Wanaume wanaovaa cheni na hereni wanataka nini?

Wanaume wanaovaa cheni na hereni wanataka nini?

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Siku hizi ni kawaida kumkuta mwanaume amevaa cheni shingoni au hereni masikioni. Tena utamkuta mwanaume mwenye akili zilizotimia (achilia mbali mateja) amevaa hereni na cheni kubwa huku akijiona mjanja! Huu ni ujanja au ni dalili za kukengeuka?

Tangu dunia hii ilipoumbwa, inajulikana kwamba urembo ni kwa ajili ya wanawake. Mwanaume hata ukiwa rafu ni pouwa tu--hakuna mtu atakayekushangaa, tofauti na ilivyo kwa wanawake. Mwanamke ni kiumbe anayejisikia kuonekana nadhifu na mrembo nyakati zote. Hivyo hupenda kuvaa vifaa vya urembo kama vile hereni, mikufu, pete, vidani, bangili, nk. Sasa wale wanaume wanaovaa vifaa hivi vya KIKE tuwaweke fungu gani? Si wavae na sketi kabisa ili tujue moja?

Kwa kweli wanaume wenzangu wanaovaa pete, hereni na mikufu wananiudhi sana. Mimi siwezi hata kuvaa saa kwa kuwa inanifanya nijihisi nimevaa bangili! Sasa iweje wanaume na ndevu zao watamani kuvaa urembo wa kike?

Naomba tujadiliane BILA JAZBA hadi jibu lipatikane. Samahani sana, najua hata humu JF wavaa hereni wamo.
 
Niwe mkweli saa yangu mkononi saa nzuri ya 200k au 300k , cheni yangu ya silver nyembamba isiyokua na kidani na visuruali vyangu kadet na vishati vyangu vya kunienea na sio oversize na ichwani nywele zangu fupi na kwenye kidevu hakuna ndevu huku kucha za mikono zikiwa fupi na nina nukia utuli ndo hua navaa halafu leo uhamasishe niache kuvaa cheni?? Whaaaat shit is this
 
Au hua natupia jinzi yangu nzuri tishet V colour shape na cheni na simpo chin na saa yangu mkononi huku nikiwa nadhifu wewe halafu ulete zako hapa kuendeleza uchafu wako
 
Cheni ni kitu kizuri sana ilmradi zisiwe zile za kuudhi


Samahani, nimetupa jiwe gizani kama limekupata vumilia tu. Mwanaume hutakiwi kutishika kirahisi--gangamala.

Jamani, mnaona wadau wameanza kuibuka mmoja mmoja?
 
Loading.......

Scanning............

........................................78%
 
Mleta mada umejawa wivu mpka shetan nae anakuogopa khaah


Sent from my iPhone using JamiiForums.🔩🔨
 
Cheni inamfanya mwanaume aonekane sexy....

Na mwanamke aonekaneje?

Mimi ninachojua ni kwamba u-sexy ni kwa ajili ya wanawake tu--mwanaume anasifiwa kwa kazi na pesa sio kwa kuonekana SEXY! Kama kuna aliye handsome, hiyo inatosha. Mikufu, vidani na bangili kwa wanaume vya nini?
 
Samahani, nimetupa jiwe gizani kama limekupata vumilia tu. Mwanaume hutakiwi kutishika kirahisi--gangamala.

Jamani, mnaona wadau wameanza kuibuka mmoja mmoja?

Ww n shoga kweli


Sent from my iPhone using JamiiForums.🔩🔨
 
Mbona wamasai mwanaume ndo naeongoza kwa kuweka urembo mwln mwake? Tuwaitaje sasa,,,, acha wivu mkuu dunia inasonga we endelea kukaa


Sent from my iPhone using JamiiForums.🔩🔨
 
Back
Top Bottom