BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 525
- 1,257
Abiria Wanawake Kisiwani Pemba, wamelalamikia tabia ya baadhi ya madereva wa pikipiki ‘boda boda’ kuwaingia mwilini wakati wanapokuwepo kwenye vituo vyao, kutaka usafiri wa aina hiyo.
Walisema mara unapofika kwenye eneo lao la vituo na kutaka usafiri, huvamiwa na kuanza kukukopea mizigo na wengine kuwashika mikono, wakivutiana kwenye chombo chake.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwenye eneo la Mtuhaliwa wilaya ya Mkoani Pemba, walisema wamekuwa wakisikitishwa na tabia hiyo.
Mmoja kati ya wanawake hao aliyekataa jina lake lichapishwe alisema, baadhi ya waendesha boda boda hao, wamekua wakiwaingia mwilikini, kwa lengo la kufanya ushawishi.
Alieleza kuwa, kinachowaudhi ni kule kuanza kupokea kuanzia mizigo mikubwa hadi vipochi vya mkononi, na wengine kukumata mikono.
‘’Ukiteremka gari tu, wanaaza kukuzonga, wengine wanakupokea hata vipochi vyenye simu, na wengine wanaanza kukushika shika mikono, wakitaka upande boda bado yake,’’alisema.
Kazija Issa Mohamed wa Mwambe alisema, juzi kwenye kituo cha boda boda cha Mtambile-Kengeja aliangushwa chini, baada ya waendesha boda boda, kuvutia mkoba wake.
Alieleza kuwa, mara alipoteremka gari akitokea Chake chake, alishuhudia ameshadakwa na wendesha boda boda, na kuvutwa kwa ghafla mkoba wake na kuanguka chini.
‘’Hawa waendesha boda boda baadhi yao sio wastaarabu, maana wamekuwa wakituingia maungoni kutaka abiria, jambo ambalo sio zuri,” alieleza.
Kwa upande wake Mmanga Haji Kassim, alisema juzi mume wake aligombana na mwendesha bodaboda eneo la Kenya-Chambani, baada ya kumvamia mke wake.
“Ni kweli waendesha bodaboda wengi wao hawana nidhamu, maana mimi juzi kushuka gari wakati mume wangu yupo na usafiri ananisubiri, yeye ameshanikamata mkono,’’alilalamika.
Mwendesha bodaboda wa njia ya Mtambile-Kengeja Mohamed Haji, alisema wamekuwa wakikatazana jambo hilo, ingawa badhi yao wapo watukutu.
“Ndio maana tulitaka tuweka zamu, ili kuepusha hilo, lakini bado hatujakubaliana na ndio maana, tumekuwa tukishtumiwa kuwafanyia vurugu abiria hasa wa kike,’’alieleza.
Mwendesha bodaboda wa Machomane Chake Chake, Issa Kassim Issa, alisema nidhamu na ustaarabu ndio jambo ambalo wamekuwa wakisisitiza kila siku na viongozi.
Mwenyekiti wa waendesha bodaboda mkoa wa kusini Pemba Kassim Juma, aliwataka abiria wanawake kuripoti katika vyombo vya sheria, wanapogundua kuvunjiwa haki zao.
‘’Hakuna hata bodaboda mmoja, aliyeruhusiwa kumvamia abiria, bali kama kuna zamu ndio jambo jema kama hakuna, aulizwe kistaarabu,’’alisisitiza.
Hivi karibuni mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud aliwataka waendesha boda boda hao, kutojihusisha na kitendo cha aina yoyote, kinachoashiria uvunjifu wa haki za binadamu.
Kwa sasa kisiwa cha Pemba kina wastani wa bodaboda 300, zikiwemo zile zilizotolewa kwa njia ya mkopo kutoka kwa Rais wa Zanzibar chini ya benki ya CRDB na wafadhali wengine.
Chanzo: pembatoday
Walisema mara unapofika kwenye eneo lao la vituo na kutaka usafiri, huvamiwa na kuanza kukukopea mizigo na wengine kuwashika mikono, wakivutiana kwenye chombo chake.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwenye eneo la Mtuhaliwa wilaya ya Mkoani Pemba, walisema wamekuwa wakisikitishwa na tabia hiyo.
Mmoja kati ya wanawake hao aliyekataa jina lake lichapishwe alisema, baadhi ya waendesha boda boda hao, wamekua wakiwaingia mwilikini, kwa lengo la kufanya ushawishi.
Alieleza kuwa, kinachowaudhi ni kule kuanza kupokea kuanzia mizigo mikubwa hadi vipochi vya mkononi, na wengine kukumata mikono.
‘’Ukiteremka gari tu, wanaaza kukuzonga, wengine wanakupokea hata vipochi vyenye simu, na wengine wanaanza kukushika shika mikono, wakitaka upande boda bado yake,’’alisema.
Kazija Issa Mohamed wa Mwambe alisema, juzi kwenye kituo cha boda boda cha Mtambile-Kengeja aliangushwa chini, baada ya waendesha boda boda, kuvutia mkoba wake.
Alieleza kuwa, mara alipoteremka gari akitokea Chake chake, alishuhudia ameshadakwa na wendesha boda boda, na kuvutwa kwa ghafla mkoba wake na kuanguka chini.
‘’Hawa waendesha boda boda baadhi yao sio wastaarabu, maana wamekuwa wakituingia maungoni kutaka abiria, jambo ambalo sio zuri,” alieleza.
Kwa upande wake Mmanga Haji Kassim, alisema juzi mume wake aligombana na mwendesha bodaboda eneo la Kenya-Chambani, baada ya kumvamia mke wake.
“Ni kweli waendesha bodaboda wengi wao hawana nidhamu, maana mimi juzi kushuka gari wakati mume wangu yupo na usafiri ananisubiri, yeye ameshanikamata mkono,’’alilalamika.
Mwendesha bodaboda wa njia ya Mtambile-Kengeja Mohamed Haji, alisema wamekuwa wakikatazana jambo hilo, ingawa badhi yao wapo watukutu.
“Ndio maana tulitaka tuweka zamu, ili kuepusha hilo, lakini bado hatujakubaliana na ndio maana, tumekuwa tukishtumiwa kuwafanyia vurugu abiria hasa wa kike,’’alieleza.
Mwendesha bodaboda wa Machomane Chake Chake, Issa Kassim Issa, alisema nidhamu na ustaarabu ndio jambo ambalo wamekuwa wakisisitiza kila siku na viongozi.
Mwenyekiti wa waendesha bodaboda mkoa wa kusini Pemba Kassim Juma, aliwataka abiria wanawake kuripoti katika vyombo vya sheria, wanapogundua kuvunjiwa haki zao.
‘’Hakuna hata bodaboda mmoja, aliyeruhusiwa kumvamia abiria, bali kama kuna zamu ndio jambo jema kama hakuna, aulizwe kistaarabu,’’alisisitiza.
Hivi karibuni mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud aliwataka waendesha boda boda hao, kutojihusisha na kitendo cha aina yoyote, kinachoashiria uvunjifu wa haki za binadamu.
Kwa sasa kisiwa cha Pemba kina wastani wa bodaboda 300, zikiwemo zile zilizotolewa kwa njia ya mkopo kutoka kwa Rais wa Zanzibar chini ya benki ya CRDB na wafadhali wengine.
Chanzo: pembatoday