Wanaotafuta dawa ya kuacha ulevi tukutane hapa

Wanaotafuta dawa ya kuacha ulevi tukutane hapa

mediaman

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2011
Posts
451
Reaction score
688
Baba yangu mzazi aliishi maisha ya dhiki sana. Alikuwa mfanyakazi aliyepata mshahara mzuri tu lakini mshahara ulikuwa haumsaidii kuishi vizuri kwa sababu ya ulevi. Mwisho wa mwezi, akishapokea mshahara tu alikuwa anakesha sehemu wanazouza bia akinywa na kuwanunulia bia marafiki zake. Wanawake walikuwa wanamganda sana, naye hakukosa kuwagawia pesa.

Saa anapokumbuka kurudi nyumbani pesa zote(noti) mfukoni zimeisha. Siku hiyo ya mshahara baba akifika nyumbani mama alikuwa anafurahi kwakuwa alijua atapata pesa za kununulia chakula na mahitaji muhimu kwakuwa baba amepokea mshahara. Furaha ya mama ilikuwa inageuka huzuni baba anapomtupia vijisenti vilivyobakia baada ya kutoka kwenye ulevi.

Baba na mama walikuwa wakigombana mara kwa mara kwa sababu ya maisha hayo na yaliendelea kwa miaka mingi hadi baba alipopata dawa iliyomwezesha kuacha ulevi. Baada ya kupata dawa hiyo, akipata mshahara alikuwa anakuja nao wote nyumbani na kupanga matumizi na mama. Maisha yalianza kuwa ya furaha.

Kuna watu wengi wanaishi hivyo. Wanapata pesa lakini hazikai, zinaishia kwenye ulevi huku watoto wao wakilala njaa na kukosa ada ya masomo. Na wengine wamepigwa chupa za bia na kusababishiwa majeraha. Wengine wamekutwa mitaroni kwa sababu ulevi uliwazidia wakajikuta wameanguka na kulala popote pale. Kwa ujumla ulevi umewasababishia watu wengi maisha ya dhiki, huzuni na majuto. Wasioyafurahia maisha hayo wanatafuta sana njia au dawa ya kuacha ulevi lakini hawapati. Baba yangu alipata mashauri mengi na mapendekezo ya dawa za kuacha ulevi.

Alijaribu yote lakini hayakumsaidia, hadi siku moja alipoipata "dawa" ya ajabu. Dawa yenyewe ni rahisii tu na hainunuliwi kwa pesa: Aliyakabidhi maisha yake kwa Yesu. Alitubu na kuamua kuacha kabisa maisha yote ya dhambi kisha akampokea Yesu moyoni mwake kwa imani awe Bwana na Mwokozi wake.

Kuanzia hapo alipata uwezo wa kushinda vishawishi vyote vya ulevi. Marafiki zake walipokuwa hawamuoni vilabuni, walishangaa na kujiuliza ni kweli ameacha ulevi? Siku zilivyoenda, waliamini kuwa ni kweli ameacha. Hiyo ndio dawa, tusitafute dawa nyingine zaidi ya hiyo.
 
Wengine wameenda kwa YESU ila sasa wamerudi wanakunywa tena nini shida? wengine tuliwapeleka kwa tiba asili wakafanyiwa matambiko wakaacha kabisa, sasa wanakunywa. ingawa wote hawa unywaji wao wa sasa ni kawaida tofauti na zamani. kwakweli mambo ya imani (iwe dini, au mizimu au n.k) yanasaidia
 
wengine wameenda kwa YESU ila sasa wamerudi wanakunywa tena nini shida? wengine tuliwapeleka kwa tiba asili wakafanyiwa matambiko wakaacha kabisa, sasa wanakunywa. ingawa wote hawa unywaji wao wa sasa ni kawaida tofauti na zamani. kwakweli mambo ya imani (iwe dini, au mizimu au n.k) yanasaidia
Shida ni hiyo uliyoisema. Walienda kwa Yesu kisha wakarudi. Nafikiri hao hawakuwa wameamua kwa dhati kukaa kwa Yesu daima. Matokeo yake waliposhawishiwa kuurudia unywaji, walikubali wakajikuta wanakunywa tena.
 
Viwanda vya bia ndiyo vinaongoza kwa uaminifu kuchangia pato la taifa! Na wakati wa majanga vinatoa sana kuliko walokole feki!
Kiufupi baba yako alikuwa mkarimu sana, alipoacha akawa na robo mbaya kwa watu kuwatoa
Unazungumzia nchi gani? Japan? Japan pato la taifa linachangiwa na viwanda gani? Viwanda vya bia vitaendelea tu kuwepo. Point hapa ni jinsi ya kuwasaidia wanaoteseka na unywaji.
 
Lazaro Nyalandu alimgaragaza Tundu Lissu kwenye kura za kamati kuu!

Huyu mzee wa MIGA, mwanasheria a Acacia anaaminika na nani sasa kama hadi kamati kuu anashindwa kura?
 
Lazaro Nyalandu alimgaragaza Tundu Lisu kwenye kura za kamati kuu.!

Huyu mzee wa MIGA ,mwanasheria a Acacia anaaminika na nani sasa kama hadi kamati kuu anashindwa kura??
Off topic, mkuu
 
wengine wameenda kwa YESU ila sasa wamerudi wanakunywa tena nini shida? wengine tuliwapeleka kwa tiba asili wakafanyiwa matambiko wakaacha kabisa, sasa wanakunywa. ingawa wote hawa unywaji wao wa sasa ni kawaida tofauti na zamani. kwakweli mambo ya imani (iwe dini, au mizimu au n.k) yanasaidia
Mkuu fafanua hapo unaposema unywaji wao wa sasa ni tofauti na zamani.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom