KERO Wanaotuuzia maji ya DAWASA Wakazi wa Mbezi Makabe hadi Msumi wakati hatuna huduma wao wanayapata wapi?

KERO Wanaotuuzia maji ya DAWASA Wakazi wa Mbezi Makabe hadi Msumi wakati hatuna huduma wao wanayapata wapi?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

NBica

Member
Joined
Sep 13, 2010
Posts
39
Reaction score
36
Wakati Wananchi wenzetu wa maeneo mbalimbali wakilalamika adha ya kukosa huduma ya maji, huku kwetu Wakazi wa Mbezi Makabe hadi Msumi hali siyo nzuri na ni kama tumeshazoea hali hiyo.

Tunapata adha ya kukosa maji japokuwa tuna mabomba ya DAWASA, Maji yanaweza yasitoke hata wiki tatu bila maelezo yoyote na yakitoka yatatoka baadhi ya maeneo tu.

Ajabu hayo maji ya DAWASA ambayo hayatoki kwetu kuna magari yanakimbizana kutuuzia maji hayo ya DAWASA, Dumu la Lita 1,000 tunauziwa kwa kwa Tsh. 15,000/= hadi 20,000/=

Swali la msingi tunalojiuliza wengi wetu hawa wanaouza maji ya DAWASA wanayapata wapi kwa wingi huo na kwanini sisi hatupati?

Hii kero tunaomba Serikali itusaidie maana imekuwa ya miaka mingi, hata Watu kudhani DAWASA wanakata maji ili hao Wafanyabiashara ya maji wapate fursa ya kufanya biashara yao.
 
Wakati Wananchi wenzetu wa maeneo mbalimbali wakilalamika adha ya kukosa huduma ya maji, huku kwetu Wakazi wa Mbezi Makabe hadi Msumi hali siyo nzuri na ni kama tumeshazoea hali hiyo.

Tunapata adha ya kukosa maji japokuwa tuna mabomba ya DAWASA, Maji yanaweza yasitoke hata wiki tatu bila maelezo yoyote na yakitoka yatatoka baadhi ya maeneo tu.

Ajabu hayo maji ya DAWASA ambayo hayatoki kwetu kuna magari yanakimbizana kutuuzia maji hayo ya DAWASA, Dumu la Lita 1,000 tunauziwa kwa kwa Tsh. 15,000/= hadi 20,000/=

Swali la msingi tunalojiuliza wengi wetu hawa wanaouza maji ya DAWASA wanayapata wapi kwa wingi huo na kwanini sisi hatupati?

Hii kero tunaomba Serikali itusaidie maana imekuwa ya miaka mingi, hata Watu kudhani DAWASA wanakata maji ili hao Wafanyabiashara ya maji wapate fursa ya kufanya biashara yao.
Wakati wa uchaguzi serikali ya mtaa kuna gari lao lilikuwa linapaki hapo kwa ribaba wanagawa maji bure
Vp bado lipo

Ova
 
Wanayatoa pale mbezi shule karibu na daraja la mto mbezi ,waziri yuko bize huko kwao tanga ishi ya maji mtajijua

USSR
 
Wananunua dawasa, pale mbezi mwisho karibu na ofisi za Tanesco.
 
Back
Top Bottom