Wanaume mtaendelea kulogwa msipoacha haya ....

Wanaume mtaendelea kulogwa msipoacha haya ....

"Mimi nimevuka bahari bila kichwa kulowa maji, silogeki".

Jana alikuja jamaa hapa JF ana trend na thread anatafuta demu Mzungu awe na urafiki kwa nia ya kuoa. Tena wa kukaa naye Tanzania si kutafuta safari ya ughaibuni.

Nikaona fadhaa sana. Kwanini mtu anatafuta Mzungu kwa umahsusi hivi? Sina tatizo na mapenzi ya watu wa rangi tofauti yakitokea tu kama mapenzi, lakini huyu anawinda Mzungu akanifanya nijiulize sana.

Kwetu hakuna mabinti wa kuvutia?

Kimetokea nini?

Nimesikiliza hiyo audio.

Kama mtu anakutana na wanawake wa aina hiyo, akiamua kutafuta Mzungu aliyetuliza kichwa wala siwezi kumshangaa.
 
Mwamba ngoma huvutia kwake, na msipobadilika mtapiga kelele sana na kutumika sana wakati wanaowatumia mwisho wa cku wanawaacha na kutafuta wake wenye hekima na busara wakawaowa na wanaishi. Hakuna cha mume wala mke, hiyo dhambi ipo kote. Mwanamke mmoja kwa upumbavu wake kaachwa basii kila kona analaumu wanaume hadi wadada ambao hawajaolewa nao wamekataa ndoa kisa muasi mmoja. Nwaname mpumba pia hvyo hvyo kaachwa anasema wanawake wote hovyo hadi vijana wamekataa kuoa. Tena huo uchawi mnaokimbilia ndiyo ishara tosha kuwa hamna hekima wala busara hata kidogo.
Wakaenda matarishi wenye nyaraka za mfalme na wakuu wake, kati ya Israeli yote na Yuda, na kwa amri ya mfalme, kusema, Enyi wana wa Israeli, mrudieni BWANA, Mungu wa Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, apate kuwarudia waliosalia wenu waliookoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru.
 
Aisee
We ngoja umpate wa kukufanya ucheke kama chizi unacheka na ukuta ndio ujue ushapigwaaa
Hahahahah ila kuna makabila fulani ukioa lzm limbwata ulishwe tuu,kwa upande wangu sio kwamba najisifia ila siku nagundua kitu kama hicho Mungu ndio anajua aiseee...
 
Wanaume mnalipia vbaya kuweni macho jamani

Kama kuna mwanaume aliemwumiza vbaya mwanamke huku duniani na mwanamke akaamua kuambia jamii nzima jinsi alivyoumizwa, huyo mwanamke Mungu ambariki lakini sio asee mpaka naona huruma

Ndio wanaume walivuruga sana mama zetu, dada zetu huko nyuma, lakini Dhambi ya kumvuruga mwanamke ni mbayaaa, bora umvuruge mnyama kuliko mwanamke

Wazungu wanasema one woman's trash is another woman's tressure! Lakini trash haijawahi kuwa cleaned ndio hio inayoleta matatizo kwa wanaume hivi leo wanakuja na vilio wanawake wa kuoa amnaaa, wanawake wanapenda helaaaa, wanawake hawafugiki wanapenda mteremkoo. wanawake hawajatuliaaa hii yote ni kwasababu mjinga mmoja wa kiume alimwumiza mwanamke m1 tu sumu ikasambaa mpaka kwa vizazi vya 5 ndio akina mimi na wewe

Nchi za ulaya ya Europe akina Norway, Finland, wanaume walianzaga michezo ya kuwaumiza wanawake wanawake wakaambiana buana, ikafika mahali wanawake wakagoma kuzaa, miaka ikasogea serikali ikaona nchi yao haina wazawa, wakafanya Urafiki wakaambiwa wanawake wamegoma kwasababu hii na hii na wanaume ndio chanzo kama hawatabadilika hatutazaa

Serikali ikaweka Beijing pale ikawasikiliza, sasa hivi huwezi cheza na mwanamke wa kizungu, hiyo punishment yake utajutaa kuzaliwa mwanaumee

Me nawaombeni wanaume wa kiTanzania mliobaki mtubu Dhambi za baba zenu kwa Mungu wa Mbinguni na mbadilike otherwise mtakuwa mnalia tuuu hamna wa kuoa hamna wa kuoa mpaka Yesu anarudi nyie kazi zenu ni kujipiga bao tu mwisho wa siku unakuwa mngese kwisha habari yako

No man is an island unafikia tu point unataka kuoa lakini kwasababu ulivuruga unakosa kuoa mke mzuri unaishia kupata design ya uliowavuruga mwanzo afu unalalamika, Jeesooos!

Sasa wanawake skuhizi wamekuja na itikadi mpyaaa, baada ya kuona wanaume wanaendekeza michepukooo (side chic, side piece), ndani ya ndoa kunanuna nje ya ndoa kunacheka

Ni vile tu wanaume hawajui wanawake wakishaambizana vitu vya hushikilia milele

Isikilize hii video ujionee muujiza wa itikadi mpya wa wanawake juu ya wanaume yeleuuuwi



Msicheze na wanawake, ni maji ya moto hao ohooo

Ndo mawazo ya wasiopenda kazi.
Chapeni kazi.
Asilimia kubwa ya michepuko ndio ninyi nyie
Mnaojidhalilisha na kutembea na waganga ili mambo yenu yanyooke
Huwezi kushindana na mwanaume other wise you will be heading to hell.
 
Bro utaishia kuwa mngese
No man is an island!
Acha itikadi OA!
Unaonekana una itikadi za kaskazini. Ninyi mmewamaliza wa kwenu. Sasa umeanzisha dhehebu lako la mafundisho ya ulaya???

Na bado usidhani utamroga mtu wewe ubaki salama maana Mungu hugawa adhabu sawasawa na upumbavu ulioufanya na ndivyo ilivyokuwa kwa Adam na Eve

Badala ya kuombea vizazi vyenu vipone na mjisahihishe mlipo kosea. Nyinyi mnaleta upumbavu

Ama kweli mwanamke mpumbavu hu.......(bible)
 
Unaonekana una itikadi za kaskazini. Ninyi mmewamaliza wa kwenu. Sasa umeanzisha dhehebu lako la mafundisho ya ulaya???

Na bado usidhani utamroga mtu wewe ubaki salama maana Mungu hugawa adhabu sawasawa na upumbavu ulioufanya na ndivyo ilivyokuwa kwa Adam na Eve

Badala ya kuombea vizazi vyenu vipone na mjisahihishe mlipo kosea. Nyinyi mnaleta upumbavu

Ama kweli mwanamke mpumbavu huvunja nyumba yake kwa mikono miwili.......(bible)

Msisahau kuwa ratio ya wanaume na wanawake ni ndogo inafikia nchi nyingine zinapitisha sheria kila m'naume aoe m'namke zaidi ya mmoja

Tatizo lenu ni wa binafsi na hanpendani na roho mbaya hasa nyie wanawake wa akina yeleuwiii. Mna matatizo sana
 
Back
Top Bottom