Wanaozunguka nchi nzima kushawishi umma ukubaliane na mkataba mbovu wa DP World ndio hao hao watakaosema mama anaupiga mwingi tukiachana nao

Wanaozunguka nchi nzima kushawishi umma ukubaliane na mkataba mbovu wa DP World ndio hao hao watakaosema mama anaupiga mwingi tukiachana nao

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Huwa najaribu kujiuliza, hawa wenzetu wameumbwaje? Sijawahi kupata jibu. Akili zao zinafanya kazi vipi, huwezi kuelewa.

Mkataba wa DP WORLD ni mbovu, na unatunyonga sisi wenyewe. Tunapiga kelele vifungu vibovu virekebishwe, lakini CCM wamekuwa wakitumia kodi zetu kuzunguka nchi nzima wakisema huo mkataba hauna ubaya wowote uko sawa tu.

Presha sasa imekuwa kubwa, mabaya ya mkataba wa DP WORLD yanawekwa bayana hadi vilabuni huko vijijini ndani ndani kabisa.

Naamini muda si mrefu, huenda mama akasalimu amri na kuachana na DP WORLD.

Mtashangaa hawahawa ambao wamezunguka nchi nzima wakiusifia mkataba wa DP WORLD kuwa ni mzuri na hauna kasoro, ndio hao hao watakaozunguka tena nchi nzima wakimsifia mama kwamba anaupiga mwingi, mkataba ulikuwa haufai.

Yangu macho, yajayo yanafurahisha
 
Screenshot_20230821-034156_Lite.jpg
 
Mimi ni mtanzania na ninaunga mkono mkataba wa DP WORLD....huna nguvu ya kunifutia uraia wangu [emoji1787]
sijapewa Landcruiser na Million 500 kama wenzangu walioenda dubai ! Namimi nikipata hivyo naweza kuutetea mkataba...maana hakuna aliyepata io mgao na akathubutu kuupinga mkataba wanajua kabisa hela walishakula na wakiiambiwa warejeshe hawana hata kumi.
 
Wewe ni Mtanzania kweli?
Hapana, nilipachikwa tu Utanzania, mimi nimezaliwa Tanganyika, nimekulia Tanganyika, nimeanza kusoma Tanganyika. Akaja nyerere ghafla yu ananambia "wewe sasa Mtanzania".

Hivi unajuwa nyerere aliipeleka wapi Tanganyika? Au ndiyo imeolewa ikapoteza jina lake kama wafanyavyo wagala?
 
Wanafikiri kwa kutumia tumbo
Wanatusumbua Nchi nzima tunashindwa hata kumtizama Kwa mapana ELIMU ya vizazi vijavyo itakuwaje, wao kutwa kucha wanawaza maslah binafsi,

Viongozi wasio na maono ni Janga la Taifa.
 
Back
Top Bottom