Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

toka hapo ikanipa funzo, mambo ya kulipia videti sitaki mie, kideti nilipie, kunitongoza unitongoze ebooooh....ila kwa sasa ninalipa (sometimes) maana nikitoka natoka na mume wangu....... hata nikilipa ina thamani....
BADILI TABIA kwa kweli sikujua.........kumbe kutongoza huwa kunalipiwa.............
Kwa hiyo kama huyo jamaa angelipia hicho ki-date ingekuwa ni halali kabisa kukutongoza na huenda ndiye angekuwa hubby wako leo hii..................Just thinking loud.............LOL
 
Last edited by a moderator:
asa ilipofika jumamosi nilimuona kwa mbaali akapunga mkono na kuingia mitini, hamad jumapili nikawa naenda macdonad kula nikakutana nae njiani, akaamua kunijoin, nikamruhusu vizuuuuri, nikafika nikaagiza, then nikamuita mhudumu nikamwambia nipe bili yangu chips kuku zangu na juisi tu huyu kaka atajilipia mwenyewe...(halafu alikuwa ameagiza na take away za kuwapelekea madogo zangu home) jamaa alimind mpaka kesho........

hahhaa na dawa ndo hiyo hahhaha uwiii
 
asingekuwa mume wangu, si unajua mume mwema hutoka kwa Bwana? ila (mtazamo wangu binafsi) mwanaume 1st date lazima uonyeshe uanaume wako, lipia kidate, unless kama mwanamke ndo kakualika.... yaani imagine nimlipie yeye, na rafiki yake aliyemualika bila kutarajia? kwa kweli hapana, napenda mwanaume anayetake responsibility.....unajua Mtambuzi kwenye 1st date mimi hujitahidi kumsoma mwanaume, hususan vitu vidogo vidogo vingi..... na 1st impression ukiharibu umeumia.....



 
Last edited by a moderator:
Kumbe ndio maana nilimkosa MARIETTA. Kwenye 1st date nilimpiga mzinga, nakumbuka kipindi hicho nilikuwa sina kazi halafu nilikuwa nimeuawa mbayaa.........................LOL
 
Hizo gharama sisi wahasibu tunaita SUNK COST. Mfano wake ni mtu anayetafuta madini. Zile gharama anazotumia kujua kama kuna madini au la zitakuwa zimetumika whether amepata madini au la
 
hahaha..nimekumbuka one day nilitaka kumtoa my baby for lunch..baada ya ku-order nikashtukia kwamba i dont have my wallet with me!!!
Nkajifanya kwenda kwenye supermarket kutafuta hairspray kumbe naenda nyumbani kuchukua wallet!!that was a close save...i dont think he realised what had happened!
 
Du. Nimeshangaa sana na wala cjategemea km karne hii bado watu munamawazo ya aina hii.
Dating ina maanaisha kila mtu yuko ktk kumpima mwenzake kama anafaa...why not sharing cost?
Akina mama/dada acheni kuwa tegemezi...share bill na onyesha nawewe you are responsible person.

Nilichokiona hapa ni wanawake wa kibongo bado muna MINDSET duni kuwa siku zote na mahala popote mwanaume ndo kila kitu...wrong! Very wrong!

Mi nimeishi ujerumani...ukimudate demu...analipia bill yake na ww unalipa yako.

Kwan kuku date maana yake nakutumia? Muna maana ww hufaidiki kwa lolote?

Ladies u must change ur mindset!!
 
Hivi wewe ulikuwa wapi toka jana......?
Wanaume wengi wamekwepa kuchangia hii mada kwa kuogopa kuonekana ni wabahili........ Nilikuwa nasubiri mtu mwenye mtazamo tofauti ili kujaribu kubadili mindset za dada zetu, na kwa bahati mbaya sana, wanawake wanaochangia huu uzi wote wameolewa, wale wanaotarajia kuingia katika mahusiano wamekimbia, au wanachangia juu juu tu..........

Ninayo mifano mingi sana: Nakumbuka kuna mdada tulikuwa tunafanya naye kazi akaombwa mtoko na mfanyakazi mwenzetu raia wa Uingereza..... siku iliyofuata nilimsikia akiwasimulia wenzie akiwaonya kwamba wasikubali kutoka na huyo mzungu kwani ni bahili sana. Walikwenda kula kwenye mghahawa wa kitalii na jamaa akatumia nafasi hiyo kumtongoza lakini mwisho wa siku kaitisha bili yake peke yake na kulipa. Ni bahati tu yule binti alikuwa na pesa kwenye mkoba wake la sivyo angesafisha masufuria siku hiyo.......
Labda niwatahadharishe wa dada, iwapo wenzetu hawa kutoka ughaibuni (Wazungu) wakikuomba mtoko inabidi uhakikishe unazo fedha za kujigharamia labda tu akwambie yeye atalipa bill, la sivyo itakula kwako......LOL
 
Mtambuzi ukitaka kushare cost na wewe nenda ujerumani ukadate huko, sisi ni waafrica, tena watanzania
mwanaume shurti uonyeshe uanaume wako....... Pia kidate wewe si umeomba? Kisaa cha kunilipisha wakati mie sikuweka bajeti ya videti?

Narudia tena, kidate nichangie,
bado unitongoze loh.......
Nikilipa ujue nitatongoza mie alaaaah

 
Last edited by a moderator:
Nikikualika nitakua nimejiandaa japo naweza nisilipe kama nikiona Mwanaume anataka kulipa yeye au tutashare cost kama Mwanaume ataonekana hataki kulipiwa Jumla.
Ila kama umenialika ujiandae kugharamia, nilijijua sina hela nikatuli nyumbani, wewe umenitoa alipie nani?
 
akohi, acha kukariri.

Aliyekuambia maisha ya ujerumani ndio marking scheme ya maisha ya watu wote ni nani???

Hiyo mindset duni ya wanawake wa kibongo ni ipi!

Hebu msome Okot P'Biteki vizuri.

Usijifanye 'Ocol' mmmoja kati ya jamii kubwa, wee ndo utaonekana 'kilaza'

kwani, unavyooa, anayefaidika na ndoa ni nani?

Kwa nini familia ikilala njaa anayetizamwa baba?

Nenda magharibi au mashariki, hata huko ujerumani, kaya ilale njaa ndio utajua nafasi ya mwanamme ndani ni ipi.

Siwezi badili mindset kwa hoja ndogo hivi.

Huu ni ukwepaji wa majukumu tu, hakuna lolote.
 
Last edited by a moderator:
BADILI TABIA kwa kibongo bongo sawa, lakini kwa wazungu, mtaishia kuosha masufuria ya Hoteli kwa kushindwa kulipa bili ya vile mlivyotumia kwa fujo mkidhani mmepata Mzungu...... ......LOL
 
Last edited by a moderator:
Kongosho, tunawatahadharisha na utandawazi huu.........!
Mtajutaaaa, jiangalieni... Chezea Jerumani weye......!
 
Last edited by a moderator:
yani unanifanya nispend my cash bila kutegemea kisa unataka kunitongoza??..hiyo ni financial rape....you invite me out na unilipie tuuu...
 
Mmeelewa eeh?
Chukueni Point
Hizo gharama sisi wahasibu tunaita SUNK COST. Mfano wake ni mtu anayetafuta madini. Zile gharama anazotumia kujua kama kuna madini au la zitakuwa zimetumika whether amepata madini au la
 
yani unanifanya nispend my cash bila kutegemea kisa unataka kunitongoza??..hiyo ni financial rape....you invite me out na unilipie tuuu...
Wenzako walitoa mtazamo wao, huo hapo chini kulingana na heading ya mada hii...................

 
Mtambuzi, siwezi date mwanamme ambaye hata sahani ya chakula kwake ni ishu, mie msukuma bwana chakula si kitu ambacho mwanamme anatakiwa kukilalamikia ni 'aibu' kubwa.

Kama huwezi mlisha tu hata mwanamke uliyenaye, what kind of a man are you?

Never!

Kama ananitoa out, anilishe tena nitosheke, kama hana hela alete mchele na mie ntatafuta mboga na kuni mie ntapika home.

Hao wazungu haiwezi tokea nkawadate maana si upepo wangu kabisa hata ikitokea ile ananiambia ananitoa na mwambia mapema, msosi ni juu yako.

Chazeiya Konnie kwenye msosi wewe
 
Last edited by a moderator:
ha ha ha ha, tena atakuwa financial molester.

yani unanifanya nispend my cash bila kutegemea kisa unataka kunitongoza??..hiyo ni financial rape....you invite me out na unilipie tuuu...
 
Nimechekaje, mpaka mama Ngina ananishangaa hapa........................
Ha ha ha haaaaaaaa Konnie.............. Chezea Wasukuma weye.......LOL
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…