Uchaguzi 2020 Wanawake wa Jiji la Mbeya wamlipia fomu Mbunge wa milele wa jimbo hilo, Joseph Mbilinyi(Sugu) na kumpelekea nyumbani kwake

Hivi jiji la Mbeya lina askari polisi wangapi? Kwenye uchaguzi mkuu hakuna kuomba msaada wa polisi eneo jingine, kila mmoja anapambana na hali yake. Wananchi wakigangamala hakuna kura ya kuibiwa, labda mawakala wawe wazembe!
Polisi wanaweza wasaidia kwenye chaguzi za marudio tu, uchaguzi mkuu awatoshi nchi nzima ni wachache.
 
Yule Dada akiona hii habari kishuzi cha yusufu kitahusika!
 
7 Julai 2020
Mbeya, Tanzania

WAZEE WA KIMILA MBEYA WAMCHANGIA DR. TULIA ACKSON, FOMU YA UBUNGE


Naibu spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bi. Tulia Ackson Mwansasu akutana na viongozi wa kimila (machifu) walioongozwa na Chifu Mkuu wa Machifu wa Rungwe Chifu Joel Burton Mwakatumbula ili anapokwenda kutia nia wanampa kichache na kumtakia kila la kheri anapokwenda kugombea.
Source : MbeyaYetuOnlineTV
 
sioni mtu wa kumtoa sugu hapa, wapo wanaojaribu kwa kutoa misaada lakini wanachosahau ni kwamba sugu yupo mioyoni mwa wana mbeya na sio mifukoni.

yupo mioyoni mwetu, Hata wakimsingizia haleti maendeleo tunabaki kucheka tu maana kodi tunakusanya nyingi tu na sugu hahusiki kwenye kupanga hio kodi tunayokusanya itumikaje.
 
Nadhani Ma Ded watakua wanatangaza matokeo huku familia zao wameshaziondoa mkoa husika na akimaliza kutangaza tu hapo hapo anaondolewa kwa kasi na kuhamishwa kituo cha kazi kabisa aisee.
 
mkuu subiri dawa ikuingie vizuri,
 
Huyu bila shaka kakimbia Mbeya Mjini , Saul ajiandae
 
Nadhani Ma Ded watakua wanatangaza matokeo huku familia zao wameshaziondoa mkoa husika na akimaliza kutangaza tu hapo hapo anaondolewa kwa kasi na kuhamishwa kituo cha kazi kabisa aisee.
mkuu umepiga chura teke na kumuongezea mwendo umeeleza vizuri zaidi sayansi ya wizi wa kura na bao la mkono inavyotakiwa kufanyika practically kuhakikisha ile timu nzima ya waropokaji wanaopinga juhudi inabaki mtaani maana bunge ndio platform yao kubwa ukiwatoa mjengoni DJ Makengeza na kampuni yake kwanza watakosa pesa na nguvu ya kufanya uchochezi na watasambaratika!!

Sugu, Professa J, ZZK na DJ and co kwa maslahi ya nchi hawapaswi kurudi mjengoni mbinu ni hiyo tayari ipo na nzuri kabisa!!
 
View attachment 1499535

Hili kwangu ni jambo jipya kidogo, kwa wanawake wenye uwezo wa kawaida kumlipia fomu Mbunge mstaafu mwenye marupurupu kibao, si jambo la kawaida hata kidogo.

Ama kwa Hakika kutoa ni moyo.
Tulia lazima ashinde hata kwa kuiba kura au kwa ubabe sidhani kama watamuacha naibu speaker ashindwe na watakuwa wamejipanga kutimiza hilo hata kwakutumia nguvu hadi watu walale
 
Kazi ipo[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…