Mwanga Lutila
JF-Expert Member
- Nov 10, 2016
- 4,208
- 14,143
Wakuu wasalaam..
Niko vijiji vya ndani ndani huku Ndiwili wilaya ya kilolo nimekuja kwa shughuli zangu..baridi ni kali .
Katika matembezi yangu nikakutana na watoto wadogo chini ya miaka 10 wengi ni 7 na 8 wakifanya vibarua vya kusomba mbao yaani kuzitoa msituni na kuzipeleka lilipo gari ili tu wapate pesa ya madaftari na kwendea mnadani kununua nguo hasa "majaketi" ndo wanazungumzia sana.
Katika kuongea nao kuhusu wazazi, baadhi yao wanakaa na bibi na wengine na mama pia ila baba zao wanasikiaga wapo mjini.
Roho imeniuma sana , watoto wadogo lakini wamejivika majukumu ya kikubwa.
Mtoto kama huyu hawezi kuwa na huruma wala upendo kwa mtu baadae maana hajui neno huruma wala upendo.
Watoto hawa wanawakilisha maelfu ya watoto wengi walioko vijijini.
Wanaume kama umeacha mtoto huko vijijini eti yuko na mama yake sijui bibi yake fanya juu chini kamchukue uishi nae mwenyewe..
Kuna sehemu za nchi ukipita unaweza sema ndani ya Tanzania kuna nchi nyingine.
Niko vijiji vya ndani ndani huku Ndiwili wilaya ya kilolo nimekuja kwa shughuli zangu..baridi ni kali .
Katika matembezi yangu nikakutana na watoto wadogo chini ya miaka 10 wengi ni 7 na 8 wakifanya vibarua vya kusomba mbao yaani kuzitoa msituni na kuzipeleka lilipo gari ili tu wapate pesa ya madaftari na kwendea mnadani kununua nguo hasa "majaketi" ndo wanazungumzia sana.
Katika kuongea nao kuhusu wazazi, baadhi yao wanakaa na bibi na wengine na mama pia ila baba zao wanasikiaga wapo mjini.
Roho imeniuma sana , watoto wadogo lakini wamejivika majukumu ya kikubwa.
Mtoto kama huyu hawezi kuwa na huruma wala upendo kwa mtu baadae maana hajui neno huruma wala upendo.
Watoto hawa wanawakilisha maelfu ya watoto wengi walioko vijijini.
Wanaume kama umeacha mtoto huko vijijini eti yuko na mama yake sijui bibi yake fanya juu chini kamchukue uishi nae mwenyewe..
Kuna sehemu za nchi ukipita unaweza sema ndani ya Tanzania kuna nchi nyingine.