Wanasheria msaada wenu tafadhari

Orketeemi

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2013
Posts
5,063
Reaction score
12,866
Kwanza salaam.
Nilinunua laptop tar 31.1.2014. Arusha mjini na nikapew warranty ya mwaka mmoja. Baada ya kuitumia kwa miez 2 imekufa spika nikaipeleka tar 10 mwez huu, wakaniambia baada ya week 2 nikaichukue lakin leo wamenipigia sim inaonesha wamshindwa kurekebisha. Je nini nifanye?
 
Kama umeirudisha kwa ajiri ya kosa la kiufundi (technical defect) na wala si kosa lako mfano labda kuingusha au kuifundugua na kugusa gusa vitu fulani temper with computer bado hiyo warranty inafanya kazi. Hakuna kwa namna yoyote atakana uwajibikaji, kwa hiyo wakileta za kuleta wewe wapeleke mahakamani. Onyo, kama ni makosa yako then ni bora husijisumbue
 
Nashukuru sana,. Si kosa langu maana sijaiwah kuiangusha wala kuifungua popote
 
lakini kwanza hujasema wamekwambia inakuwaje, wameshindwa kwa hiyo? Umewaomba hela yako wakataa ama wamesemaje? Wame suggest nini.

Halafu hujasema warranty ni ya duka ama ya mtengenezaji. Risiti inasemaje? Unayo risiti yenyewe? Juzi jamaa yangu kanunua mu-electronics wa bei mbaya zaidi ya milioni hakupewa risiti ili eti "apunguziwe VAT," na wewe ulichukua risiti au "ulipunguziwa VAT"?
 
Risiti ya mwenye duka,.
Nimeona kama kuna ujanja ujanja unataka kufanyika, walinipigia muda ambao ilikuwa si rahisi kwenda maana nipo Moshi ila nmewaambia nitaenda kesho asubuhi. Kinachouma kingine ni nauli za moshi-Arusha
 
Risiti ya mwenye duka,.
Nimeona kama kuna ujanja ujanja unataka kufanyika, walinipigia muda ambao ilikuwa si rahisi kwenda maana nipo Moshi ila nmewaambia nitaenda kesho asubuhi. Kinachouma kingine ni nauli za moshi-Arusha

na ww bhana! kwan mosh hamna maduka ya laptop!" .........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…