Wanasheria wa Reginald Mengi wakutana na waandishi wa habari na Kumjibu Rostam Aziz

Wanasheria wa Reginald Mengi wakutana na waandishi wa habari na Kumjibu Rostam Aziz

Status
Not open for further replies.
...mkutano wa mengi leo unatakiwa kuzuiwa na vyombo vya usalama ..kwa kuwa unaaingiza nchi kwenye malumbano yasiyoisha .....muda wa mengi kuanza kusumbuliwa na dola wazi umefika ..uvumilivu wao umefika kikomo...

sio mengi tu hata rostam hatakiwi kuzungumza tena....wote wameongea sasa waachie polisi na mahakama zifanye kazi...wasigawe wananchi..

katika taratibu za kawaida za usalama ndio hivyo...sasa ndio tutajuwa kama kweli rais ameapa kulinda usalama wa wananchi au la...hatuwezi kuwa na taifa la kiumbea umbea wa kusutana kama wake wenza ...miaka mitano yote tumekalia kusutana tu hakuna kinachofanyika .... we are tied with this weak gorvernment....watuache tufanye kazi!!

Kumfungia Mengi kutokuongea ni kujaribu kumnyamazisha ili asitoboe siri za ufisadi unaoimaliza nchi. Usalama gani unahatarishwa kwa watu tu kuongea hasa kama wanayoongea ni 'umbea'?

Hatari niionayo mimi ni kwa JK kutokuyafanyia kazi yanayoongelewa na ni kwa vile tu yanamhusu na yeye.
 
Unajua garama za kupload kwa bongo @ kapinga

kweli ulaya raha...maana access ambazo mtu unakuwa unazipata kwa urahisi halafu huko kwetu inakuwa ni ndoto...inasikitisha na kutia hasira sana..!
 
jamani mimi sio mwana siasa! napenda mtu akiongea atoe facts and ushahidi kamili....

ataje majina,tarehe na places..... SIO POROJO!!!
 
Atueleze leo pesa alizokopa za kuzalisha hakuna matata zimeishia wapi naona rostam hakusema hili jana pamoja na ile mitambo ya kiwanda ni serikali imemsaidia kujenga kiwanda kile akakifilisi
 
Nafahamishwa na mwandishi wetu kuwa wameambiwa atafanya Press Conference SI ofisini kwake bali Royal Palm (Movenpic) Hotel.


mmiliki wa royal palm hotel na kempski ni mmoja....mwarabu wa kempski..ila ameamua kuwacha jina royal palm kwa sababu za kibiashara[these are sister companies]

kama amesusa kempski basi akienda royal palm ni kama kuruka mavi na kuikanyaga mkojo...yote ni uchafu tu!!

aende peacork kama anataka hoteli ambayo mafisadi aliowataja hawana chembe ya share!!!
 
katiba ya nchi inampa kila mtu uhuru wa kuongea ili mradi asivunje sheria, wewe unaejifanya "mwanausalama" kwa nini unataka kuwaziba watu midomo, waacheni waongee wakichoka watalala, serikali isijiingize kwenye hili jambo, kwani ni mpaka pale mmoja wa hawa atakapoamua kulipeleka suala kwenye sheria, mahakamani hapo ndipo litatakiwa likemewe na serikali kuwa wanaingilia uhuru wa mahakama. Kwa sasa kumzuia mtu ku "vent emotions" ni kutumia madaraka vibaya na kuvunja katiba.

Mengi ni ordinary citizen mwenye uhuru wa kutoa mawazo yake kama mwananchi, wa kuzuiwa ni ra ambaye yeye ni elected official ambaye anakidhalilisha chama chake kwa kuongea na ordinary citizen.

Hakuna polisi wala uwt, wakati wa udikteta umeisha kumbuka "the culture of silent" is no longer practical in tanzania.

you gal stop flooding
 
mmiliki wa royal palm hotel na kempski ni mmoja....mwarabu wa kempski..ila ameamua kuwacha jina royal palm kwa sababu za kibiashara[these are sister companies]

kama amesusa kempski basi akienda royal palm ni kama kuruka mavi na kuikanyaga mkojo...yote ni uchafu tu!!

aende peacork kama anataka hoteli ambayo mafisadi aliowataja hawana chembe ya share!!!

Una uhakika gani na hili mkuu??
 
Vipi mlioko Dar, huo mkutano wa Mengi na Waandishi wa habari umesha anza??? tunaomba updates
 
Bado watu wamezima simu au sijui kuna jam ya simu eneo lile manake simu haziingii
 
point ni kwamba Mengi hatoi facts, ushahid mzito hana!...

tunaboeka nae!.... na kama angetokea mtu mwengine ambae hana hela ("not rich") akaongea kama RM, unadhani angelikuwepo wapi sasa?
 
mmiliki wa royal palm hotel na kempski ni mmoja....mwarabu wa kempski..ila ameamua kuwacha jina royal palm kwa sababu za kibiashara[these are sister companies]

kama amesusa kempski basi akienda royal palm ni kama kuruka mavi na kuikanyaga mkojo...yote ni uchafu tu!!

aende peacork kama anataka hoteli ambayo mafisadi aliowataja hawana chembe ya share!!!

mkuu hivi mkutano na waandishi wa habari lazima afanyie hotelini?Si anaweza akaenda hata hapo mnazi mmoja akaitisha press.
 
HEBU SOMA KITU HICHI ALICHOANDIKA MH MAHANGA

Ninavyojua mimi ni kwamba kama mtu hawezi kupeleka malalamiko yenye ushahidi fulani (hata kama si kamili) kwenye vyombo vya dola, ni vigumu sana vyombo hivyo kufanyia kazi tuhuma hizo. Kwa mtazamo wako unataka wananchi waachane na mkondo huu wa sheria na walalamike na kuwashitaki wanaodhani ni waovu kwa umma! Ili iweje? Wapigwe mawe? Wazomewe ili waache ufisadi? Kwa njia hii tuna hakika wataacha? Au nchi itakuwa salama? Mimi nadhani hii ni hatari.

Kwa mtazamo wako na hao wengine ni kwamba Tanzania kwa utawala bora ni sifuri kabisa na sasa wananchi wamekosa imani na serikali, na mahakama na vyombo vyote vya dola, na sasa wako tayari kuchukua mkondo wa mob justice. Je, mnataka wananchi waingie mitaani wawapige mawe wanaodhaniwa mafisadi au watawala wabovu, au wawatoe Ikulu kwa nguvu watawala waliopo sasa? Na hii eti ni kwa sababu wakifuata mkondo wa sheria kwa kutoa ushahidi polisi, takukuru na mahakamani ushahidi utaharibiwa na dola au hautafanyiwa kazi!

Huo mtazamo kwamba nchi hii haina utawala bora kiasi hicho mimi sikubaliani nao, na hata taasisi za kimataifa zinazopima utawala bora katika nchi mbalimbali hawakubaliani na mtazamo wako huo kwamba TZ ni ya mwisho mwisho katika utawala bora. Kwa kweli kinyume chake ndiyo kweli, kwamba TZ inasifiwa kwa jitihada zake za utawala bora kulinganisha na nchi nyingi za Afrika, hata zote zinazoendelea duniani. Ushahidi huu hata wewe unaujua.

Vile vile yaonekana wewe na wenzako mnadai kwamba serikali ya TZ haijali kabisa matatizo na kero na umasikini wa wananchi wake, bali matumbo ya watawala na washikaji wao. Hili nalo si kweli, ingawa suala la rushwa (kama ilivyo kwa nchi karibu zote duniani) bado ni tatizo hapa kwetu. Lazima tuendelee kukemea na kupiga vita rushwa kwa kufuata utawala wa sheria na haki za raia wote.

Lakini juhudi za serikali kuboresha huduma za jamii na kupambana na umasikini (kilimo, elimu, afya, maji, miundombinu na kupunguza umasikini nchini na kusaidia ajira hasa za kujiajiri, na hata kupambana na hiyo rushwa) ni kubwa sana na zinaonyesha jinsi serikali inavyojali wananchi wake. Angalia mgawanyo wa bajeti ya Taifa kwenye sekta hizo kila mwaka.

Wewe Ngurumo unajua pia kwamba nchi na taasisi wafadhili duniani hawapeleki misaada kwa nchi ambazo serikali yake haipangi bajeti yake kwa vipaumbele vya kulenga wananchi wake (pro-people budget) wala nchi ambapo utawala bora ni zero. Lakini angalia jinsi TZ inavyopata misaada mingi kuliko nchi nyingi kutokana na vigezo hivyo kuwaridhisha wafadhili. Hivi wao wameshindwa kuona hayo mnayoyaona nyie ya utawala mbovu na kutowajali wananchi? Hapana, sikubaliani na hilo.

Kuhusu ushahidi wa Dr. Slaa kukataliwa Bungeni, hili sina hakika nalo sana, lakini sijui kwanini hakupeleka ushahidi huo polisi au takukuru? Wangeziharibu? Huwezi kupeleka ushahidi kama huo ukaacha kubaki na nakala zako.

Kwamba tunapokuwa serikalini hatujui matatizo ya wananchi mpaka ati nije niache ubunge na uwaziri nirudi kuwa mwananchi wa kawaida ndipo nijue shida zao, si kweli. Tunazijua sana kero hizo (tunaishi nao) na zinatuumiza vichwa sana. Kiongozi mzuri ni yule anapotaka uongozi wa watu ajue anakwenda kushughulikia kero za hao wananchi, na si masilahi yake. Na mimi naamini asilimia kubwa sana ya viongozi wetu ni wa aina hiyo. Wanajali shida za wananchi.

Lakini hapa ninaloliona ni wananchi wengi kupiga siasa muda wote, badala ya kungojea msimu wa uchaguzi wafanye maamuzi ya kuchagua viongozi/chama kulingana na ahadi walizotoa, ili kabla ya hapo wajizatiti kufanya kazi kwa bidii kujiondolea umasikini. Tatizo ni CCM kuwakera watu wanaodhani ni muda muafaka kubadili chama tawala, lakini bila kungoja kutumia sanduku la kura. Tatizo ni kuwakosanisha wananchi na serikali/chama tawala kwa kushikilia mambo au jambo ambalo kwa ujumla wake halina tija kubwa sana kwa watanzania walio wengi bali lina mtazamo wa ubinafsi, chuki, wivu na uelekeo wa kisiasa.

Milton
 
Mengi hana jipya la kuongea, hana ushahidi wowote wa madai yake, ila ni kama kawaida yake ni kulialia na kutaka wananchi wawe pamoja naye wakati yeye mwenyewe ni fisadi nyangumi hapa hakuna wahindi wala wamasai fisadi ni fisadi tu! umezowea kuparamia paramia watu lakini mara hii umeparamia mbuyu, hatuwezi kukuamini maneno yako ya porojo eti kwa kuwa wewe mweusi yeye mweupe, ndio unakotupeleka huko. Hadi sasa RA 3 MENGI 0
 
na hao mabwana kwa kuonyeshana vijisenti hawajambo, huyu kafanyia Kempisk... huyu leo ni Movenpick... si waende Idara ya Maelezo hizo hela tunazihitaji huko Mbagala kwenye mabomu. Tumeshakwepeshwa na issue za wabunge kujiongezea mishahara, Bongo bwana ni rahisi sana kutumisdirect
 
Tired of this..
Hivi haiwezekani kuwaweka wote wawili pamoja na kuwa na kitu kama MDAHALO???
 
Mengi hana jipya la kuongea, hana ushahidi wowote wa madai yake, ila ni kama kawaida yake ni kulialia na kutaka wananchi wawe pamoja naye wakati yeye mwenyewe ni fisadi nyangumi hapa hakuna wahindi wala wamasai fisadi ni fisadi tu! umezowea kuparamia paramia watu lakini mara hii umeparamia mbuyu, hatuwezi kukuamini maneno yako ya porojo eti kwa kuwa wewe mweusi yeye mweupe, ndio unakotupeleka huko. Hadi sasa RA 3 MENGI 0


Kweli unahasira nae sana, ukweli ni kuwa wote(Mengi na Rostam) ni MAFISADI. Sasa sijui anataka kutuambia nini sisi watanzania masikini.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom