The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,968
- 2,957
Kuna wengi wanaolalamika kwamba walipatwa kuumizwa na utawala wa magufuli. Kuumizwa huko kunahusishwa kibinafsi na utawala wa Magufuli, ikimaanisha walipitia waliyoyapitia tu kwa kuwa Magufuli alikuwa rais.
Wanaolalamika sio wapinzani pekee bali pia wako wanachama wa chama cha mapinduzi ambao wanaona kwakweli Mungu aliwatetea Kwa kumtwaa Rais.
Sehemu kubwa ya malalamiko haya yanatokana na ukweli kwamba katiba ya Tanzania inampa rais madalaka makubwa sana, Kwa kiwango ambacho ana ruhusiwa kuyatumia hata kwenye mitazamo binafsi hakuna mamlaka ya kumuingilia.
Kwa msingi huo nawashangaa sana hasa makada wakubwa ndani ya chama tawala ambao wako bize kufurahia kifo cha marehemu badala ya kuondoa mianya inayoweza kuwaletea Magufuli mwingine au hata zaidi ya Magufuli.
Kwa sababu kwa katiba ilivyo sasa ina mfanya rais kufanya chochote anachoona na asiulizwe wala kuzuiwa na mtu yeyote.
Mnaweza mkawa mmekomaa na kufurahia mkajikuta mara ghafla akapenya mtu wa kaliba ya Magufuli akaikatisha furaha yenu kabisa.
Wanaolalamika sio wapinzani pekee bali pia wako wanachama wa chama cha mapinduzi ambao wanaona kwakweli Mungu aliwatetea Kwa kumtwaa Rais.
Sehemu kubwa ya malalamiko haya yanatokana na ukweli kwamba katiba ya Tanzania inampa rais madalaka makubwa sana, Kwa kiwango ambacho ana ruhusiwa kuyatumia hata kwenye mitazamo binafsi hakuna mamlaka ya kumuingilia.
Kwa msingi huo nawashangaa sana hasa makada wakubwa ndani ya chama tawala ambao wako bize kufurahia kifo cha marehemu badala ya kuondoa mianya inayoweza kuwaletea Magufuli mwingine au hata zaidi ya Magufuli.
Kwa sababu kwa katiba ilivyo sasa ina mfanya rais kufanya chochote anachoona na asiulizwe wala kuzuiwa na mtu yeyote.
Mnaweza mkawa mmekomaa na kufurahia mkajikuta mara ghafla akapenya mtu wa kaliba ya Magufuli akaikatisha furaha yenu kabisa.