ndandawamalenja
JF-Expert Member
- Nov 1, 2012
- 475
- 353
Yaani kadada kamemset mzee (uncle wake wife) mpaka amekuwa kama zezeta. Picha kamili ipo hivi. Huyu ni mzee wa heshima kabisa, ni bosi wa taasisi moja nyeti hapa Dar. Siku moja hivi kama mwaka umepita huyo mzee alisepa home, akawa hajulikani alipo. Baadae tukasikia amepanga nyumba sehemu hapahapa Dar anaishi na mwanamke, (yaani kaacha nyumba yake ya kama 600 million, mke waliyeishi wote kama 20 yrs hivi, mtoto mmoja aged 20 na gari 2 ndogo). Huyo mke mpya akawa karibu na ndugu wa mwanaume mpaka alipopata uhakika kwamba mzee harudi tena nyumbani kwake. Akaanza kutimua ndugu mmoja mmoja mpaka akabaki yeye na mdingi tu. Kapewa mtaji anapiga dili za kwenda China kufuata bidhaa. Akisafiri anamwita mamake ndo aje akae na mumewe, ati hataki kumwacha na mtu mwingine. Sijui wanamlisha nini. Mdingi wa watu, yaani ukimwona kama msukule. Yupoyupo tu. Juzijuzi kulikuwa na shughuli ya kiukoo ndugu wakaamua kufanyia kwake, u know what? Eti huyo mother house kafunga vyumba vyote kaacha kimoja tu wazi kwamba wageni wote wa mumewe (wa kike na kiume) watumie hicho, ambacho mdogo wa mumewe amefikia humo! Halafu ndugu zake yeye wote wawili wa kike watumie vyumba 2 vilivyo empty. Walipolalamika, mama (huyo mdada sasa, ambae ni mdogo kwa my wife) kaja juu kishenzi, kwamba amefunga vyumba vingine kwa sababu last week aliibiwa pea ya viatu. Mdingi yupo kimya kama kamwagiwa mtaji, mkewe anadhalilisha ndugu zake wapatao 15, wawili kati yao ni wakubwa zake kisa pea ya viatu sijui vya 50,000. Mshahara wa huyu mzee ni kama 6 million per month. Utu wa mtu kwa pea ya viatu!!!!! Ndugu wakabeba mizigo yao hao wakasepa lakini wakaahidi hawatarudi tena. Mzee kampigia wife wangu simu kujaribu kureconcile (yeye ndio alianzisha kulalamika kuwa hawawezi kudhalilishwa na akataka kumchapa makofi mke wa uncle yake). Sasa mzee wa watu alichoongea hata hakieleweki, inaonekana ndugu anawapenda na dawa zimekolea. Wife hajui amsaidieje uncle wake wakati ndugu wengine wamemsusa mdingi, including mama yake mzazi!!! Tumsaidieje huyu mzee?? Wakati huohuo wadada acheni zenu bana!! Mnakuwaje na roho mbaya kuliko shetani? Ah!