Wanawake 50% kwa 50% tumedandia trneni kwa mbele, tujipange upya..

WanawakeLive

Member
Joined
Nov 14, 2011
Posts
6
Reaction score
1
wanawake tumekuwa ktk mstari wa mbele kudai HAKI na FURSA SAWA kwa wote (50% kwa 50%) mbona majukumu ya familia tunayakwepa??? tena na majina kibao ya kuwadhalilisha wenzi wetu, (sharobaro, mwanaume suruali, nk) tutaongozaje jamii na taifa kama hatuwezi kuongoza familia zetu?

Namaanisha matumizi ya nyumbani huku tunajitetea mwanamke tumeubwa kulelewa!!

Huku tunasema mfumo dume unatukandamiza tunataka viti maalum, na nafasi kibao za uongozi kwenye jamii....nyumbani kuwajibika hatutaki, tunamwachia mume majukumu yote! bora mwanamke ambae hana hela, naongea na sisi wenye vijisenti...TUTAFIKA?

MIAKA 50 YA UHURU??
 
Mi nawachokoza tu wadada wa JF eti mnasubiri ziingie mzipangie bajeti? eti daughter enhe?
 
Hivi kipindi chenu tayari kimeshaanza kwenda hewani shemeji?
 
Ngoja waje be patient please utawajua wao ni akina nani
 
huyu jamaa amegusa penyewe nijuavyo vitu vinavyo wagusa moja kwa moja hawavichangii,ila kusema ukweli sijui tuendako maana akinamama akikupatia
 

Kufika mtafika ila chamoto mtakiona!!!!:eyebrows:
 
Its too headache tena hawa wanamaliza shule na kupata kazi haraka haraka, anasahau kama kuna maisha bila hela!! Akifikisha 32 hadi 35 anaanza kulia lia oooh nataka kuolewa nipate familia hapo walishachezea mashine mpaka basi huku akiwa busy kutafuta hela na kuweka mambo ya 50% by 50%.
 
Mwanamme akitaka nizisake pesa sawa na yeye, analazimika kusaidia na ulezi pia.

hapo umenena sio anadai usawa kwenye kuzisaka tu mambo mengine anaachiwa mama,na time ya kuzihonga huko kwa malaya mbona huwa hawaombi usawa?
 
acha wewe, siku hizi wanawake wanalea wanaume, ndo wanalipa ada za watoto, wanahakikisha msosi upo mezani! Wanaume wao wanaweka heshima bar na kutunza small house

anyway mgawanyo wa majukumu ndani ya nyumba inategemea na makubaliano yenu, wanawake wanashiriki kwa njia mbalimbali siku hizi ingawa inaweza isifike 50% kama unavyosema
 
Mwanamke pambo babuwee, ulisikia wapi kuna mwanamme akafanikiwa bila mwanamke? Unanchekesha!

"man has enough blood only for one head, when its used in one the other fails".
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…