Wanawake na mabinti 16 Mbaroni kwa Kuhamasisha Ukahaba wapo wanaocheza "Kibao Kata"

Wanawake na mabinti 16 Mbaroni kwa Kuhamasisha Ukahaba wapo wanaocheza "Kibao Kata"

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imewakamata jumla ya Wanawake na mabinti 16 wanaojihusisha na mtandao wa matendo maovu ikiwemo kuhamasisha ukahaba kwa kucheza ngoma za usiku maarufu kama 'Kibao Kata' bila staha.

Akizungumza kuhusu matukio hayo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini amesema Watu hao wamewakamata kutoka maeneo tofauti ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam yakiwemo, Mwananyamala, Kinondoni, Tandale, Sinza, Buza na Magomeni. Ameeleza kuwa watafikishwa Mahakamani kwa taratibu za kisheria.

Naibu Waziri Sagini amesema idadi kubwa ya wanaojihusisha na matendo hayo ambayo ni kinyume cha sheria ni wanawake na mabinti wadogo wenye umri chini ya miaka 18 ambapo uchunguzi umebaini kuwa wanawake hao wanaoonekana kukubuhu kufanya vitendo hivyo husafirishwa kwenda ughaibuni na kutumikishwa katika biashara ya ukahaba, jambo.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ACP Jumanne Muliro amesema watuhumiwa hao wanaendelea kuhojiwa na Jeshi hilo litahakikisha linaendelea kudhibiti mitandao ya watu hao ikiwa ni pamoja na kuendeleza msako na utekelezaji wa maagizo mbalimbali yatakayotolewa katika maeneo yaliyotajwa kukamatwa watuhumiwa hao.
 
hii nchi imekuwa sio huru tena

yaani mtu akate viuno akamatwe ila wanaoiba wanatesa uraiani

Hayo yanafanyika huko uswahilini huku watoto wadogo wakiangalia mambo yanayofanywa na watu zaidi ya miaka 18...

Nafikiri sio shida kama watakodi ukumbi na kuwepo wenyewe wakubwa wakivikata viuno bila uwepo wa watoto na ikiwezekana huko huko ndani wapigane miti kabisa hakuna atakayewasumbua...

Ila hii yakufanya huu ujinga wazi mtaani ikishugudiwa na watoto na wengine wasiopenda kuona huo ujinga si sawa....
 
Hayo yanafanyika huko uswahilini huku watoto wadogo wakiangalia mambo yanayofanywa na watu zaidi ya miaka 18...

Nafikiri sio shida kama watakodi ukumbi na kuwepo wenyewe wakubwa wakivikata viuno bila uwepo wa watoto na ikiwezekana huko huko ndani wapigane miti kabisa hakuna atakayewasumbua...

Ila hii yakufanya huu ujinga wazi mtaani ikishugudiwa na watoto na wengine wasiopenda kuona huo ujinga si sawa....
una uhakika unacho kinena ?
 
Noma sana!
Nakumbuka mwaka jana nilimtembelea rafiki yangu Buza,kuna ukumbi ukitoa buku unachovya kidole kimoja..elfu kumi unachovya vidole kumi mpaka mkono unaloa
 
Tandale unampa buku 5 anavuta cgara kwa exost!
 
Bwana Naibu Waziri
Huko Arusha tumesikia juu ya wizi wa kutisha wa fedha za serikali upo kimya ila la wasichana wanaotumia mauno yao kama rasilimali pekee walionao ndio unavalia njuga? 🤧
Uchafuzi uliopita umetuletea viongozi wa kipekee
Haya kawashitaki hao watoto kwa kosa la kukata mauno
 
Naamuru waachiwe mara moja,suala la kukata viuno hata bungeni wanataka uno kama kawa.
 
Kuchoshana tu. Mbona ndiyo utamaduni wa muafrika. Kucheza mapaja na maziwa nje.
 
Back
Top Bottom