Wanaume wa hii mikoa sita (6) acheni kukaa vijiweni bila kufanya kazi.

Wanaume wa hii mikoa sita (6) acheni kukaa vijiweni bila kufanya kazi.

RIGHT MARKER

Senior Member
Joined
Apr 30, 2018
Posts
129
Reaction score
473
💼 MHADHARA WA 6.
Habari ya leo wanaJF...

Kwenye mhadhara huu naomba kuzungumzia tabia ya wanaume wengi (wazawa) wa mikoa ya DAR ES SALAAM, LINDI, MTWARA, TANGA, PWANI na hata kule ZANZIBAR ambao kutwa wanashinda vijiweni bila kufanya kazi.

Vijana wengi wa hiyo mikoa wanashinda vijiweni siku nzima (kila siku) bila kufanya kazi wala kutafuta kazi huku baadhi wakiwa wamevaa mataulo na misuli kiunoni mchana kweupe. Baadhi ya vijiwe wamevipa majina fulani fulani vikiambatana na neno CAMP; kwa mfano unaweza kukuta hapo kijiweni kumeandikwa WATOTO WA MJINI CAMP, utawakuta wamelala, wengine wanacheza bao huku wanapulizwa na upepo wa miti au bahari.

Kilichopo hapo ni uvivu, kwasababu vijana utakaowakuta hapo huwa wanaketi vijiweni siku nzima, na muda wa chakula ukifika wanakwenda kula chakula kwa wazazi au kwa ndugu zao kisha wanarudi vijiweni kuendelea kupiga stori. Stori zinazozungumzwa hapo ni za siasa, uchawi, mapenzi, na lawama mbalimbali.

Hakika mikoa hiyo ina idadi kubwa sana ya vijana wavivu (wasiopenda kusoma, kufanya kazi wala kutafuta kazi). Unakuta kijana wa miaka isiyopungua 30 anaishi maisha ya "KULA KULALA" kwa mume wa dada (shemeji), na akiamka asubuhi anasubiri breakfast kutoka kwa wazazi au shemeji; baada ya hapo anakwenda kijiweni kupiga stori. Asset pekee anayomiliki ni smartphone ambayo amepewa na dada yake aliyenunuliwa simu mpya.

Tabia hiyo ya kushinda vijiweni bila kufanya kazi ni tofauti na mikoa mingine. Mikoa mingine ukikuta vijana wameketi vijiweni ni bodaboda wanasubiri abiria, na ukihesabu idadi ya vijana waliopo kijiweni ni sawa na idadi ya pikipiki zilizoegeshwa pembeni. Mikoa mingine hukuti vijana wameketi kijiweni bila channels za hela, na ukikuta vijana wapo kijiweni wana maduka yao pembeni.

BY: RIGHT MARKER-TZ
Mbezi Louis, Dar es Salaam.
 
Kuna Dini Flani ni kama jambo hili ni muhimu sana kwao kwa wanaumeee

Kutwa kucheza Bao weeeew saa sabaa King'oroaa wanaacha wakitoka wanaendaa kula nyumbani alfu wanarudi

Saa kumi King'oraa baadaya ya hapo nyumbani

Sijasema mtuu
 
Rombo wanafanya kazi ya kunywa pombe kutwa mzima mpaka hawawezi kuongilia wake zao!

Watu wa Dodoma wamejaa Pwani wanaomba omba 24/7

Wamasai wamekimbia kwao na mashuka yao bila chupi wamejaa Pwani!

Kuna mabwenga kutoka Inshomile wako Pwani wanahudumia wenyeji 24/7

Na wewe kenge bila shaka unaandika uharo ukiwa Pwani, umekimbia kwenu Uporoto huko!

Kila jamio inashughuli zake za kiuchumi na lifestyle yao!
Pwani wengi wao ni wavuvi na uvuvi unafanyika usiku!

Usilazimishe Kila mtu anuke jasho ili tu umuone mchapa kazi!
Umeshawahi kusikia baa la njaa Pwani?
 
Tabia hiyo ya kushinda vijiweni bila kufanya kazi ni tofauti na mikoa mingine. mikoa mingine ndo kama ipi?
 
Me huwa nayashangaa hayo majitu ya hiyo mikoa,eti muda wa kazi kabisa yenyewe yako misikitini yamelala kwenye ile mikeka ya kuswalia.
 
kwanini hurudi nyumbani unazurura zurura ukiwa hiyo mikoa ya pwani?
 
Cha ajabu ni kwamba wanaume wa mikoa mingine wanatoka huko makwao kuja kutafuta maisha kwenye hiyo mikoa!!
 
waache tu washinde na misuli yao,huenda wana tumbo la kuhara ndio maana hawavai nguo.
 
Kuna Dini Flani ni kama jambo hili ni muhimu sana kwao kwa wanaumeee

Kutwa kucheza Bao weeeew saa sabaa King'oroaa wanaacha wakitoka wanaendaa kula nyumbani alfu wanarudi

Saa kumi King'oraa baadaya ya hapo nyumbani

Sijasema mtuu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Me huwa nayashangaa hayo majitu ya hiyo mikoa,eti muda wa kazi kabisa yenyewe yako misikitini yamelala kwenye ile mikeka ya kuswalia.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
💼 MHADHARA WA 6.
Habari ya leo wanaJF...

Kwenye mhadhara huu naomba kuzungumzia tabia ya wanaume wengi (wazawa) wa mikoa ya DAR ES SALAAM, LINDI, MTWARA, TANGA, PWANI na hata kule ZANZIBAR ambao kutwa wanashinda vijiweni bila kufanya kazi.

Vijana wengi wa hiyo mikoa wanashinda vijiweni siku nzima (kila siku) bila kufanya kazi wala kutafuta kazi huku baadhi wakiwa wamevaa mataulo na misuli kiunoni mchana kweupe. Baadhi ya vijiwe wamevipa majina fulani fulani vikiambatana na neno CAMP; kwa mfano unaweza kukuta hapo kijiweni kumeandikwa WATOTO WA MJINI CAMP, utawakuta wamelala, wengine wanacheza bao huku wanapulizwa na upepo wa miti au bahari.

Kilichopo hapo ni uvivu, kwasababu vijana utakaowakuta hapo huwa wanaketi vijiweni siku nzima, na muda wa chakula ukifika wanakwenda kula chakula kwa wazazi au kwa ndugu zao kisha wanarudi vijiweni kuendelea kupiga stori. Stori zinazozungumzwa hapo ni za siasa, uchawi, mapenzi, na lawama mbalimbali.

Hakika mikoa hiyo ina idadi kubwa sana ya vijana wavivu (wasiopenda kusoma, kufanya kazi wala kutafuta kazi). Unakuta kijana wa miaka isiyopungua 30 anaishi maisha ya "KULA KULALA" kwa mume wa dada (shemeji), na akiamka asubuhi anasubiri breakfast kutoka kwa wazazi au shemeji; baada ya hapo anakwenda kijiweni kupiga stori. Asset pekee anayomiliki ni smartphone ambayo amepewa na dada yake aliyenunuliwa simu mpya.

Tabia hiyo ya kushinda vijiweni bila kufanya kazi ni tofauti na mikoa mingine. Mikoa mingine ukikuta vijana wameketi vijiweni ni bodaboda wanasubiri abiria, na ukihesabu idadi ya vijana waliopo kijiweni ni sawa na idadi ya pikipiki zilizoegeshwa pembeni. Mikoa mingine hukuti vijana wameketi kijiweni bila channels za hela, na ukikuta vijana wapo kijiweni wana maduka yao pembeni.

BY: RIGHT MARKER-TZ
Mbezi Louis, Dar es Salaam.
Ila sio walalamishi kama mikoa ya kaskazini na wamelizika na maisha yao.
 
Vijana wengi wa hiyo mikoa wanashinda vijiweni siku nzima
Ongeza mikoa list ni ndefu sana kuna mikoa utawakuta kwenye vitu viwili km sio vitatu Pool table, Draft au Bao kuna mikoa nimepita nimekuta hizo sehemu wanakaa muda mwingi sana ila usichojua ni kwamba hapo kwenye hio michezo yote wanacheza kamari Pool table wanacheza kamari, Draft wanacheza kamari na hio Bao ni kamari mshindi anarudi nyumbani na kibunda
 
Back
Top Bottom