Wanataka 150,000/= ili nipate hati ya nyumba

Wanataka 150,000/= ili nipate hati ya nyumba

Pole mleta uzi, Kwa changamoto uliyo kutanana nayo. Naomba nikupe elimu kidogo;
Zoezi la Urasimishaji Makazi, kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali ni Kwamba Kila Mmiliki wa Ardhi atachangia Shilingi Laki Moja na Elfu Hamsini (150,000). Hii gharama itahusisha kazi zifuatazo;
1. Kutambua Mipaka ya Kiwanja/Eneo lako
2. Kuandaa Michoro ya Mipango Miji, Hii itaonesha Matumizi Mbalimbali ya Ardhi (Makazi, Biashara Shule n.k)
3. Kupima (Kuweka alama za Upimaji Ardhini, hapa ndio panahusisha zoezi la upandaji mawe maalumu ya Upimaji, kuonesha mipaka kati ya Kiwanja na Kiwanja au Kiwanja na Barabara).

Baada ya Haya mazoezi matatu kukamilika na Ramani zote kusajiliwa na Wizara (kiwanja kikapata namba, pamoja na Kitalu). Hapo ndio inakua Mwisho wa matumizi ya ile Laki Moja na Elfu Hamsini (150,000/=).

Kazi hizo nilizo zitaja hapo juu Zinaweza Fanywa na Wataalamu wa Ardhi kutoka Halmashauri Husika au Makampuni Binafsi.

Baada ya Kukamilika sasa kwa zoezi la Upangaji na Upimaji, zoezi linalofuata ni Umilikishaji. Hapa sasa kile kiwanja chako kinatakiwa kitengenezewe Hati.

Hati hazitolewi Bure; Kuna gharama ambazo mmiliki wa Kiwanja Anapaswa kuzilipa kwa Serikali ili aweze Kumilikishwa. Gharama za hati huwa hazilingani kama zile za Upangaji na Upimaji. Gharama za hati zinategemea Vitu vikubwa vitatu;
1. Ukubwa wa Kiwanja
2. Matumizi ya Kiwanja
3. Mahali kiwanja Kilipo.
Kwa mfano; Kiwanja cha makazi chenye ukubwa wa Mita za Mraba 1,000 kilichopo Katikati ya Mji, Gharama zake za hati hazita Fanana na Kiwanja Chenye ukubwa kama Huo ila matumizi yake ni Ya Biashara.

Kwa Kifupi;
Kuna Gharama za Upimaji na Gharama za Umilikishaji (Hati), tofauti kubwa Gharama sa Upangaji na Upimaji zinaweza Kulipwa hata kwa Kampuni Binafsi kupitia Akaunti za Benki.
Ila gharama za Hati zinalipwa Serikalini peke yake, Na siku izi malipo yote ya Serikali, ni lazima yafanyike kwa Control Number.

Mtoa mada Unaweza tumia huu kama Muongozo kutatua changamoto yako.
 
Pole mleta uzi, Kwa changamoto uliyo kutanana nayo. Naomba nikupe elimu kidogo;
Zoezi la Urasimishaji Makazi, kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali ni Kwamba Kila Mmiliki wa Ardhi atachangia Shilingi Laki Moja na Elfu Hamsini (150,000). Hii gharama itahusisha kazi zifuatazo;
1. Kutambua Mipaka ya Kiwanja/Eneo lako
2. Kuandaa Michoro ya Mipango Miji, Hii itaonesha Matumizi Mbalimbali ya Ardhi (Makazi, Biashara Shule n.k)
3. Kupima (Kuweka alama za Upimaji Ardhini, hapa ndio panahusisha zoezi la upandaji mawe maalumu ya Upimaji, kuonesha mipaka kati ya Kiwanja na Kiwanja au Kiwanja na Barabara).

Baada ya Haya mazoezi matatu kukamilika na Ramani zote kusajiliwa na Wizara (kiwanja kikapata namba, pamoja na Kitalu). Hapo ndio inakua Mwisho wa matumizi ya ile Laki Moja na Elfu Hamsini (150,000/=).

Kazi hizo nilizo zitaja hapo juu Zinaweza Fanywa na Wataalamu wa Ardhi kutoka Halmashauri Husika au Makampuni Binafsi.

Baada ya Kukamilika sasa kwa zoezi la Upangaji na Upimaji, zoezi linalofuata ni Umilikishaji. Hapa sasa kile kiwanja chako kinatakiwa kitengenezewe Hati.

Hati hazitolewi Bure; Kuna gharama ambazo mmiliki wa Kiwanja Anapaswa kuzilipa kwa Serikali ili aweze Kumilikishwa. Gharama za hati huwa hazilingani kama zile za Upangaji na Upimaji. Gharama za hati zinategemea Vitu vikubwa vitatu;
1. Ukubwa wa Kiwanja
2. Matumizi ya Kiwanja
3. Mahali kiwanja Kilipo.
Kwa mfano; Kiwanja cha makazi chenye ukubwa wa Mita za Mraba 1,000 kilichopo Katikati ya Mji, Gharama zake za hati hazita Fanana na Kiwanja Chenye ukubwa kama Huo ila matumizi yake ni Ya Biashara.

Kwa Kifupi;
Kuna Gharama za Upimaji na Gharama za Umilikishaji (Hati), tofauti kubwa Gharama sa Upangaji na Upimaji zinaweza Kulipwa hata kwa Kampuni Binafsi kupitia Akaunti za Benki.
Ila gharama za Hati zinalipwa Serikalini peke yake, Na siku izi malipo yote ya Serikali, ni lazima yafanyike kwa Control Number.

Mtoa mada Unaweza tumia huu kama Muongozo kutatua changamoto yako.
Nashukuru sana kwa maelezo mazuri kabisa ambayo yamenifungua pakubwa mno na nimejua pakuanzia , inamaana pindi ntakapo rudi ntawaomba wanipatie control number kwa ajili ya kufanya malipo . Ila ili pendeza vitu kama hivi wangekuwa wanatupa elimu kidogo na kwa kupitia haya maelezo ntakuwa mjumbe mzuri kwa wengine watakao kitana na sintofahamu kama yangu .
 
Kuna hati ya nyumba?
Nadhani ni hati ya urasimishaji wa makazi , nilikosa namna nzuri ya kuandika hapo ila ukisoma vizuri nahisi naweza kueleweka hasa nilikuwa nimemaanisha nini .
 
NDEFU KIDOGO

Habari zenu wakuu , nadhani wote tunalikumbuka vizuri lile zoezi la urasimishaji liloanza chini ya raisi wa awamu ya tano marehemu jpm . Ukiachilia mbali changamoto zake , moja ya mambo ambayo mimi kama raia nilifurahia ni jinsi ambavyo wananchi tuliweza kujua hatua kwa hatua juu ya mchakato mzima wa urasimishaji wa ardhi na makazi kwa kupitia mikutano mbali mbali ya mitaa ambayo alianzishwa kwa lengo lakumjuza mwananchi nini kinatakiwa .

Nakumbuka vizuri hatua ya kwanza ni ilikuwa ni kuandaa mkutano ambao uliwashirikisha pia maafisa ardhi ambao walitupa elimu nzuri kabisa juu ya faida ya kupimiwa maeneo yetu namna ya upimaji utakavyokuwa lakini pia hata gharama za upimaji , hakika ilikuwa ni mkutano mizuri sana , afisa ardhi alisema kila " mwananchi atatakiwa atoe kiasi cha sh 150, 000/= tu kwani kiasi kingine serikali yetu pendwa ilikuwa imetusaidia katika kukilipa " hakika tulipaga makofi ndelemo na vifijo juu ya taarifa hii nzuri aliyotolewa na bwana àrdhi yule . Baada ya hapo tulipimiwa maeneo yetu ikifatiwa na usimikwaji wa bicon ( bikoni ) na kuna form ambayo ilitakiwa kila mtu ampatie jirani yake aliyepakana naye aiweke sahihi ili kujiridhisha kuwa bicon zilizowekwa mipakani ziwekwa sahihi kabisa . Ikimbukwe michakato hii yote ilihusisha mikutano ya hadhara ambayo mara nyingi ilifanyika kila mtaa kwa uwazi kabisaa .

Hatimaye zoezi lilofuata baada ya hayo yote ilikuwa ni utoaji wa hati kwa wale wotee waliokwisha maliza michakato tajwa hapo juu , kwa mtazamo wangu nilifikiri hili pia lingeanzia kwenye mikutano ya mitaa wananchi tupewe taarifa kuwa hati zipo tayari pia tuelekezwe taratibu zote zin azotakiwa ili kama itawezekana kila mwananchi akajichukulie hati yake kiurahisi kabisa .


Lakini katika hali ya kushangaza jana nimepigiwa simu na mtu aliyejitambulisha yupo ofisi za ardhi , akinitaka leo siku ya jumamosi tarehe 17 , nifike katika ofisi zao ili nikajichukulie hati yangu . Leo nimeitikia wito ila nimeambiwa natakiwa nitoe laki na nusu (tsh 150,000/=) ndipo nipatiwe hatii nikajalibu kuwakumbusha juu ya ile laki na nusu tuliyowapa kipindi zoezi hili limeanza nikajibiwa kuwa ile ilikuwa ni kwa ajili ya upimaji na hii ya sasa ni kwa ajili ya hati hivyo ni vitengo viwili tofauti . Nikajitetea kwa kusema sawa " mimi leo nilikuja kwa ajili ya kuitikia wito tu sikujua kama natakiwa pia kuja na hicho kiasi mlichonitajia , hivyo naombeni muda nikajipange na pindi nitakapo pata basi nitawaleteeni hicho kitita cha laki unusu mnachokiitaji " mmoja akasema sawa lakini jitahidi si unajua tena ma-file ni mengi ukichelewa linaweza kupotea wakaniruhusu nitoke nikiwa na maswahili yafuatayo

- kwanini watu hawa hawaja taka kulitolea ufafanuzi shwala hili la gharama ya hati kama walivyofanya huko nyuma kwa kuhitisha mikutano na kuwajuza wananchi juu ya jambo hili ?..

  • kweli kiasi hiki cha sh 150,000/= walichokitaka ni sahihi au kuna harufu ya upigaji inayoninyemelea hapa ??..
  • sawa kama kiasi hiki ni sahihi nakilipa kwa njia ipi ya benki au nawapa tu cash mkononi ??..

Hitimisho
Nikiwa katika dimbwi hili la maswali kimoyo moyo Nikasema hamna shida kule jamiiforum kuna watu wana- deal na mambo haya wanaufahamu wakutosha sana ngoja nikawaulize ili nipate undani wa swala hili. Je wadau hichi nilichokutana nacho ni sahihi ???
MImi nilitaka kurasimisha nyumba wilaya ya kibindoni nikaambiwa nilipe 650,000/=!
 
Hakuna rushwa mkuu.
Upimaji ardhi ulikuwa ni kama anasa kabla ya punguzo mkuu.

HIyo ya 150k ni ya upimaji tu tena ni punguzo kwani nusu ililipwa naserikalu.

Baada ya upimaji utaenda kulipia hati baada ya hesabu ya ukubwa wa kiwanja chako

Kama sio rushwa kwa nini hawatoi contro number
 
Mkuu, kwani wew hujuwi kama urasimu umerudi. Kuna eneo lilipimwa tukaambiwa kama tunauwezo tulilipie na kama hatuna uwezo basi baadhi ya eneo wachukue ardhi.

Siku nimeenda kulipia napewa akaunti namba ya kawaida, nikaomba Control namba nikaambiwa haina haja, daaah nikahis kupigwa.., Yaani zoezi la kulipia likasimama mpaka leo, tatizo la Tz kila mwenye kicheo ni kuwaza upigaji tu.
Ni kweli huu mfumo wa kulipia bank upo mkuu, sio huko pekee
 
Ukweli ni kuwa 150,000 haitoshi kabisa kupima na kupata hati, Mara nyingi wanawadanganya ili ukubali kupimiwa, wakikuambia mwanzon hadi upate hati ni Laki 5 utakimbia, ila ukishapata Ramani ya upimaji kwa laki na nusu, mbele mambo yanakuwa hivyo, na hiyo laki na nusu nyingine kama ni Dar haitoshi
 
Kama sio rushwa kwa nini hawatoi contro number
Hayo ni malipo ya Kampuni watakupa risiti, malipo ya serikali utapewa control number ambapo kuna reg fee ya certificate 50,000, Application 20,000, deed plan 20,000, Premium 0.5 ya market value, land rent, na reg fee
 
Yaani ni kutokufahamu tu, ingekuwa mimi ningeitoa hiyo laki na nusu chap tu kama ninayo, kikubwa wamenipa control number.

Post #21 ya mkuu Komba the Great kamaliza kila kitu.
 
Mimi pia moja kwa moja nilihisi kuna kitu hakipo sawa hapa , ila nikaona ngoja nisijitie ujuaji kwa kuwa kuna watu wanauelewa juu ya haya mambo ngoja niwashilikishe nijue undani wake

Pole mleta uzi, Kwa changamoto uliyo kutanana nayo. Naomba nikupe elimu kidogo;
Zoezi la Urasimishaji Makazi, kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali ni Kwamba Kila Mmiliki wa Ardhi atachangia Shilingi Laki Moja na Elfu Hamsini (150,000). Hii gharama itahusisha kazi zifuatazo;
1. Kutambua Mipaka ya Kiwanja/Eneo lako
2. Kuandaa Michoro ya Mipango Miji, Hii itaonesha Matumizi Mbalimbali ya Ardhi (Makazi, Biashara Shule n.k)
3. Kupima (Kuweka alama za Upimaji Ardhini, hapa ndio panahusisha zoezi la upandaji mawe maalumu ya Upimaji, kuonesha mipaka kati ya Kiwanja na Kiwanja au Kiwanja na Barabara).

Baada ya Haya mazoezi matatu kukamilika na Ramani zote kusajiliwa na Wizara (kiwanja kikapata namba, pamoja na Kitalu). Hapo ndio inakua Mwisho wa matumizi ya ile Laki Moja na Elfu Hamsini (150,000/=).

Kazi hizo nilizo zitaja hapo juu Zinaweza Fanywa na Wataalamu wa Ardhi kutoka Halmashauri Husika au Makampuni Binafsi.

Baada ya Kukamilika sasa kwa zoezi la Upangaji na Upimaji, zoezi linalofuata ni Umilikishaji. Hapa sasa kile kiwanja chako kinatakiwa kitengenezewe Hati.

Hati hazitolewi Bure; Kuna gharama ambazo mmiliki wa Kiwanja Anapaswa kuzilipa kwa Serikali ili aweze Kumilikishwa. Gharama za hati huwa hazilingani kama zile za Upangaji na Upimaji. Gharama za hati zinategemea Vitu vikubwa vitatu;
1. Ukubwa wa Kiwanja
2. Matumizi ya Kiwanja
3. Mahali kiwanja Kilipo.
Kwa mfano; Kiwanja cha makazi chenye ukubwa wa Mita za Mraba 1,000 kilichopo Katikati ya Mji, Gharama zake za hati hazita Fanana na Kiwanja Chenye ukubwa kama Huo ila matumizi yake ni Ya Biashara.

Kwa Kifupi;
Kuna Gharama za Upimaji na Gharama za Umilikishaji (Hati), tofauti kubwa Gharama sa Upangaji na Upimaji zinaweza Kulipwa hata kwa Kampuni Binafsi kupitia Akaunti za Benki.
Ila gharama za Hati zinalipwa Serikalini peke yake, Na siku izi malipo yote ya Serikali, ni lazima yafanyike kwa Control Number.

Mtoa mada Unaweza tumia huu kama Muongozo kutatua changamoto yako.
We mngoni acha kujifanya mjuaji. Hiyo pesa wanayotaka ni halali kabisa.
Waambie wakupe control number ukalipie
 
Uko sahihi mdau nami pia nililipa 120,000 ambapo niliambiwa ni gharama za upimaji. Baadaye nilipigiwa tena hesabu nyingine kulingana na ukubwa wa kiwanja na mpaka sasa nilishapewa hati
Mkuu, hiyo gharama uliyotozwa kulingana na ukubwa wa kiwanja ulilipa kwa 'control number' ama kwa mfumo upi?
 
Hati ya nyumba? Acha kusumbua JF nenda Halmashauri kaeleweshwe badala ya kutupigisha ramli humu
 
Mkuu, hiyo gharama uliyotozwa kulingana na ukubwa wa kiwanja ulilipa kwa 'control number' ama kwa mfumo upi?
Walicalculate wao wakanipa control namba kwenda kulipa ilikuwa kama 120,000 square mita 730
 
Back
Top Bottom