Wanawake tusaidiane hili na wanaume tunahitaji ushauri wenu

Wanawake tusaidiane hili na wanaume tunahitaji ushauri wenu

cutelove

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2017
Posts
3,448
Reaction score
7,972
Kwa nini mwanamke akifiwa mume na akaachiwa biashara au miradi mikubwa kwa nini miradi hufa mapema na kama mwanamke amejitahidi sana kusimamia hata miaka 5 haifiki

Na yawezekana mwanamke alikuwa anashirikishwa kikamilifu kwenye miradi kwa nini inafeli..

Sio wote lakini walio wengi biashara au miradi inakufa mapema na wengi nimewashuhudia walifiwa wakaachiwa mali lakini muda mchache kila kitu kinakuwa kimeisha

Tusaidiane tatizo ni nini na ila kwa wanaume ni tofauti,wenyewe wakifiwa mali zao au biashara zao huendelea kama kawaida ila kwa wanawake walio wengi huanza kufilisika,tunakosea wapi?
 
Wakati wa uhai, mara nyingi ushirikishwaji wa wanawake ni mdogo sana, kwa maana hiyo, mwanamke haelewi uendeshaji wa miradi ya mumewe inavyoenda.

Anaweza akapata picha kwa mbaali na taarifa fupi za miradi, kama hajui kwa undani mambo yanavyoendeshwa inakua shida sana kuindeleza hiyo miradi kwa ufanisi.
 
Wakati wa uhai, mara nyingi ushirikishwaji wa wanawake ni mdogo sana, kwa maana hiyo, mwanamke haelewi uendeshaji wa miradi ya mumewe inavyoenda.

Anaweza akapata picha kwa mbaali na taarifa fupi za miradi, kama hajui kwa undani mambo yanavyoendeshwa inakua shida sana kuindeleza hiyo miradi kwa ufanisi.
Kwa hiyo makosa ni mwanaume kutomshirikisha kikamilifu mke wake wakati wa uhai wake
 
wanawake wajane wenye pesa nyingi ndio wanaongoza kwa kulea viben10 nahisi hii pia inaweza kuwa sababu
 
Kwa hiyo makosa ni mwanaume kutomshirikisha kikamilifu mke wake wakati wa uhai wake

Hilo ni kosa moja kwa upande wangu. Lakini pia miradi/biashara nyingi haziendeshi kwa uwazi au kama tunavyoona. Zingine zina mambo ya ndani kiasi kwamba hata iweje mwanamke hawezi kuambiwa.
 
Back
Top Bottom