Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,259
- 20,891
Muinjilisti,kwanza naomba ufahamu kuwa lengo la mimi na wewe kubadilishana mawazo kutokana na mitizamo yetu tofauti kwenye hili jambo sio kutafuta mshindi bali ni hoja zitakazopelekea kuisaidia jamii yetu na changamoto zake so sihitaji ushindi!Umesema "unalalama wadada wenye wenye magari huku wakati huohuo wazae kwa uchungu?"Sikia hilo ni tatizo lililotokana na malezi,mtu anataka aolewe au atoke na mwenye gari akifikiri hayo ndo maisha wakati ni kinyume chake!Umesema mifumo imechakachuliwa na ukataja mambo mengi na tabia nyingi mbaya za wanaume kama marioo,kupaka mkorogo nk,kwanza nakubaliana na wewe kua hili ni tatizo but limetokea wapi?Nini chanzo chake?Ukifuatilia utagundua ni tatizo lilelile la malezi,wanaofanya hivyo hawajitambui!Lakini umenishangaza,kwenye mifumo iliyochakachuliwa hukutaja na ule wa mwanamke kuyaacha majukumu yake.Umetaja ujinga wa wanaume tu!Umesema waoaji ni wachache na hao wachache wenye uwezo wa kulea familia ni wachache,pia umesema wengine ni kama akina Eiyer wanataka kuoa halafu hawana kazi!Kwanza tofautisha mtu anaetaka kuoa bila kuwa na plan au malengo na mwenye malengo.Hapa nawazungumzia wenye malengo,yaani unakua kwenye harakati za kuanzisha biashara au unatafuta kazi huku ukitafuta mchumba pia,hapa wakina dada hawawataki hawa,wanawataka wenye magari tayari!Wale wanaotaka kuoa bila malengo wana matatizo na pia ni mada nyingine!