Wanaume Watakiwa Kukaa Wakiwa Wanakojoa!!

Wanaume Watakiwa Kukaa Wakiwa Wanakojoa!!

Elisha Ray

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2012
Posts
323
Reaction score
94
Wakuu, hii ni ya Taiwan kwamba wanataka kupitisha sheria kuwa na wanaume nao wawe wanakaa wakati wanakojoa. Kama tujuavyo wanaume wakiwa wanakojoa huwa kuna matone ya mkojo ambayo hurukia kwenye kingo za choo mpaka pale pa kukalia na most of the time hawafuti choo maana hata ukiflash bado yanakuwepo. Sasa yale matone baada ya muda hutengeneza vijidudu ambavyo vinasababisha U.T.I na magonjwa mengine ya namna hiyo kwa wanawake kwani kutokana na maumbile yao huwa rahisi kwao kushambuliwa kama nao hawasafishi/hawafuti choo kabla ya kutumia (katika public toilets au nyumba zenye wakaka wasiosafisha vyoo baada ya kutumia). Sasa na hii sitashangaa ikija bongo na mie siko tayari kukaa ili nikojoe wakati naweza kukamua nimesimama... Wajameni kwa wale wasio na tabia ya kufuta choo baada ya kukojoa badilikeni kuweni wasafi basi ili hii kadhia isije kwetu eeenh???? Tuwapende mama/dada/wake zetu basi na kwenye afya zao pia!!!! Ni rahisi tu, ukikojoa futa zile kingo then flash... Hii mambo ya kuambiwa mke/mama/dada/mtoto ana UTI haipendezi halafu kumbe wewe mume/baba/kaka ndo chanzo!!!!
 
kwa waislam popote walipo dunian hii n common.unajua hii dini bana hua haiachi kitu.baadae wanadamu na akili zao mgando ndio wanakuja kufaham.hahahaha...
 
i thought kila mahali duniani wanaume wana toilets zao na wanawake zao,kumbe kuna sehemu bado kuna sharing,haya wakaka mjirekebishe je wataweka camera chooni kuhakikisha hili?
 
Aisee itasaidia wataacha kukojoa ovyo kama ilivyo tabia hii kwa wanaume wengi
 
Nashukuru kwa kuzaliwa Muislam kwani dini yangu ilishanifundisha kitambo kua kusimama wakati wa kukojoa si jambo jema.
 
james cameron ana mkono wake katika serikani ya taiwan????
 
Mi huwa nawaonea huruma tu wanawake wanaotumia vile vyoo vyetu vya uma. Hasa vyenye sink refu kwenda juu, maana hayo makojo yanayomwagika pale juu. Mi huwa sinyi kwenye vile vyoo.
 
Kwa kweli hii tabia mbaya ya kuacha mikojo juu imejaa maofisini!!
Tabia inakera sana,unaingia toilet unakuta mkaka aliyetoka ameacha ramani!majority sio wapenzi wa kunywa maji mara kwa mara,hivyo unakuta ramani za njano kwenye choo cha kukaa!!kwa style hii wanawake wataacha kupata U.T.I?
 
  • Thanks
Reactions: Aza
i thought kila mahali duniani wanaume wana toilets zao na wanawake zao,kumbe kuna sehemu bado kuna sharing,haya wakaka mjirekebishe je wataweka camera chooni kuhakikisha hili?

Mkuu hata kama choo ni cha wanaume peke yao,wao hawasikii kinyaa kila saa kutazama mikojo ya wenzao?
Inakuwaje wakati wa kukata gogo?Ninavyoelewa itamlazimu kukaa na sio kusimama!!!
Usafi ni kitu cha kistaarabu sana,kila mtu anatakiwa kuelewa!!
 
Mbona hii haina shda,kukaa tu!c ndo kuchuchumaa bwana,hyo cmpo.Najifanya nakata gogo kwisha habari.
Au?
 
Nashukuru kwa kuzaliwa Muislam kwani dini yangu ilishanifundisha kitambo kua kusimama wakati wa kukojoa si jambo jema.

Al Islaam nadhif ! upo ushahidi wa kisayansi kuwa ukikojoa umesimama unaweza kuanguka na ukazimia !
 
nabii Muhammmad(S.A.W) alishatangaza tokea karne ya 7,
si hilo tu lakiafya na mengine kibao
 
kwa waislam popote walipo dunian hii n common.unajua hii dini bana hua haiachi kitu.baadae wanadamu na akili zao mgando ndio wanakuja kufaham.hahahaha...

itabidii serikali dhaifu wamtumie kova ili wawaogopeshe watu baada ya sheria hiyo kutungwa TANZANIA ; nna fikiri wakitumia tuu mahakama ya kisutu haitatosha kwakuwa watu watatoa rushwa kama karanga.
 
Suala la usafi halina dini na wala sidhani kama ni relevant hapa. Ishu ni mtu binafsi kuwa msafi maana wapo watu kibao wanakojoa hovyo wa 'dini' zote.. Wewe kama ni msafi ni msafi tu na kama ni msafi nusu nusu ndo hivo tena. Inaudhi sana pale unapomuona mtu very smart katoka chooni na wewe unapoingia unakuta mikojo yake kila kona wakati choo kilikuwa kisafi na sio kama alikuwa amelewa!!! Sio kama najifagilia ila mimi hufuta nikimaliza (nilikuwa sifuti enzi hizoo) na hii ni baada ya wife kunichimba mkwara kwamba akipata UTI patakuwa hapakaliki so toka siku hiyo nafuta popote pale niendapo na inapendeza sana. USAFI MUHIMU popote ulipo...
 
kwa waislam popote walipo dunian hii n common.unajua hii dini bana hua haiachi kitu.baadae wanadamu na akili zao mgando ndio wanakuja kufaham.hahahaha...

kwamba?....
 
itabidii serikali dhaifu wamtumie kova ili wawaogopeshe watu baada ya sheria hiyo kutungwa TANZANIA ; nna fikiri wakitumia tuu mahakama ya kisutu haitatosha kwakuwa watu watatoa rushwa kama karanga.

mh!
ili nalo linaihusu sisiem eeh?
 
teh teh teh....kwanini mtu analazimishwa kufanya asichotaka?
 
Back
Top Bottom