Wanasiasa Tanzania wamewameza wachumi na wanasheria

Wanasiasa Tanzania wamewameza wachumi na wanasheria

MPadmire

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2006
Posts
3,957
Reaction score
3,245
Ukiangalia hii nchi, mambo ya kiuchumi yanaenda ovyo sana.

Shilingi inazidi kushuka thamani, leo ni 1680 TSHS kwa DOla moja ya Marekani

Kilimo Kwanza imekuwa ni kelele tu na kuwapa mabeberu/mabepari ardhi ya Tanzania kwa kisingizio cha uwekezaji

Watu wanajali maendeleo ya vitu badala maendeleo ya watu

Siasa chafu ndo inatawala hii nchi

Wachumi wa Tanzania hii siwasikii hata wakiongea katika vyombo vya habari na kupaza sauti ama kutoa ushauri... Nchi hii kuna wachumi? Vyuo vikuu Mzumbe, UDSM, SUA e.t.c, Where are you?
 
Mbaya zaidi Tanzania tunaimport hata vitu vya aibu, mpaka toothpick kutoka china

Vijana wameachwa hoi bin taaban, vijana wanaendesha boda boda badala ya kuzalisha export products

Vijana ni bomu litakaloilipukia CCM,
 
Wachumi wenyewe ndio hao kina Kikwete na Mwigulu Nchemba.
 
Wale wanaojiita wasomi wote feki. Hata wasomi tuliokuwa tunawaona na kuwasikia nao wamejiunga kwenye behewa la wasomi feki na wamekuwa feki tu. Angalia arguments zao! Hazina mashiko kabisa. Tuna ma-Prof. na ma-Dr. lukuki lakini mmh....!! Wapi Wangwe, Nguyulu, Beno, ....... na wengine wengi. Mbona kimya?? Msitunyamazie, taifa litaangamie.
 
Mtaalam WA kilimo Profesa Kikwete bado hajarudi toka Vietnam utamsikia mtaalam wetu mpya
 
Ukiangalia hii nchi, mambo ya kiuchumi yanaenda ovyo sana.

Shilingi inazidi kushuka thamani, leo ni 1680 TSHS kwa DOla moja ya Marekani

Kilimo Kwanza imekuwa ni kelele tu na kuwapa mabeberu/mabepari ardhi ya Tanzania kwa kisingizio cha uwekezaji

Watu wanajali maendeleo ya vitu badala maendeleo ya watu

Siasa chafu ndo inatawala hii nchi

Wachumi wa Tanzania hii siwasikii hata wakiongea katika vyombo vya habari na kupaza sauti ama kutoa ushauri... Nchi hii kuna wachumi? Vyuo vikuu Mzumbe, UDSM, SUA e.t.c, Where are you?


Kabla hujaanza kuwalaumu hao angalia hapa JF jukwaa linaloongoza kwa kutembelewa, jukwaa kama hili ambalo kwa asilimia themanini kama siyo tisini linaweza kumsaidia kijana kujikwamua kimaisha linatembelewaje ukilinganisha na jukwaa la siasa.
 
Kabla hujaanza kuwalaumu hao angalia hapa JF jukwaa linaloongoza kwa kutembelewa, jukwaa kama hili ambalo kwa asilimia themanini kama siyo tisini linaweza kumsaidia kijana kujikwamua kimaisha linatembelewaje ukilinganisha na jukwaa la siasa.
Exactly brother!I agree with you.
 
Kabla hujaanza kuwalaumu hao angalia hapa JF jukwaa linaloongoza kwa kutembelewa, jukwaa kama hili ambalo kwa asilimia themanini kama siyo tisini linaweza kumsaidia kijana kujikwamua kimaisha linatembelewaje ukilinganisha na jukwaa la siasa.
Ni ukweli kuwa waTanzania wengi tu ni makanjanja. Wanachojali ni kuwa na karatasi (vyeti) na kujipachika sifa za kisomi(Profesa, Dr.) lakini kivitendo ni kama shule ya msingi. Ushahidi nenda kwenye maktaba za vyuo vikuu uangalie ni asilimia ngapi ya vitabu/machapisho ni vya wasomi wa ndani. Ndogo mno. Si wasomi wa vyuoni tu hata makazini utendaji hauendani na sifa walizonazo wataalamu wetu. Hali ni hivyo kwa wataalamu wa kilimo, madaktari, mainjinia, n.k. Nahisi mfumo wa elimu unahusika kwa kiasi kikubwa.
 
Back
Top Bottom