ISMAIL MKIMBIZI
Senior Member
- Jan 13, 2013
- 192
- 23
Familia yetu Baba, mama, mimi na wadogozangu wawili tumefunguliwa mashitaka katika mahakama ya mwanzo na tayari tumepokea samasi kufika mahakamani hapo tarehe 10 mwezi huu.
HISTORIA YA MGOGORO
1. Baba yetu amekuwa na mgogoro wa Ardhi (kiwanja) na jirani yetu kwa muda mrefu sana.
2. 2008 Baba yetu alimshitaki huyo mzee jirani yetu kuvunja uzio na kuingia kwenye kiwanja chake baba akashinda katika Baraza la Kata.
3. Huyo mzee jirani akakata rufaa wilayani Baraza la Ardhi akashindwa pia. Baba akashinda.
4. Akakata rufaa nyingine Mahakama kuu kitengo cha ardhi, Jaji akagundua makosa katika hukumu ile hakuamua mshindi ni nani akatoa amri kesi hiyo ikasikilizwe upya chini ya mwenyekiti mwingine asiwe yule ambaye alimpa ushindi baba. Sababu ya jaji kuirudisha wilayani ni kwamba mwenyekiti aliandika katika hukumu yake kuwa wazee wa baraza walikubaliana na hukumu ya kata na kutoa maoni yao kuwa mshindi ni baba, lakini kwenye hukumu hapakuwa na maoni yoyote yaliyoandikwa kuthibitisha alivyosema katika hukumu. Hivyo ikaonekana kama kaiamua yeye kama yeye sio jopo la yeye na wazee wa baraza, kwamba hakuwatendea haki pande zote mbili.
5. Ilivyosikilizwa upya, huyo mkata rufaa jirani yetu amemshinda baba.
6. Baba ameomba rufaa mahakama kuu amepewa samasi kumwita huyo mzee jirani kufika mahakamani mwezi wa tano.
7. Wanae wa huyo mzee jirani baada ya ushindi wa mzee wao wakavamia eneo la mgogoro wakavunja uzio na kupanda mahindi na maharage upande mmoja. Na upande wetu tukapanda upande mwingine kwa kuridhika kutofanya vurugu kwa kuwa Rufaa imeombwa tusubiri mahakama iamue tusifanye fujo kwa uvamizi wao.
8. Huyo jirani ameibuka na samasi kutoka mahakama ya mwanzo na hati ya amri ya kizuizi cha baraza la ardhi la wilaya akidai tumedharau amri halali ya Baraza.
9. Baba anashangaa kuona hati hiyo huku akisema hajawahi kuambiwa hata kwa mdomo na Mwenyekiti wa baraza au mtu yeyote barazani kuwa anazuiliwa kufanya kitu eneo la mgogoro ambalo kuna machungwa aliyopanda, mapera na migomba kwa zaidi ya miaka (30) thelathini iliyopita. Anadai ana uhakika M/kiti na huyo jirani wamemtega kwa kuwa alihofia uendeshaji wa kesi wa m/kiti akamripoti TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA kitu kilichozua uhasama wa baba na mwenyekiti huyo aliyediriki kumtishia kwa maneno makali Baba pale barazani kuwa ataona nani zaidi kati ya mwenyekiti wa TUME na yeye. Kwamba wametengeneza kizuizi hicho kisiri siri wamtie hatiani.
10. Tumeshitakiwa Baba, mama, mimi na wadogo zangu wawili (jumla watano) kisa eti tumepanda mahindi na maharage ,huwa tuna chuma machungwa, tunavuna ndizi, tunafyeka nyasi nk kwenye eneo lenye kizuizi cha mahakama. Tunajiuliza maswali
(a) Kizuizi kinazuia upande mmoja mwingine unaruhusiwa kufanya kazi eneo lenye mgogoro?
(b) Kizuizi kinatolewa kwa siri sio wazi na kwa nini anapewa huyo jirani yetu baba hatarifiwi akapewa na yeye?
(c) Kizuizi hicho cha Baraza la wilaya kina nguvu wakati Baba amekata rufaa na imepokelewa Mahakama Kuu?
(d)Tufanyeje siku tukifika mahakama ya mwanzo kama njia ya kujitetea?
(e) Mtu akipatikana na hatia hiyo ya kukiuka amri ya baraza adhabu yake/zake ni zipi?
Ndugu wanasheria tunaomba msaada wenu.
HISTORIA YA MGOGORO
1. Baba yetu amekuwa na mgogoro wa Ardhi (kiwanja) na jirani yetu kwa muda mrefu sana.
2. 2008 Baba yetu alimshitaki huyo mzee jirani yetu kuvunja uzio na kuingia kwenye kiwanja chake baba akashinda katika Baraza la Kata.
3. Huyo mzee jirani akakata rufaa wilayani Baraza la Ardhi akashindwa pia. Baba akashinda.
4. Akakata rufaa nyingine Mahakama kuu kitengo cha ardhi, Jaji akagundua makosa katika hukumu ile hakuamua mshindi ni nani akatoa amri kesi hiyo ikasikilizwe upya chini ya mwenyekiti mwingine asiwe yule ambaye alimpa ushindi baba. Sababu ya jaji kuirudisha wilayani ni kwamba mwenyekiti aliandika katika hukumu yake kuwa wazee wa baraza walikubaliana na hukumu ya kata na kutoa maoni yao kuwa mshindi ni baba, lakini kwenye hukumu hapakuwa na maoni yoyote yaliyoandikwa kuthibitisha alivyosema katika hukumu. Hivyo ikaonekana kama kaiamua yeye kama yeye sio jopo la yeye na wazee wa baraza, kwamba hakuwatendea haki pande zote mbili.
5. Ilivyosikilizwa upya, huyo mkata rufaa jirani yetu amemshinda baba.
6. Baba ameomba rufaa mahakama kuu amepewa samasi kumwita huyo mzee jirani kufika mahakamani mwezi wa tano.
7. Wanae wa huyo mzee jirani baada ya ushindi wa mzee wao wakavamia eneo la mgogoro wakavunja uzio na kupanda mahindi na maharage upande mmoja. Na upande wetu tukapanda upande mwingine kwa kuridhika kutofanya vurugu kwa kuwa Rufaa imeombwa tusubiri mahakama iamue tusifanye fujo kwa uvamizi wao.
8. Huyo jirani ameibuka na samasi kutoka mahakama ya mwanzo na hati ya amri ya kizuizi cha baraza la ardhi la wilaya akidai tumedharau amri halali ya Baraza.
9. Baba anashangaa kuona hati hiyo huku akisema hajawahi kuambiwa hata kwa mdomo na Mwenyekiti wa baraza au mtu yeyote barazani kuwa anazuiliwa kufanya kitu eneo la mgogoro ambalo kuna machungwa aliyopanda, mapera na migomba kwa zaidi ya miaka (30) thelathini iliyopita. Anadai ana uhakika M/kiti na huyo jirani wamemtega kwa kuwa alihofia uendeshaji wa kesi wa m/kiti akamripoti TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA kitu kilichozua uhasama wa baba na mwenyekiti huyo aliyediriki kumtishia kwa maneno makali Baba pale barazani kuwa ataona nani zaidi kati ya mwenyekiti wa TUME na yeye. Kwamba wametengeneza kizuizi hicho kisiri siri wamtie hatiani.
10. Tumeshitakiwa Baba, mama, mimi na wadogo zangu wawili (jumla watano) kisa eti tumepanda mahindi na maharage ,huwa tuna chuma machungwa, tunavuna ndizi, tunafyeka nyasi nk kwenye eneo lenye kizuizi cha mahakama. Tunajiuliza maswali
(a) Kizuizi kinazuia upande mmoja mwingine unaruhusiwa kufanya kazi eneo lenye mgogoro?
(b) Kizuizi kinatolewa kwa siri sio wazi na kwa nini anapewa huyo jirani yetu baba hatarifiwi akapewa na yeye?
(c) Kizuizi hicho cha Baraza la wilaya kina nguvu wakati Baba amekata rufaa na imepokelewa Mahakama Kuu?
(d)Tufanyeje siku tukifika mahakama ya mwanzo kama njia ya kujitetea?
(e) Mtu akipatikana na hatia hiyo ya kukiuka amri ya baraza adhabu yake/zake ni zipi?
Ndugu wanasheria tunaomba msaada wenu.