Wanawake, mwanaume anayekutongoza kakudharau

Jogoo akitaka kumpanda mtetea hatumi mshenga. Kama kutuma mwakilishi akutongozee ni heshima basi na kuchapiwa ni hekima!
 
Mbona Mimi mwanaume Wangu nimemzidi Na amenitongoza Na tunapendana
 
Ukitongozwa Mshukuru Mungu Umeonekana Kuna muda Utawatafuta hao unaotaka wakuogope Mama na Kiujumla Mwanaume Mkamilifu hajawahi kumuogopa mwanamke anayemtaka ukitakwa utafatwa bila shida
 
Nyie ndiyo aina ya watu wenye kujenga hofu na taharuki zisizo na msingi katika jamii bila sababu za kweli.
Mawazo kama haya huweka matabaka ya binadamu ya 1st, 2nd na 3rd classes ambayo kimsingi hayapo.

Yaani kwa mfano ukimtamani Samia unywee na ujizuie kumtamkia lililopo moyoni mwako kwa kuogopa eti utafungwa kwa kuonekana umemdharau mweshimiwa!

Heshima na thamani ya mwanamke huonekana kwa kutongozwa sana ama wanaume kuonekana wakimsorolea kwa wingi na kumgombania kama mambwa ama kuuana kabisa, hicho ndiyo kipimo cha nje cha kuonesha uzuri wa mwanamke.

Weka hapa mbinu za kumtongoza Rais ama mawaziri na wanawake wengine wakwasi na siyo kujenga hofu ya kuwatokea bhana.

Unapomtongoza mwanamke lazima kuna msukumo wa ndani wa kuanzisha naye mahusiano ya kijamii unaokuwa umekupata na siyo kumdharau.
 
Kuna uzi niliona huku Dada analalamika kwamba anatongozwa na watu waliochoka tu akatolea mfano anatongozwa na bodaboda ,wazoa taka etc.

Kiukweli mwanamke ukijiweka cheap utatongozwa hadi na wanywa wanzuki au chimpumu maana wanaona ni level zao.
 
Inawezekana ni kweli mimi wanawake wanaonisumbua ni hawa kina mwajuma kanda mbili ila wale mademu wakali wenye bussness zao ukitest tu.
 
Hahaha au sio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…