahkama ya Kadhi, kule Znz wenzetu wanayo na mambo yao yanakwenda vyema kwa utatuzi wa masuala ya ndoa/talaka pamoja na mirathi kwa watu wao. Suala kwa mara nyengine huku DSM na Tanganyika tunashinwa ama tunakwama wapi?

Tanganyika iko wapi?
Wasome wenzio kuanzia mwanzo utafahamu shida iko wapi.
 
Nauliza hivi: Kwani tatizo liko wapi hadi saasa la kuundwa kwa Mahkama ya Kadhi, kule Znz wenzetu wanayo na mambo yao yanakwenda vyema kwa utatuzi wa masuala ya ndoa/talaka pamoja na mirathi kwa watu wao. Suala kwa mara nyengine huku DSM na Tanganyika tunashinwa ama tunakwama wapi?

Hata mimi naona mambo yanakwenda vizuri hasa. Isipochomwa moto bar basi ni kanisa na watuhumiwa badala ya kukamatwa zinapigwa risasi hewani watawanyike. Kweli tupo pamoja.
 
Yup...! 'Mfumo Dume'
Mwenye hizo sheria za Ndoa/talaka na Mirathi atuwekee humu ndani tuone jinsi zinavyofanya kazi !

Utasubiri sana. Wenye mada na washika mapembe wameikimbia mada yao baada ya wanawake wenye akili zao kumwaga ya moyoni. Mi nilifikiri kuna la maana wanataka kumbe ni ufukunyuku tu wa kutaka kudhulumu wajane urithi ili wasifanye kazi saa zote wawe wanacheza bao.

Kiukweli wanawake wa kiislamu wanatakiwa wasimame hasa ili kupata haki. Kumbe ukimuoa ukamla uroda ukikinai unaweza kumpa likizo kwa talaka 2, wewe unaoa mwingine yeye anasubiri. Ukipata hamu tena unamrudia, unaanza tena wallah mbona raha! Ngoja nitafakari other merits, kama vipi na mimi niingie kundini niwe nagonga tendegu naacha, nikipata hamu narudi tena naacha, hivyo hivyo kama mwongozo unavyosema. Haka kamchezo katamu, lazima tukaundie mahakama
 
Nauliza hivi: Kwani tatizo liko wapi hadi saasa la kuundwa kwa Mahkama ya Kadhi, kule Znz wenzetu wanayo na mambo yao yanakwenda vyema kwa utatuzi wa masuala ya ndoa/talaka pamoja na mirathi kwa watu wao. Suala kwa mara nyengine huku DSM na Tanganyika tunashinwa ama tunakwama wapi?

Ningekuwa wewe ningeanza kwanza kum prove wrong Salma2015, ndiyo ningeendelea, kinyume na hapo ni kujidharaurisha kwa kuongea mambo bila hoja wala vielelezo, hata bila vision.

Wasome hao hapo kwanza:
Salma2015
na
Black Rose
Ndipo uendelee.
 
Hakuna aliyekataza ila mnatakiwa muanzishe katika mfumo wa Bakwata na sio kupitia serikali maana Serikal haina dini.Mbona hapo liko waz kabsa!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom