Sehemu kubwa ya magomvj ya sisi Watanzania husababishwa na kitu kimoja tu, ambacho ni ugumu wa kusema neno SAMAHANI.
Hata sijui kwanini tunakuwa hivi? Hata humu JFkuna shida hiyo, mtu yuko radhi msiongee tena, ili tu akwepe kusema SAMAHANI.
Iko wazi kuwa Jide ana kazi ngumu katika hii kesi, kwa sababu Gadner hakumtaja kwa jina, hivyo kuna shughuli ya kujithibitisha kama ni yeye aliyezungumzwa.
Sasa kwanini wafike huku kote? Wakati Gadner anajua kama pale alimzungumzia Jide? Ugumu kusema neno SAMAHANI tu?
Sijui tunatengeneza jamii ya aina gani? Hasa humu kwenye mitandao, kila mtu anajifunza kuwa kiburi na kuonesha umwamba kwa mwenzie?
Hakuna tena kupingana kwa hoja, ila kutukanana na kudhalilishana tu. Tena wengi wa watu wa hivi hawana hata muda wa kujiongeza.
Hasomi vitabu na wala hajiongezi kielimu, ila yeye yuko hapa kukera watu hasa wanaoonekana wana heshima na kuaminiwa. Na hata wakijua wamewakosea hawataki kusema SAMAHANI.
Ova