Wanatakiwa kuweka tangazo kuwa unywaji wa soda kupita kiasi ni hatari kwa Afya yako

Ndo hivyo ndugu yangu,maendeleo yanapokuja yanakuja na athari zake,hatuwezi kuepuka technology.

Nilishangaa sana wakati ule Kenya wamezuia mahindi yetu yasiingie kwao kwa kuwa si mazuri kwa afya zao,lakini kwa upande mwingine karibu kampuni zote zinazoiza mbegu za mahindi hapa tz zimetokea Kenya.
 
Wamesikia teyari. Ivi vinywaji ni hatariiii
 
Hivi hawa wanaokunywa energy drinks hata 6 kwa siku nao wawe kundi gani!!
 
unawaza ngono tu eti?
sifa mojawapo ya kiumbe hai ni kujamiana, yaani kufanya ngono kwa jamii zote za wadudu, ndege na wanyama akiwemo binadamu ili kuendeleza uzazi. Sasa kama ufanisi wa kufanya ngono unapungua maana yake uzazi unaisha, kwa nini uzazi uishe kizembe wakati muda wake haujafika? Afya ya uzazi nayo ni muhimu kulindwa isiathirike.
 
Kiuhalisia soda ni hatari hata kuliko bia na sigara. Japo hivyo vingine navyo vina madhara makubwa. Niliyoyaona baadhi ya nchi nilizowahi kutembelea nje ya Africa, kushindwa kuweka onyo kwa bidhaa hatari kuzitumia ni kosa kubwa sana. Ni nchi zetu tu masikini tunauana kwa ulafi wa fedha. Mimi nina miaka mitano sasa sijanunua soda.
 
Insulin inaachiliwa na figo tena🙄
 
Wanasema mirinda nyeusi INA vijiko 9 vya sukari, sawa na 10g kwa kila 100ml za soda , fanta na Pepsi vijiko vitano vitano, hatuponi wallahi
 
Nakubaliana na wewe. Mkakati wangu wa kupunguza mwili na kuwa fit, umefanikiwa sana baada ya kuachana na sukari kabisa na mavinywaji ya kijinga jinga kama hizo soda na juice.

Sukari ni mbaya sana. Wanakijiji wa Okhghimi huko Okinawa japan, huishi miaka mingi sana, siri ni kuwa wako active sana, na hawali sukari kabisa, sana sana wanaitoa kwenye miwa, sio hii industrial sugar.
 
...kupita kiasi...
Bado kuna mtu hafahamu kuwa kuna tatizo katika kila "kupita kiasi"?!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…