Wanasheria mtusaidie katika hili. Tunaangamizwa watanzania wenzenu

Wanasheria mtusaidie katika hili. Tunaangamizwa watanzania wenzenu

mkataba wa kazi ninao

Hayo matatizo ni mengi kwenye asasi zetu za serikali..hebu jaribu kuwasiliana na afisa utumishi wa hapo ulipo mara nyingi wanachelew kupeleka majina yenu na mikataba ya ajira utumishi na kusababishwa kuchelewa kutoka kwa cheque namba..utumishi wataanza kukutambua pale tu utakapoanza kuwa na hiyo cheque namba.. Inawezekana kabisa tatizo ni la hapo ulipo
 
unganeni na muishtaki wizara husika, I hope mna kumbukumbu za usaili mliofanyiwa na barua za kuitwa kazini. Hilo ni tatizo dogo sana msiogope mmeshashinda. Mkiona hamuwezi sana nendeni LHRC
 
kama mkataba unao manake unakuonesha nani mwajiri wako,kimsingi huyo ndo unaweza kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. Hapa umesema mko kama hamsini hivi,hatujajua mnataka shitaka lenu kuwa la kawaida(ordinary civil suit) au la uwakilishi (representative civil suit) ni lazima kujua kuwa kwa mjibu wa sheria hapa kuna taratibu tofauti za kufuata kufungua mashitaka hayo.
sijajua uko maeneo yapi lakini kama unaweza mtafute mwanasheria karibu yako au kituo chochote kinachotoa msaada wa kisheria,kwa ushauri zaidi,mana atakuwa na nafasi ya kupitia mkataba wako na kuona haki zako ziko namna gani.
Ingawa kwa maelezo yako inaonekana mnahaki ya kulipwa sitahili zenu. Usiogope tatizo watanzania wengi ni waoga sana linapokuja swala la kumshitaki mwajiri wako. Unapopigania haki yako hupaswi kuwa mwoga wala kukata tamaa,haki ya mtu haiwezi kupotea mwanadamu atakachofanya ni kuichelewesha tu,kila la heri na mungu akutangulie.
 
Maneno hayatoshi kua ushahidi...
Tatizo ni kutotambuliwa na kuingizwa kwenye system tu?
 
Back
Top Bottom