Wanasheria upande wa mafisadi ni wa kuogopa kama ukoma

Wanasheria upande wa mafisadi ni wa kuogopa kama ukoma

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Katika suala la kukodisha bandari zetu tujifunze kitu kimoja kikubwa. Kwamba taaluma ya sheria inapotumiwa na mafisadi ni hatari kama ukoma kwenye jamii.

Siku moja tu imepita tumewasikia wanasheria wizara ya ujenzi na uchukuzi wakiwa na waziri wao wakijaribu kutetea uamuzi wa serikali kutaka kuipa falme ya dubai usimamizi na uendeshaji bandari zetu zote kuanzia bahari, maziwa na mito. Na pia kuwapa miundombinu yote inayohusika na utendaji wa bandari hizo kuzisimamia. Uamuzi kama huo bila shaka unatikisa uhuru wa nchi yoyote. Na kwa kuanzia eti watafanya makubaliano na kampuni mali ya mfalme wa dubai kuanza kuendesha bandari ya dar es Salaam.

Nalotaka kuonesha hapa ni jinsi wanasheria wa wizara walivyotetea usiri wa majadiliano yao hadi makubaliano ya kuiteua kampuni ya DPworld huku tayari nchi ikiwa imeshaingia mkataba kukabidhi shughuli zake zote za bandari kwa dubai.

Wanasheria hao wanadai eti washindania wa ksndarasi ndio wanaotaka usiri bila kuelewa kwamba wananchi na jamii inataka uwazi. Nia ya kushindanisha kampuni ni ili kila moja itoe bei yake halisi kufuatana na gharama zake na sio kama kucheza kamari kubahatisha nani anaweza kumpiga bei ya juu kabisa mteja.

Licha katika nadharia ya ubepari dhana ya kwanza kua ndio sahihi lakini ukweli dhana ya pili kucheza kamari ili kumpiga mteja ndio inatumika. Hapo ndio makampuni yanataka usiri na kutumia mbinu chafu za kila aina wakati umma unataka uwazi ili yule mwenye weledi na teknolojia kuweza kutoa ofa ya bei ya chini ndio ashinde kandarasi.

Jambo la kushangaza ni jinsi wanasheria wa wizara walivyoweza kutetea matakwa ya wakandarasi kudai kataka usiri na kuona madai ya umma kutaka uwazi kama sio sahihi. Hapo ndio tunaona shida na hatari nchi kubebeshwa kupewa huduma kwa gharama kubwa ambazo pengine wala sio mahitaji yake ils ni kutokana na vishawishi tu vya biashara za kimataifa kutafuta soko.

Baadhi ya wanasheria wa wizara ambao nadra kuonekana mbele ya umma walionekana kua na siha njema sana hadi kimoyoni mtu kuweza kuhoji vipato vyao kama ni mishahara na marupurupu ya kikazi pekee.
 
Kwenye swala la ulinzi wa rasilimali zetu.... hakika aliijua kesho yetu!....

aliona hadi pale uono wa macho yetu ulipokomea!

Aliishi ile kauli..."Watanzania mniombee"

Aliiona kesho yetu...

Ulale pema peponi jasiri muongoza njia....

tumeachwa nyikani! Wala sio njiani!
Itoshe tu kusema......

' Tutakukumbuka daima milele'
 
Kwenye swala la ulinzi wa rasilimali zetu.... hakika aliijua kesho yetu!....

aliona hadi pale uono wa macho yetu ulipokomea!

Aliishi ile kauli..."Watanzania mniombee"

Aliiona kesho yetu...

Ulale pema peponi jasiri muongoza njia....

tumeachwa nyikani! Wala sio njiani!
Itoshe tu kusema......

' Tutakukumbuka daima milele'
Mkuu jamaa alikuwa na uchungu na rasilimali za taifa. Alichagua wasaidizi shupavu. Angalia Umeme, maji porojo tupu.
 
Kwenye swala la ulinzi wa rasilimali zetu.... hakika aliijua kesho yetu!....

aliona hadi pale uono wa macho yetu ulipokomea!

Aliishi ile kauli..."Watanzania mniombee"

Aliiona kesho yetu...

Ulale pema peponi jasiri muongoza njia....

tumeachwa nyikani! Wala sio njiani!
Itoshe tu kusema......

' Tutakukumbuka daima milele'
 
Mkuu jamaa alikuwa na uchungu na rasilimali za taifa. Alichagua wasaidizi shupavu. Angalia Umeme, maji porojo tupu.
Shauri yenu, zusheni na zidisheni kila mnalojisikia. Watu wameshawastukia na kuwapuuza na agenda yenu ya kijinga!!
 
Shauri yenu, zusheni na zidisheni kila mnalojisikia. Watu wameshawastukia na kuwapuuza na agenda yenu ya kijinga!!
Upatikanaji wa Umeme, maji ukoje leo. Miaka miwili ya uongozi uzushi na hali halisi mtaani kwako ikoje? Rushwa huduma hospitalini. Kusikilizwa kwa ofisi zote za umma mtanzania yoyote?
 
Umeme ulikuwa upo miaka mitano ya JPM. Sasa hivi visingizio havitoshi mara maji, mvua , crane na ujinga mwingine.
Sijui huko, huku kwetu haujawahi kuwa changamoto ya kihiiivyo. Kukiwa na tatizo ukipiga tu makao makuu wanakufikia ndani ya dakika.
 
Katika suala la kukodisha bandari zetu tujifunze kitu kimoja kikubwa. Kwamba taaluma ya sheria inapotumiwa na mafisadi ni hatari kama ukoma kwenye jamii.

Siku moja tu imepita tumewasikia wanasheria wizara ya ujenzi na uchukuzi wakiwa na waziri wao wakijaribu kutetea uamuzi wa serikali kutaka kuipa falme ya dubai usimamizi na uendeshaji bandari zetu zote kuanzia bahari, maziwa na mito. Na pia kuwapa miundombinu yote inayohudika na utendaji wa bandari hizo kuzisimamia. Uamuzi kama huo bila shaka unatikisa uhuru wa nchi yoyote. Na kwa kuanzia eti watafanya makubaliano na kampuni mali ya mfalme wa dubai kuanza kuendesha bandari ya dar es Salaam.

Nalotaka kuonesha hapa ni jinsi wanasheria wa wizara walivyotetea usiri wa majadiliano yao hadi makubaliano ya kuiteua kampuni ya DPworld huku tayari nchi ikiwa imeshaingia mkataba kukabidhi shughuli zake zote za bandari kwa dubai.

Wanasheria hao wanadai eti washindania wa ksndarasi ndio wanaotaka usiri bila kuelewa kwamba wananchi na jamii inataka uwazi. Nia ya kushindanisha kampuni ni ili kila moja itoe bei yake halisi kufuatana na gharama zake na sio kama kucheza kamari kubahatisha nani anaweza kumpiga bei ya juu kabisa mteja.

Licha katika nadharia ya ubepari dhana ya kwanza kua ndio sahihi lakini ukweli dhana ya pili kucheza kamari ili kumpiga mteja ndio inatumika. Hapo ndio makampuni yanataka usiri na kutumia mbinu chafu za kila aina wakati umma unataka uwazi ili yule mwenye weledi na teknolojia kuweza kutoa ofa ya bei ya chini ndio ashinde kandarasi.

Jambo la kushangaza ni jinsi wanasheria wa wizara walivyoweza kutetea matakwa ya wakandarasi kudai kataka usiri na kuona madai ya umma kutaka uwazi kama sio sahihi. Hapo ndio tunaona shida na hatari nchi kubebeshwa kupewa huduma kwa gharama kubwa ambazo pengine wala sio mahitaji yake ils ni kutokana na vishawishi tu vya biashara za kimataifa kutafuta soko.

Baadhi ya wanasheria wa wizara ambao nadra kuonekana mbele ya umma walionekana kua na siha njema sana hadi kimoyoni mtu kuweza kuhoji vipato vyao kama ni mishahara na marupurupu ya kikazi pekee.

Ni vyema umebadili nyimbo, ilikuwa "bandari imeuzwa" sasa imekuwa "kukodisha bandari".
".

Mengine hayo ni porojo zako tu. Unajiaminisha ujinga tu.
 
Kwahiyo kila Mtanzania ana umeme na maji ya kuaminika.

Jukumu la serikali ni nini?
Hata kipindi hicho unachokifanyia reference, si kila mtanzania alikuwa na umeme na maji ya kutosha. Sijasema hivyo pia!
 
Hata kipindi hicho unachokifanyia reference, si kila mtanzania alikuwa na umeme na maji ya kutosha. Sijasema hivyo pia!
Umeme, maji ulikuwa vizuri. Rushwa serikalini ilipungua sana Ulisikilizwa hata kama ulikua mlalahoi. Hospitalini ofisi zote za umma.
 
Upatikanaji wa Umeme, maji ukoje leo. Miaka miwili ya uongozi uzushi na hali halisi mtaani kwako ikoje? Rushwa huduma hospitalini. Kusikilizwa kwa ofisi zote za umma mtanzania yoyote?
Wewe umelala kweli kweli, unafahamu umeme wetu wa gas sasa Watanzania wanakwenda kuwafungia Zambia? Ulianza wakati wa Kikwete, mwendazake akauzuwia miaka 6, kuondoka tu watu sasa wanauuza nje ya Tanzania.


Unafahamu haohao Watanzania wanaweka huo umeme Zanzibar hivi sasa> Combination ya solar na gas?

Hivi nyinyi mko wapi, Mmelala?
 
Back
Top Bottom