Wanaume kama umetelekeza mtoto kijijini nenda kamchukue

Wanaume ni watu wenye upendo sana ukiona mtoto anateseka basi ujue hata baba yake anateseka mara mbili hakuna Mwanaume anayekuwa financial stable akaacha damu yake.

Hao watoto utakuta baba zao wengi ni walevi, drug addict walio kata tamaa kujitunza wenyewe ni big issue sembuse kumchukua mtoto kijijini kuja naye mjini si ndio future ya mtoto inakuwa falling kabisa
 
Asante kalesa
 
Kwani hakuna familia zinazoanzishwa vijijini? Mpaka kusema watoto wengi waliopo huko wazazi wao wapo mijini
Mkuu zipo familia zinaanzishwa lakini changamoto za ngono zembe ni kubwa sana. Mabinti wadogo wanapata mimba alafu wazazi ndio hao boda boda au wanafunzi wenzao, wengine ni wale waliomaliza kidato cha nne au darasa la saba wanaokimbilia mijini,huko wanapata ujauzito na wanaume wasioeleweka au tabia zao za kuwa na msururu wa wanaume kwa lengo la kupata fedha au ndoa) hufanya mimba zao kukataliwa. Hao nao baada ya kujifungua hupeleka watoto vijijini.

Kingine ni Mila ya baadhi ya makabila hasa Kanda ya ziwa, Binti analazimika kuzaa Ili aache mtoto nyumbani, kwa kiLe kinachoitwa kuongeza ukoo.

Nimefanya project fulani vijijini na hilo nina ushuhuda nalo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…