Wanawake ni maua na muda wake wa kunyauka haukawii kufika

Wanawake ni maua na muda wake wa kunyauka haukawii kufika

Siwema mama yake alishindwa kumwandaa mapema awe kama kina Nancy sumari mwishowe akawaachia vijana Wakala na kujigaragazaa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]..
Angepewa taarifa hii mapema mkuu huenda angeshituka,nasikia siku hizi ajaribu kuongeza ukaribu wake zaidi na jamii ya mbwa?
 
Ingia kwenye Facebook yake chukua picha zake za zamani hata mbili kisha mtumie
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kila mtu anataka vitu vizuri Mkuu. Yeye aliona wewe huwezi kumpa hivyo vizuri ndio maana akaenda kwa mwengine.

ACHA KULALAMIKA UNAPOACHWA.

NB. JIPENDE MWENYEWE HUTOJUTA

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Siyo kila mahusiano yatakuwa ya kudumu na kuishia katika ndoa. Wakati mwingine watu wanakuja katika maisha yetu ili kutufundisha vitu fulani. Hata wale wanaotuumiza sana na kutuachia makovu moyoni ukichunguza vizuri ni lazima kuna funzo kubwa walilotuachia. Pengine tunapaswa kuwashukuru sana badala ya kufurahi tunapokutana nao maisha yakiwa yamewaelemea. Maisha haya hayana fundi ati!
 
Mkuu inaonekana umefurahi kweli kweli. Na huwa nashangaa sana nikiona mtu anafurahi baada ya kumuona ex wake aliyepigwa na maisha. Mtu mlideti. You shared your past together. Things didn't work out - pengine kwa sababu ya utoto, kutokuyajua maisha sawasawa au tu mlikuwa tofauti sana na msingeweza kukaa pamoja hata mngejaribu vipi. Kwa nini ufurahi ukiona mwenzio pengine hayupo katika hali uliyomtegemea kuwa nayo?

Na kuna guarantee yo yote kwamba angebakia na wewe angekuwa bado anaendelea kung'aa? Unafikiri kinachomng'arisha mwanamke ni pesa peke yake? Na ina maana wanawake wasiwe na vigezo vyao bali wawe kama kokoro tu kumng'ang'ania popoma ye yote hata kama hana vigezo walivyojiwekea? Kwa nini thamani ya mwanamke kama binadamu
huru na kamili inafungamanishwa na kuwa na mwanaume hata kama huyo mwanaume ni boya tu asiye na sifa hata moja ya kuitwa mume wa mtu?

Na siyo kila mahusiano yatakuwa ya kudumu na kuishia katika ndoa. Wakati mwingine watu wanakuja katika maisha yetu ili kutufundisha vitu fulani. Hata wale wanaotuumiza sana na kutuachia makovu moyoni ukichunguza vizuri ni lazima kuna funzo kubwa walilotuachia. Pengine tunapaswa kuwashukuru sana badala ya kufurahi tunapokutana nao maisha yakiwa yamewaelemea. Maisha hayana fundi ati!
Unajishangza we hujui kuwa Adui muombee njaa.

Hii ni kanuni ya kawaida hata kama.unajifanya wewe hauko hivyo.
 
Mkuu inaonekana umefurahi kweli kweli. Na huwa nashangaa sana nikiona mtu anafurahi baada ya kumuona ex wake aliyepigwa na maisha. Mtu mlideti. You shared your past together. Things didn't work out - pengine kwa sababu ya utoto, kutokuyajua maisha sawasawa au tu mlikuwa tofauti sana na msingeweza kukaa pamoja hata mngejaribu vipi. Kwa nini ufurahi ukiona mwenzio pengine hayupo katika hali uliyomtegemea kuwa nayo?

Na kuna guarantee yo yote kwamba angebakia na wewe angekuwa bado anaendelea kung'aa? Unafikiri kinachomng'arisha mwanamke ni pesa peke yake? Na ina maana wanawake wasiwe na vigezo vyao bali wawe kama kokoro tu kumng'ang'ania popoma ye yote hata kama hana vigezo walivyojiwekea? Kwa nini thamani ya mwanamke kama binadamu
huru na kamili inafungamanishwa na kuwa na mwanaume hata kama huyo mwanaume ni boya tu asiye na sifa hata moja ya kuitwa mume wa mtu?

Na siyo kila mahusiano yatakuwa ya kudumu na kuishia katika ndoa. Wakati mwingine watu wanakuja katika maisha yetu ili kutufundisha vitu fulani. Hata wale wanaotuumiza sana na kutuachia makovu moyoni ukichunguza vizuri ni lazima kuna funzo kubwa walilotuachia. Pengine tunapaswa kuwashukuru sana badala ya kufurahi tunapokutana nao maisha yakiwa yamewaelemea. Maisha hayana fundi ati!
Hiiiiiii bhagosha!
 
Imekuwa kawaida katika dunia ya leo kwa wasichana kuufaidi usichana bila kuangalia future yao. Wengi wamepoteza future zao kwa kujiona ni warembo sana na kujiona tayari wao ni watu maarufu (celebrities) na wanastahili kuepukwa na watu wa hali ya chini na kujiwekea vigezo na masharti ya nani anastahili na asiyestahili kuwa nae katika uhusiano, urafiki n.k.

Bila shaka wanaume wengi wamejikuta katika uhusiano wa kudumu hadi ndoa na wanawake wa kawaida sana au mahusiano ya muda mfupi na warembo wazuri kwa sababu ya uthamani waliojiwekea kiasi kwamba kuwa nae unahitaji kutumia gharama kubwa kuhudumia.

Wengine wamejikuta wakilaani ndoa kwa sababu zilezile na kuanzisha kampeni za KATAA NDOA, NI UTAPELI kwa sababu inawezekana kweli ni utapeli kuhudumia mwanamke aliyejiweka ni wa thamani sana.

Nimeandika haya kwa sababu hivi leo nimekutana na mwanamke ambaye nilikuwa nae kimahusiano mwaka 2015 alikuwa mrembo sana, sikuweza kuhudumia kwa sababu sikufikia vigezo vyake nikaamua kukaa pembeni. Nilivyomona nilipata jibu kumbe WANAWAKE NI MAUA HAYAKAWII KUNYAUKA, hata mvuto tena wa kujiposti mtandaoni kama ilivyokuwa kila siku post zaidi ya 5 facebook. Ilikuwa ni pambo ambalo akiwa mtandaoni ni wamoto haswa, ila kwa sasa uangavu wa sura, mvuto havipo tena.

Makunyanzi yameanza na sura ya huzuni ya kuzalishwa na mume wa mtu ambaye sidhani kama yupo karibu nae tena. Nimejiuliza sana hata akinipa mzigo naweza nishindwe kufanya nae mapenzi, kwa sababu siyo yule aliyeng'ara kila sehemu. In short NOT ATTRACTIVE
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Siwema mama yake alishindwa kumwandaa mapema awe kama kina Nancy sumari mwishowe akawaachia vijana Wakala na kujigaragazaa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]..
Vijana wa ovyo kabsaaa wamemkula dada wa watu wakamtupa kama Big G

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kwahiyo angekukubali asingeota hayo makunyanzi😀😀😃😃
 
Makunyanzi yameanza na sura ya huzuni ya kuzalishwa na mume wa mtu ambaye sidhani kama yupo karibu nae tena.

Miaka hiyo alikuona takataka,labda kwa mambo ya kijingajinga. Na leo umekuwa lakini yale yale.
-Umejuaje kazaa na mme wa mtu?
-Kakwambia alibakwa,au hiari?
-Kaomba msaada? Umemsaidia hujamsaidia, hilo sisi linatusaidia nini!!! Alikuwa na haki kukupotezea, pamoja na kwamba mada yenyewe inaeleweka.

Nimejiuliza sana hata akinipa mzigo naweza nishindwe kufanya nae mapenzi, kwa sababu siyo yule aliyeng'ara kila sehemu. In short NOT ATTRACTIVE.

Ulipomuona tu, ngono, ngono!!!!!
Hahahahahahaha vijana wa siku hizi. Pengine alikukataa kwa tabia ambayo bado unayo. Je,una uhakika anaweza kukuvulia kweli,au unajifariji tu!!!
Dada vipi mbona povu???
 
Sawa.

Yawezekana ungemuoa angekuwa amechakaa zaidi pia. Au yawezekana huko kuchakaa kuko kichwani mwako tu maana ndicho unatamani kitokee.
Wewe ndiye umefikiria vizuri kwa kuuona ukweli kuliko mtoa mada.
Maana yeye yupo mkusali dua la kuku tu, kumuombea mabaya yampate huyo mwanamke.

Mbona miye niliwahi kumpenda mama wa makamo kunizidi.

Kumbe sasa, kwa kauli ya mtoa mada, wanawake wakongwe hawawezi kupendwa, wakati watu wanawasorolea kama walivyo wasichana tu!

Ingawa vijana wenzangu walikuwa wakinambia... "Kulala na mwanamke alokuzidi umri ni sawa na kusoma gazeti la zamani", mf: la mwaka jana December uje kulisoma leo halafu ujidai kufuatilia matukio current affairs! 😆😆😆.
Mimi wala sikujali.
 
Back
Top Bottom