Wanasheria naomba jibu?

Mndwyika.wetu

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2012
Posts
652
Reaction score
829
Kikatiba ni wakati gani maandamano ya wanachi yanapokua halali na wakati gani yanakua haramu?

Je maandamano ni hisani kutoka polisi?

Je katiba inasema maandamano halali ni yale tu ya kuunga nkono na kusifia wakuu ?

Maandamano yakiwa ni ya kupinga, kulalamika (picketing) yanakua haramu?
 
Tusubiri waje tuwasikie
 
mbona sasa ushatoa jibu unataka sie tukujibu nini tna
 
Tunatakiwa kujua kwamba katiba ni sheria mama inayotoa haki tu ila namna ya hio haki, mipaka ya hio haki na utaratibu wa kuipata hio haki hua inatolewa na sheria zingine za bunge, ndo maana kwenye katiba hakuna sehemu inasema ukiuua kwa kukusudiwa basi unyongwe!

Ni ukweli kua katiba inatoa haki ya maandamano kwa watu, taasisi nk bila bugdha au kuathiri sheria zingine za nchi, ibara ya 30 ya katiba inasema kua ibara zilizomo ndani ya katiba hazi haramishi sheria nyingine za nchi.

Sasa maandamano yana ratibiwa na kuandaliwa chini ya sheria ya jeshi la polisi na kazi saidizi ambayo inataka ili maandamano yawepo basi yafaa kwanza waandaji wa maandamano waombe kibali cha maandamano hayo masaa 48 kabla ya kuandamana... Na endapo hili halitofuatwa basi maandamano hayo hayatakua halali kisheria, lakin endapo polisi wakikataa kutoa kibali icho basi wandamanaji wanaweza kufungua kesi mahakama kuu chini ya hati ya dharura wakiwashtaki mwanasheria mkuu wa serikali na mkuu wa jeshi la polisi waieleze mahakama sababu hasaa ni nini ya kuwanyima watu haki yao ya kikatiba.

Lakini kitu cha juu Kabisa kuliko vyote kwenye mfumo wa sheria ni busara, endapo itaonekana maandamano yale yalikua yana ulazima sanaa na uharaka sanaa kuinusuru jamii basi yatakua halali na ya haki bila hata kibali chochote kwa kile kitakachoitwa "kwa manufaa ya jamii".
 
Nasubir kupata elimu ya sheria wanasheria acheni uvivu na ubahiri tuelimisheni watz wenzenu jmn
 
Lipo tatizo moja la sheria za Tanzania, inakupa jambo kwa mkono wa kulia kisha inakupoka kwa mkono wa kushoto.
Maandamano yameruhusiwa kikatiba, hvyo ni Constitutional right, lakini katiba hyo hyo imeweka masharti ya kufuata ili kufanya maandamano, hivyo sio Absolute right. Masharti hayo ni kuomba ulinzi wa polisi(kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa). Sheria ya polisi inaipa jeshi la polisi mamlaka ya kuzuia kutendeka jambo lolote ambalo wanaamini litahatarisha amani na usalama wa nchi. Sasa ukizisoma katiba na sheria ya vyama vya siasa , na ya jesh la polisi 'kwa ujumla wake', utaona polisi hawana mamlaka ya kuzuia mikutano, bali inatoa fursa ya polisi na waandamanaji kukubaliana muda na mazingira ya ufanyikaji maandamano hayo. Sasa wakubwa wanalijua hli ndio maana mapendekezo ya sheria mpya ya vyama vya siasa yanajaribu kuweka masharti makali kidogo.
 

Haya tuambie nani anaetoa kibali cha maandamano?
 
Absolutely.
Ahsante kwa Elimu nzuri na muhimu.
 
apo kwenye kutoa kibali tu ndo tatizo.ata kama ya halali polisi lazima washirikishwe iwe ni kwa ajili ya kuwalinda au kukataa kutokana na sababu zao
 
Mi naona logic ni nzuri sana ya polisi kuwa notified maana waandamanaji watahitaji kuwa na ulinzi pia watu wengine ambao hawaandamani wanahitaji kupata ulinzi na usalama.

Bila hayo, wahuni na wezi wangetumia maandamano kama kichaka cha kufanya wizi na kuhatarisha amani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…