Wanawake jiinueni kiuchumi, ndio uhuru wenu

Wanawake jiinueni kiuchumi, ndio uhuru wenu

Kidagaa kimemwozea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
3,680
Reaction score
6,554
Kama hauna au hauko vizuri kiuchumi utumwa unakunyemelea katika muktadha wowote ule. Ndiposa nakuja na ushauri huu kwa jinsi ya ke kuwa wajitahidi kujiimarisha kiuchumi na kutokuwa tegemezi katika jinsi ya Me ili waondokane na utumwa katika mahusiano na katika Ndoa.

Yapo mawazo mgando kuwa wanawake wenye alimu au uchumi mzuri hawaolewi! Hayo ni mawazo ya kikale yasiyo na nafasi katika jamii ya wanamabadiliko.

Mwanamke nivyema ukajitengenezea Nafasi ya kujimudu mwenyewe kiuchumi katika kipindi Cha maisha yako ili usiwe tegemezi au mzigo kwa jamii na kukwepa kutumikishwa. Na Kufa kwa Uhuru wako.

Vilevile itakupa nafasi kushiriki kikamilifu katika harakati za kuhudumia familia na mwenza wako, kushiriki katika kuinua uchumi wa nchi n.k

Karibu kwa maoni
 
Hapa ndipo nyie washauri butu mnapofeli. Mnahisi mnatoa ushauri positive but actually mnazungumza pumba.

Ipo hivi hata mwanaume akikaa na mwanamke mwenye pesa ambaye atamtegemea kwa kila kitu mambo yatakuwa ni yale yale yaani mwanaume kupitia wakati mgumu.

Ushauri sahihi ni kuwaambia wanawake watafute kujifunza maarifa ya kwanza kushimu vipato vya wanaume zao, kutunza pesa za wanaume zao na kutokuwa na mahitaji mengi ambayo wanategemea mwanaume atoe pesa kuyalipia kwa sababu tu yeye ni mwanamke hiyo si sawa.

Pili, wajifunze kupambana kujitafutia kipato ili kuchangia gharama za familia na kuwapunguzia wanaume zao mzigo. Kwasababu kama mwanamke anatengeneza laki tatu na mwanaume laki tatu then hapo ndani kutakuwa na laki sita ambayo itasaidia sana kupunguza gharama za maisha yao na kuwapunguzia kazi ngumu ya kutafuta pesa.

Kwahiyo ninyi mnaowashauri wanawake acheni kuwatengeneza mentality kuwa wanaume wanawachukia au wanataka kuwatumikisha au kuwageuza watumwa si kweli. Wanaume kama wao pia tunachoka kutafuta pesa halafu unarudi nyumbani mtu anakupokea na bills au gharama ambazo hata hujui katoka nazo wapi ili mradi tu akutoe pesa, unategemea kwa mazingira hayo utampenda au kumchukulia kama kiumbe pekee?

Siku zote mtu anayemuegemea mwingine kwa kila kitu kwa sababu za kiuvivu na uonevu huwa naishia kuishi kama mtumwa.

Hawa wanawake wenyewe waulize hivi wakikaa na watoto wa ndugu zao au ndugu zao au hata house girls na wao wakawa wanalipa kila bili kwenye nyumba bila kusaidiwa huwa wanajisikiaje na wanawatreat vipi hao wanaoishi nao?

So ifike muda wanawake wajitambue kuwa kuishi na mwanaume sio mashindano na kukomeshana. Ukiona unataka mwanaume akukeletee kila kitu kisa tu unampikia ,kumfulia,na kumfanyia usafi then unauwezo mdogo sana wa kuelewa Dunia inakwendaje sasa.

Maisha ni magumu sana, sasa unapoishi na mtu halafu unataka kila anachotafuta kwa shida wewe utumie kwa kutapanya matokeo yake ndio anakuona kama mtumwa kwake. But ukiwa msaada kwa kusaidia kutafuta pesa na kuweka mezani kumpa sapoti atakuona muelewa na msaada mkubwa hautaona anakuona kama kilaza.
 
Hapa ndipo nyie washauri butu mnapofeli. Mnahisi mnatoa ushauri positive but actually mnazungumza pumba.

Ipo hivi hata mwanaume akikaa na mwanamke mwenye pesa ambaye atamtegemea kwa kila kitu mambo yatakuwa ni yale yale yaani mwanaume kupitia wakati mgumu.
Kuna pwenti za Muhimu sana unaongea lakini kidogo punguza kushambulia
 
Back
Top Bottom