Wanawake wa kibongo na wivu huu

Wanawake wa kibongo na wivu huu

Dear

Member
Joined
Nov 18, 2009
Posts
46
Reaction score
3
Salaam wa JF
Mimi kila siku uwa najiuliza kwa nini sisi Wanawake tuna huu wivu,
Kama mimi ni mdada na nina marafiki wa kiume yaani si wakimapenzi washkaji tu,
yaani mlisoma wote,
sasa mmoja wa rafiki kama akioa,siku mkakutana labda kwenye party na mke wake,au njiani atakuchunia na siku ingine anakutafuta ebwana ehh samahani sana nilikuchunia siku ile nilikuwa na wife yaani wife wangu anawivu sana,nikisalimiana na wadada ananuna siku nzima.
Kuna Kaka mmoja pia nilisoma naye,wakati tuko chuo tulikuwa washkaji ile mbaya,alafu tulikuwa tumezaliwa tarehe moja mwaka mmoja,hivo tulikuwa tunaitana pacha,
sasa baada ya kupotezana kama miaka 3,tukaonana town,pembeni akiwa na mchumba,alivyoniona kwa kweli alishidwa kuvumilia na kunihug,pacha vipi upo,yaani nimekutafuta kichizi,story story za salam baada ya kuisha,akaniambia,mshikaji ehh uyu mchumba wangu,sasa yule dada bwana alikuwa amekasirika nusura apasuke
mimi nikampa hongera,sasa nataka nimpe mkono yule dada kwa salamu akatoa nje,akaangalia pembeni hakunisalimia kabisa,
basi yule kaka aliona aibu sana akasema ahh mchumba naona kachoka sana leo,basi mie kuona hivyo nikaona niage mapema.

Sasa hii najua sio kwangu tu imewatokea na wengine,swali ni je sisi wadada wa KiTZ tunamatatizo gani jamani,kwa maana kama mumeo asiwe anasalimiana na wadada aliosoma nao au kukua nao mtaani kisa wewe.
Je huu wivu ni kutojiamini au ni nini?
Na hizi tabia pia wakaka wanazo sometym wakiwa na wake zao au girlfriend wanajifanya hawakujui kabisa.
Mlio nje mtupe data za huko je wazungu pia wako hivyo kama waBongo?
 
Hao ni wale wanaume wasiojiamini hata kidogo ...kumsalimia mtu na kutambulisha sio tatizo kiivyo Labda urafiki wa mashaka
 
Salaam wa JF
Mimi kila siku uwa najiuliza kwa nini sisi Wanawake tuna huu wivu,
Kama mimi ni mdada na nina marafiki wa kiume yaani si wakimapenzi washkaji tu,
yaani mlisoma wote,
sasa mmoja wa rafiki kama akioa,siku mkakutana labda kwenye party na mke wake,au njiani atakuchunia na siku ingine anakutafuta ebwana ehh samahani sana nilikuchunia siku ile nilikuwa na wife yaani wife wangu anawivu sana,nikisalimiana na wadada ananuna siku nzima.
Kuna Kaka mmoja pia nilisoma naye,wakati tuko chuo tulikuwa washkaji ile mbaya,alafu tulikuwa tumezaliwa tarehe moja mwaka mmoja,hivo tulikuwa tunaitana pacha,
sasa baada ya kupotezana kama miaka 3,tukaonana town,pembeni akiwa na mchumba,alivyoniona kwa kweli alishidwa kuvumilia na kunihug,pacha vipi upo,yaani nimekutafuta kichizi,story story za salam baada ya kuisha,akaniambia,mshikaji ehh uyu mchumba wangu,sasa yule dada bwana alikuwa amekasirika nusura apasuke
mimi nikampa hongera,sasa nataka nimpe mkono yule dada kwa salamu akatoa nje,akaangalia pembeni hakunisalimia kabisa,
basi yule kaka aliona aibu sana akasema ahh mchumba naona kachoka sana leo,basi mie kuona hivyo nikaona niage mapema.

Sasa hii najua sio kwangu tu imewatokea na wengine,swali ni je sisi wadada wa KiTZ tunamatatizo gani jamani,kwa maana kama mumeo asiwe anasalimiana na wadada aliosoma nao au kukua nao mtaani kisa wewe.
Je huu wivu ni kutojiamini au ni nini?
Na hizi tabia pia wakaka wanazo sometym wakiwa na wake zao au girlfriend wanajifanya hawakujui kabisa.
Mlio nje mtupe data za huko je wazungu pia wako hivyo kama waBongo?
Mi nipo ndani ngoja niuchune tu!
 
Tatizo ni wanaume wengi wa kiafrica kukosa kuwa waaminifu. Hivyo mdada yule alidhania kuwa anaibiwa mbele ya macho yake. Na visingizio ni hivyo hivyo ohh tulisoma wote. Pili inategemea wanaaminiana kiasi gani huenda mdada anajua jamaa akiachiwa sekunde tu zipu ilishafunguka!!
Watu wa nje at least wanajitahidi kuwa waaminifu. Akikuambia huyu tulisoma wote ni kweli. Na kama alikuwa girlfriend wake wa zamani basi atakutambulisha kuwa huyu ni X wangu. Hata kama ni wewe umeolewa basi utamwambia jamaa huyu alikuwa X wangu wa zamani na hakuna taabu. mnakaa na kununuliana kahwa!! hata kukaribishana nyumbani!! Je sie a kina MAGANGA TUNAWEZA HAYO?? waswahili husema kisima ulichokunywa maji husahau- waweza kumbushia ati!!
wengine waendeleze na kumalizia.
 
Salaam wa JF
Mimi kila siku uwa najiuliza kwa nini sisi Wanawake tuna huu wivu,
Kama mimi ni mdada na nina marafiki wa kiume yaani si wakimapenzi washkaji tu,
yaani mlisoma wote,
sasa mmoja wa rafiki kama akioa,siku mkakutana labda kwenye party na mke wake,au njiani atakuchunia na siku ingine anakutafuta ebwana ehh samahani sana nilikuchunia siku ile nilikuwa na wife yaani wife wangu anawivu sana,nikisalimiana na wadada ananuna siku nzima.
Kuna Kaka mmoja pia nilisoma naye,wakati tuko chuo tulikuwa washkaji ile mbaya,alafu tulikuwa tumezaliwa tarehe moja mwaka mmoja,hivo tulikuwa tunaitana pacha,
sasa baada ya kupotezana kama miaka 3,tukaonana town,pembeni akiwa na mchumba,alivyoniona kwa kweli alishidwa kuvumilia na kunihug,pacha vipi upo,yaani nimekutafuta kichizi,story story za salam baada ya kuisha,akaniambia,mshikaji ehh uyu mchumba wangu,sasa yule dada bwana alikuwa amekasirika nusura apasuke
mimi nikampa hongera,sasa nataka nimpe mkono yule dada kwa salamu akatoa nje,akaangalia pembeni hakunisalimia kabisa,
basi yule kaka aliona aibu sana akasema ahh mchumba naona kachoka sana leo,basi mie kuona hivyo nikaona niage mapema.

Sasa hii najua sio kwangu tu imewatokea na wengine,swali ni je sisi wadada wa KiTZ tunamatatizo gani jamani,kwa maana kama mumeo asiwe anasalimiana na wadada aliosoma nao au kukua nao mtaani kisa wewe.
Je huu wivu ni kutojiamini au ni nini?
Na hizi tabia pia wakaka wanazo sometym wakiwa na wake zao au girlfriend wanajifanya hawakujui kabisa.
Mlio nje mtupe data za huko je wazungu pia wako hivyo kama waBongo?

Hapo kwenye red ndio jibu lako! Actually hiyo ipo kwetu sote sio wadada peke yenu; mie nina dada amabye mumewe amepora mpaka email yake ya yahoo na kuna wakati ukiingia yahoo mesenja akikuona tu anaanza kucha kukuchimba!

Ni mbaya sana; enzi zile tukiwa ma-Playaza ukinifanyia hivi maan yake unanialika eeh bana si ushanishutumu na kunihukumu; basi mie namalizia kwa kutenda!😡
 
Wanawake wa kibongo na wivu huu
Dear
user_online.gif
Today, 09:55 AM
FL1 vipi hapo kwenye RED


Hao ni wale wanaume wasiojiamini hata kidogo ...kumsalimia mtu na kutambulisha sio tatizo kiivyo Labda urafiki wa mashaka
 
fl1 vipi hapo kwenye red

hahahah kimey hapo kwenye red ndo hivohivo kama nimeelewa topic vizuri pale jamaa kashindwa kusalimia harafu baadae anarudi sorry nilishindwa kukusalimia maana wife ana wivu
teteteteh kwa nini usijiamini utoe salam kisha utambulishe
 
Tatizo walio nje bado kuamka mida hii. Ngoja nisepe.(Hangover ya man u, bado kwisha kichwani)😀😀😀
ha ha ha hommie acha tu nagugumia maji tu leo nikiweka za kinoname usintenge maana wajua yaliyo nisibu!!
 
Tatizo ni wanaume wengi wa kiafrica kukosa kuwa waaminifu. Hivyo mdada yule alidhania kuwa anaibiwa mbele ya macho yake. Na visingizio ni hivyo hivyo ohh tulisoma wote. Pili inategemea wanaaminiana kiasi gani huenda mdada anajua jamaa akiachiwa sekunde tu zipu ilishafunguka!!
Watu wa nje at least wanajitahidi kuwa waaminifu. Akikuambia huyu tulisoma wote ni kweli. Na kama alikuwa girlfriend wake wa zamani basi atakutambulisha kuwa huyu ni X wangu. Hata kama ni wewe umeolewa basi utamwambia jamaa huyu alikuwa X wangu wa zamani na hakuna taabu. mnakaa na kununuliana kahwa!! hata kukaribishana nyumbani!! Je sie a kina MAGANGA TUNAWEZA HAYO?? waswahili husema kisima ulichokunywa maji husahau- waweza kumbushia ati!!
wengine waendeleze na kumalizia.

Very well said. Halafu hizo za tulisoma naye, au jirani yetu tangu tukiwa wadogo ndio wanaweza kuwa wanamegana kiulaini sana! Bila hata kushtukiwa.

Ila kwa ujumla urafiki wa kawaida kati ya mwanamke na mwanamme ni vitu vya kawaida siku hizi. Watu wanatakiwa kubadilisha mtazamo wao katika maisha, kwa kuwa mambo yanabadilika kwa haraka sana!
 
mimi nafikiri wivu wa jinsi hiyo hata kina baba wanao, wewe mdada mtambulishe mkaka kwa mumeo/rafiki wa kiume kuwa alikuwa best wako enzi za arubaini na saba uone. kila ukiingia ndani ukitoka unakumbushwa hayo hayo hata kama huo urafiki was a normal siyo intimate relationship. Nafikiri ni issue ya insecurity ambayo wanadamu wengi wa/tumeumbwa nayo....
 
hii kitu mwanawane ipo kwa sana! hata wanaume wanayo...........utaambiwa 'hata kama rafiki yako ndo umpe smile la vile!', au hata kama mnajuana tokea watoto `ndo umsemeshe kwa sauti hiyo`.......wakati wewe umeona umemsalimia kikawaida tu.
 
Hii natatizo kubwa sana na ninahisi ni mazingira ya kumuachia mpenzi wako control nyingi bila kuweka limits.

Mimi mwenyewe wiki iliopita nilitumiwa msg kwenye simu kutukanwa na mpenzi wa best friend wangu.. Chaku shangaza ni kua mimi simfahamu na kaanza tukinitukana na wala haja take time kunifahamu kabla haja ni JUDGE... It is very sad....
 
Kukumbushia wanakumbushia hata wazee itakuwa watu waliotoka chuo juzi? Abiria lazima achunge mzigo wake
 
-Si wabongo tu,hata akina dada wa kihindi ni noma zaidi...yaani uwe wewe ni BF wake halafu akuone na dem wa kiafrika,basi noma.Atalia weee na unaweza kushinda ukimbembeleza,wengine hata wanaishia kujirusha maghorofani

Noma zaidi umwambie huyu ni Ex wangu halafu tena Mwafrika mwenzio
 
kwa hiyo tuna kila right kuwa defensive.......eh! Ben uko wapi nikununulie kahawa?
 
Back
Top Bottom