Wanasaikolojia mlioko JamiiForums kwanini ukiwa na Hela husikii Njaa ila ukiwa huna Njaa itakuandama sana?

Wanasaikolojia mlioko JamiiForums kwanini ukiwa na Hela husikii Njaa ila ukiwa huna Njaa itakuandama sana?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Nimeambiwa ni tokeo la Kisaikolojia hivyo nami GENTAMYCINE Kazi yangu Kubwa katika huu Uzi ni Kusoma tu Maoni ( Comments ) zenu nielimike zaidi na ikiwezekana hata Nishibe kabisa kwani hapa nina Njaa hatari.
 
Kisaikolojia zaidi mpishi "Chief" havutiwi na chakula alichopika mwenyewe!
 
😁😁😁
Sijui kama ipo kisayansi ila ukiifikiria ngono lazma hormones zifanye kazi yake na usisimke

Pengine ukifikiria utakula nini kwa muda mrefu lazma mfumo ushtuke kuwa unahitaji chakula ila pesa ukiwa nayo huwezi kufikiria
 
Uliza na hii biashara ikichamganyia ukawa unapiga pesa ndefu nyege zinakta hata muda wa kuwaza madem au kutafuta madem unakosa
Ila January biashara amna unakuwa idol nyege sasa ndo zinaanza kiherehere [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mimi sababu ni moja tu nikiwa na kibunda mitungi inakuwa mingi sasa ile nyongo inasumbua appetite
 
Pesa na elimu ni defensive kwamba ukiwa navyo vinakulinda ukiwa na pesa unaweza kuingia hata hotelini ukala bure hii inafanywa na baadhi ya wauza hoteli ili kukuvutie pale.

Ukiwa na elimu unaweza kupewa heshima hata kweny sehemu isiyohitaji elimu mfano unaweza kupewa hta cheo katika ukoo katika mambo ya kiukoo.

Ukiwa na pesa njaa haiwezi kukuandama kwa sababu tayar nafsi yako iko huru kutoka kweny njaa kwamba kiakili unajua utakula tu kwa namna yeyote ile.

Ntakupa mfano sisi mtaani tukienda kucheza mechi enzi izo tulikuwa tunagombania jersey ila Kuna jamaa ni fundi wa mpira anajua sana huwezi kumkuta anagombania mnaweza kuvaa nyote ila wakija piga hesabu Kuna mtu atavuliwa jersey jamaa anayohitaji ili aanze kikosi cha kwanza na anacheza mwanzo mwisho...point yangu hanaga stress coz uwezo wake unambeba ivyo ivyo ukiwa na pesa unajiamini kama kula utakula tu.

Hakikisha unakuwa na pesa na elimu ni vitu vizuri sana katika defensive mechanism.
 
Hili jambo ni kweli tupu.

Siyo pesa nyingi unazokusanya kidogo kidogo, ni zile fedha za mkupuo kupata mamillioni ama mabillioni ghafla bin vuu, ndozinachanganya akili kinyama!

Pesa zitokanazo na kubahatisha madini ama mafao, wizi nk nk.

Hilo jambo mie liliwahi kunitokea zamani, baada ya kujaza begi la hela, nyekundu tupu bila hata kujua idadi ya hesabu yake.

Nilishindwa kula muda wa siku3 sipati njaa kabisa hadi nilipododoswa na washikaji zangu kwanini hawajaniona kula tangia juzi, je naumwa?

Ndipo nikakumbuka kweli sijala siku3 na bado sisikii njaa, nadhani bila kushituliwa ningedanja kwa njaa bila kujijua wala kuhisi!

Ikabidi nianze kujilazimisha kula biskuti na vimiminika huku natembea, eti naona kukaa na kuanza kula ni kupoteza muda, zilinichanganya!

Nikajaa hofu nikawa simuamini kila mtu, nikihisi kila nayekutana naye tayari kagundua kama nina hela, presha ikawa juu!

Ikawa silitui begi langu kutoka mgongoni, usiku nalala nalo, nadhani nilitaka kuchanganyikiwa!

Ninachojiuliza mpaka leo, ni kitu gani kilichoua njaa kwa siku tatu hadi nilipokumbushwa kula?

Hali hiyo nilidhani ilinitokea mimi tu, kumbe ni tatizo la "umma", ngoja nisikilize wazoefu!
Ikabidi nianze kujilazimisha kula biskuti na vimiminika huku natembea, eti naona kukaa na kuanza kula ni kupoteza muda, zilinichanganya


Hatari kwa afya Yako...
 
Back
Top Bottom