Wanawake Mufindi wamshukuru Rais Samia kwa kuwapatia mitungi

Wanawake Mufindi wamshukuru Rais Samia kwa kuwapatia mitungi

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Wanawake wa Jimbo la Mufindi wamemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia mitungi ya gesi ya kupikia, itakayowasaidia kuondokana na changamoto ya matumizi ya kuni na mikaa.

Kauli hiyo waliitoa jimboni humo juzi, Mbunge Kigahe aliwapokabidhi mitungi ya gesi 500 yenye thamani ya sh. milioni 50 iliyotolewa na Rais Samia. Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Mufindi, Frida Kahaya alimshukuru Rais Samia kwa kutoa mitungi hivo ikiwa ni sehemu ya nishati safi isiyo na athari kwa afya za wananchi.

Alisema wamejipanga vyema kuhakikisha wanaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa wanachama na wananchi wa Mufindi. Kwa upande wake, Diwani wa Viti Maalumu, Kata ya Ifwagi, wilayani humo, Magreth Kaguo, alisema Rais Samia amefanya jambo kubwa wilayani humo, lililoweka alama kwa wanawake.

Aliongeza suala hilo limegusa maisha ya wanawake wa Mufindi na kuendelea kumkumbuka Rais Samia kwa kumwombea heri katika ongozi wake.

"Tunamshukuru sana Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwani amegusa maisha yetu, ameweka rekodi kubwa katika maisha yetu. Unapozungumzia maisha ya mwanamke wa kijijini kama sisi, huwezi kuacha kutaja suala la nishati ya kupikia, tunamshukuru sana na tunaendelea kumunga mkono, alisema.
 
Hiyo mitungi ametoa Rais, au ametoa yule jamaa mjanja mjanja wa Taifa Gas? Na vipi gesi ikiisha kwenye hiyo mitungi! Watawajazia kwa muda wa mwaka mzima, au ndiyo imetoka hiyo!!!
 
Hiyo mitungi ametoa Rais, au ametoa yule jamaa mjanja mjanja wa Taifa Gas? Na vipi gesi ikiisha kwenye hiyo mitungi! Watawajazia kwa muda wa mwaka mzima, au ndiyo imetoka hiyo!!!
Labda wanataka kutoka kwenye kanga, tisheti na kofia..siku hizi wanawapa mitungi ya gesi..maana huko ni kuwapa mitungi ya gesi sio kuwapa gesi, sababu gesi ikiisha watakaa na mitungi kama pambo hadi Yesu atakaporudi.
 
CCM ni cancer yaani wauwaji,gesi ya Tanzania inatakiwa iuzwe Kwa 5000 tu
 
Wanawake wa Jimbo la Mufindi wamemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia mitungi ya gesi ya kupikia, itakayowasaidia kuondokana na changamoto ya matumizi ya kuni na mikaa.

Kauli hiyo waliitoa jimboni humo juzi, Mbunge Kigahe aliwapokabidhi mitungi ya gesi 500 yenye thamani ya sh. milioni 50 iliyotolewa na Rais Samia. Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Mufindi, Frida Kahaya alimshukuru Rais Samia kwa kutoa mitungi hivo ikiwa ni sehemu ya nishati safi isiyo na athari kwa afya za wananchi.

Alisema wamejipanga vyema kuhakikisha wanaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa wanachama na wananchi wa Mufindi. Kwa upande wake, Diwani wa Viti Maalumu, Kata ya Ifwagi, wilayani humo, Magreth Kaguo, alisema Rais Samia amefanya jambo kubwa wilayani humo, lililoweka alama kwa wanawake.

Aliongeza suala hilo limegusa maisha ya wanawake wa Mufindi na kuendelea kumkumbuka Rais Samia kwa kumwombea heri katika ongozi wake.

"Tunamshukuru sana Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwani amegusa maisha yetu, ameweka rekodi kubwa katika maisha yetu. Unapozungumzia maisha ya mwanamke wa kijijini kama sisi, huwezi kuacha kutaja suala la nishati ya kupikia, tunamshukuru sana na tunaendelea kumunga mkono, alisema.
Mitungi ya gesi ya kupikia? Itatumika kwa muda gani? Miaka10, 5,au mwezi? Ikiisha nani, anagharamia kujaza?
CCM wataendelea na huu upuuzi, wa kugawa "pipi" Mpaka lini?
Hatuhitaji vi mitungi vya gesi, tuliihitaji miundombinu ya gesi majumbani, tutumie kama umeme! Ile gesi aliyoitangaza Prof muhongo! Kwenye utawala wa kikwete! Yote imeishia hewani!! Ma k ya CCM yameuza yote ulaya.
MTU mmoja, kwa uamuzi wake anatia kizazi, kizima kwenye hasara.
 
Back
Top Bottom