miss chagga
JF-Expert Member
- Jun 7, 2013
- 57,811
- 49,053
Utauzwa mkuuLeo siku yangu imeharibika kabisa, kuna huyu mdada niko naye mwaka wa pili sasa kwenye mahusiano kumbe ni mke wa mtu bhana. na siku zote ananiambia hana mume mtoto wake aliye naye baba yake alifariki zamani.
Duuh kumbe mke wa mtu jamaa yake kanipigia simu na mikwala kibao tena ni mtu wa Tanga ananiambia ameniangalia kwa babu yake amekuta mi mwenyewe mweupe kama karatasi, haichukui hata masaa matatu kumaliza kazi na anasema nitampa faida kwa sababu ataenda kuniuza kama msukule huko kwao Tanga.
Nimeogopa kweli imebidi nimuombe msamaha tu. Jamani akina dada kama una mtu tafadhali muwe mnasema haya mambo ya kuwa misukule tena sio poa.
HahahaLeo siku yangu imeharibika kabisa, kuna huyu mdada niko naye mwaka wa pili sasa kwenye mahusiano kumbe ni mke wa mtu bhana. na siku zote ananiambia hana mume mtoto wake aliye naye baba yake alifariki zamani.
Duuh kumbe mke wa mtu jamaa yake kanipigia simu na mikwala kibao tena ni mtu wa Tanga ananiambia ameniangalia kwa babu yake amekuta mi mwenyewe mweupe kama karatasi, haichukui hata masaa matatu kumaliza kazi na anasema nitampa faida kwa sababu ataenda kuniuza kama msukule huko kwao Tanga.
Nimeogopa kweli imebidi nimuombe msamaha tu. Jamani akina dada kama una mtu tafadhali muwe mnasema haya mambo ya kuwa misukule tena sio poa.
Aseeyaani kila kitu akifanya mwanamke inakuwa tatizo, tulichofanya ni kuiga tu game yenu. nipe namba ya huyo mume mwenzio nmpe mchango wa kukuuza
Kama unatishwa na huu mkwala basi inaonekana hata siku ukiwa umeoa utatishwa na kumuacha mkeo.
Huenda ikawa kaolewa kweli au pia inaweza kuwa kapata mwingine ndio mana katafuta njia ya kukutisha ili uachane naye. Hivyo akili kichwani mwako.
Labda anatumia mbinu ya kujifanya 'mume' ukimbie
aingie....muite muonane uso kwa uso na huyo mwanamke